< Ezekieli 14 >
1 Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
Potom přišedše ke mně muži z starších Izraelských, seděli přede mnou.
2 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
I stalo se slovo Hospodinovo ke mně, řkoucí:
3 “Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
Synu člověčí, muži tito složili ukydané bohy své v srdci svém, a nepravost, kteráž jim k urážce jest, položili před tváři své. Zdaliž se upřímě radí se mnou?
4 Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
Protož mluv jim a rci jim: Takto praví Panovník Hospodin: Kdo by koli z domu Izraelského složil ukydané bohy své v srdci svém, a nepravost, kteráž mu k urážce jest, položil před tvář svou, a přišel by k proroku: já Hospodin odpovídati budu tomu, kterýž přišel, o množství ukydaných bohů jeho,
5 Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
Abych polapil dům Izraelský v srdci jejich, že se odvrátili ode mne k ukydaným bohům svým všickni napořád.
6 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
Protož rci domu Izraelskému: Takto praví Panovník Hospodin: Obraťte se a odvraťte od ukydaných bohů vašich, a ode všech ohavností vašich odvraťte tvář svou.
7 “‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
Nebo kdož by koli z domu Izraelského i z pohostinných, kteříž jsou pohostinu v Izraeli, odvrátil se od následování mne, a složil by ukydané bohy své v srdci svém, a nepravost, kteráž mu k urážce jest, položil by před tvář svou a přišel by k proroku, aby se mne tázal skrze něho: já Hospodin odpovím jemu o sobě,
8 Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
A obrátím tvář svou hněvivou proti muži tomu, a dám jej za znamení a za přísloví, a vytnu jej z prostřed lidu svého, i zvíte, že já jsem Hospodin.
9 “‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
Prorok pak, dal-li by se přivábiti, aby mluvil slovo, já Hospodin přivábil jsem proroka toho. Než vztáhnuť ruku svou na něj, a vyhladím jej z prostřed lidu svého Izraelského.
10 Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
A tak ponesou nepravost svou. Jakáž pokuta na toho, kdož by se tázal, takováž pokuta na proroka bude,
11 “‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
Aby nebloudili více dům Izraelský ode mne, a nepoškvrňovali se více žádnými převrácenostmi svými, aby byli lidem mým, a já abych byl jejich Bohem, praví Panovník Hospodin.
12 Neno la Bwana likanijia kusema,
Opět stalo se slovo Hospodinovo ke mně, řkoucí:
13 “Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
Synu člověčí, když by země zhřešila proti mně, dopouštějíc se přestoupení, tehdy vztáhl-li bych ruku svou na ni, a zlámal jí hůl chleba, a poslal bych na ni hlad, a vyhubil z ní lidi i hovada:
14 hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
By pak byli u prostřed ní tito tři muži, Noé, Daniel a Job, oni v spravedlnosti své vysvobodili by sami sebe, praví Panovník Hospodin.
15 “Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
Pakli bych zvěř lítou uvedl na zemi, tak že by ji na sirobu přivedla, a byla by pustá, aniž by kdo přes ni jíti mohl pro zvěř:
16 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
Živť jsem já, praví Panovník Hospodin, že byť tři muži tito u prostřed ní byli, nikoli by nevysvobodili synů ani dcer. Oni by sami vysvobozeni byli, země pak byla by pustá.
17 “Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
Aneb meč uvedl-li bych na zemi tu, a řekl bych meči: Projdi skrz zemi tu, abych vyhubil z ní lidi i hovada:
18 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
Živť jsem já, praví Panovník Hospodin, že byť pak tři muži tito byli u prostřed ní, nikoli by nevysvobodili synů ani dcer, ale oni sami by vysvobozeni byli.
19 “Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
Aneb mor poslal-li bych na zemi tu, a vylil prchlivost svou na ni k zhoubě, aby vyhlazeni byli z ní lidé i hovada:
20 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
Živť jsem já, praví Panovník Hospodin, že byť pak Noé, Daniel a Job u prostřed ní byli, nikoli by ani syna ani dcery nevysvobodili. Oni v spravedlnosti své vysvobodili by sami sebe.
21 “Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
Nýbrž takto praví Panovník Hospodin: Bych pak čtyři pokuty své zlé, meč a hlad, zvěř lítou a mor poslal na Jeruzalém, abych vyhubil z něho lidi i hovada,
22 Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
A aj, pozůstali-li by v něm, kteříž by toho ušli, a vyvedeni byli, synové neb dcery: aj, i oni musejí jíti k vám, a uzříte cestu jejich a skutky jejich, i potěšíte se nad tím zlým, kteréž uvedu na Jeruzalém, nade vším, což uvedu na něj.
23 Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”
A tak potěší vás, když uzříte cestu jejich a skutky jejich. I zvíte, že jsem ne nadarmo učinil všecko to, což jsem učinil při něm, praví Panovník Hospodin.