< Ezekieli 14 >
1 Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
Alors quelques-uns des anciens d'Israël vinrent à moi et s'assirent devant moi.
2 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de Yahvé me fut adressée, en ces termes:
3 “Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
« Fils d'homme, ces hommes ont pris leurs idoles dans leur cœur, et ils ont mis devant eux la pierre d'achoppement de leur iniquité. Faut-il que je sois interrogé par eux?
4 Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
Parle-leur donc et dis-leur: « Le Seigneur Yahvé dit: « Tout homme de la maison d'Israël qui prendra ses idoles dans son cœur et mettra la pierre d'achoppement de son iniquité devant sa face, et qui s'adressera au prophète, moi, Yahvé, je lui répondrai là selon la multitude de ses idoles,
5 Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
afin que je prenne la maison d'Israël dans son propre cœur, car ils se sont tous éloignés de moi par leurs idoles ».
6 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
« C'est pourquoi vous direz à la maison d'Israël: « Le Seigneur Yahvé dit: « Revenez et détournez-vous de vos idoles! Détournez vos visages de toutes vos abominations.
7 “‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
"''Car quiconque, de la maison d'Israël ou des étrangers qui habitent en Israël, se sépare de moi, prend ses idoles dans son cœur et met devant sa face la pierre d'achoppement de son iniquité, et vient trouver le prophète pour s'enquérir de moi, moi, Yahvé, je lui répondrai par moi-même.
8 Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Je tournerai ma face contre cet homme et j'en ferai un objet de désolation, un signe et un proverbe, et je le retrancherai du milieu de mon peuple. Alors vous saurez que je suis Yahvé.
9 “‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
"''Si le prophète est trompé et qu'il prononce une parole, moi, Yahvé, j'ai trompé ce prophète, j'étendrai ma main sur lui et je le ferai périr du milieu de mon peuple d'Israël.
10 Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
Ils porteront leur iniquité. L'iniquité du prophète sera comme l'iniquité de celui qui le cherche,
11 “‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
afin que la maison d'Israël ne s'éloigne plus de moi et ne se souille plus par toutes ses transgressions, mais qu'elle soit mon peuple et que je sois son Dieu, dit le Seigneur Yahvé.'"
12 Neno la Bwana likanijia kusema,
La parole de Yahvé me fut adressée, en ces termes:
13 “Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
« Fils d'homme, quand un pays péchera contre moi en commettant une infidélité, et que j'étendrai ma main sur lui, que je briserai le bâton de son pain, que j'enverrai la famine sur lui, et que j'en exterminerai les hommes et les bêtes -
14 hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
si ces trois hommes, Noé, Daniel et Job, s'y trouvaient, ils ne sauveraient que leur propre âme par leur justice », dit le Seigneur Yahvé.
15 “Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
« Si je fais passer des bêtes féroces dans le pays, et qu'elles le ravagent, et qu'il devienne désert, de sorte que personne ne puisse y passer à cause des bêtes -
16 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
si ces trois hommes y étaient, je suis vivant, dit le Seigneur Yahvé, ils ne délivreraient ni fils ni filles. Eux seuls seraient délivrés, mais le pays serait dévasté.
17 “Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
« Ou bien, si je fais venir l'épée sur ce pays, et que je dise: Epée, passe par le pays, et que j'en extermine les hommes et les bêtes,
18 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
si ces trois hommes y étaient, je suis vivant, dit le Seigneur Yahvé, ils ne délivreraient ni fils ni filles, mais ils seraient délivrés eux-mêmes.
19 “Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
« Si j'envoie la peste dans ce pays, et que je répande sur lui ma fureur dans le sang, pour en exterminer l'homme et l'animal -
20 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
quand Noé, Daniel et Job y seraient, je suis vivant, dit le Seigneur Yahvé, ils ne sauveraient ni fils ni fille, ils ne sauveraient que leur propre âme par leur justice. »
21 “Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
Car le Seigneur Yahvé dit: « Combien plus quand j'enverrai mes quatre jugements sévères sur Jérusalem - l'épée, la famine, les bêtes malfaisantes et la peste - pour en exterminer l'homme et l'animal!
22 Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
Mais voici, il restera en elle un reste qui sera emporté, des fils et des filles. Voici qu'ils sortiront vers toi, et tu verras leur conduite et leurs actes. Alors tu seras consolé du mal que j'ai fait venir sur Jérusalem, de tout ce que j'ai fait venir sur elle.
23 Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”
Ils te consoleront, quand tu verras leur conduite et leurs actes; alors tu sauras que je n'ai pas fait sans raison tout ce que j'ai fait en elle, dit le Seigneur Yahvé.