< Ezekieli 13 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
A palavra de Javé veio a mim, dizendo:
2 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
“Filho do homem, profetiza contra os profetas de Israel que profetizam, e diz àqueles que profetizam do próprio coração: 'Ouçam a palavra de Javé:
3 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
O Senhor Javé diz: “Ai dos profetas insensatos, que seguem seu próprio espírito e não viram nada!
4 Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
Israel, seus profetas têm sido como raposas nos lugares de desperdício.
5 Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
Você não subiu nas brechas ou construiu o muro para a casa de Israel, para permanecer na batalha no tempo de Iavé.
6 Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
Eles viram falsidade e adivinhação mentirosa, que dizem: 'Javé diz;' mas Javé não os enviou. Eles fizeram os homens esperarem que a palavra fosse confirmada.
7 Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
Você não viu uma visão falsa, e não falou uma adivinhação mentirosa, na qual você diz, 'Yahweh diz;' mas eu não falei?”.
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
“'Portanto, o Senhor Javé diz: “Porque falastes falsidade e vistes mentiras, portanto, eis que eu estou contra vós”, diz o Senhor Javé.
9 Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
“Minha mão será contra os profetas que vêem falsas visões e que proferem adivinhações mentirosas”. Eles não estarão no concílio do meu povo, nem serão escritos nos escritos da casa de Israel, nem entrarão na terra de Israel”. Então vocês saberão que eu sou o Senhor Javé”.
10 “‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
“'Porque, mesmo porque eles seduziram meu povo, dizendo: “Paz”; e não há paz. Quando se constrói um muro, eis que eles o rebocam com cal.
11 kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
Diga aos que a rebocam com cal que ela cairá. Haverá uma chuva transbordante; e vocês, grandes pedras de granizo, cairão. Um vento tempestuoso vai rasgá-lo.
12 Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
Quando o muro tiver caído, não lhe será dito: “Onde está o gesso com o qual você o rebocou?
13 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
“'Portanto, o Senhor Javé diz: “Eu vou até rasgá-lo com um vento tempestuoso em minha ira. Haverá uma chuva transbordante em minha ira, e grandes pedras de granizo na ira para consumi-la”.
14 Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Por isso, derrubarei a parede que vocês rebocaram com cal e a derrubarei, para que seus alicerces sejam descobertos”. Ela cairá, e você será consumido no meio dela. Então você saberá que eu sou Yahweh.
15 Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
Thus Realizarei minha ira sobre a parede, e sobre aqueles que a rebocaram com cal. Eu lhes direi: 'O muro não é mais, nem aqueles que o rebocaram -
16 wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
a saber, os profetas de Israel que profetizam a respeito de Jerusalém, e que vêem visões de paz para ela, e não há paz'”, diz o Senhor Javé”.
17 “Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
Você, filho do homem, põe seu rosto contra as filhas de seu povo, que profetizam do próprio coração; e profetiza contra elas,
18 na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
e diz: “O Senhor Javé diz: 'Ai das mulheres que cosem fitas mágicas em todos os cotovelos e fazem véus para a cabeça das pessoas de toda estatura para caçar almas! Vocês caçarão as almas do meu povo e salvarão as almas vivas para vocês mesmos?
19 Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
Vocês me profanaram entre meu povo por punhados de cevada e por pedaços de pão, para matar as almas que não deveriam morrer e para salvar as almas vivas que não deveriam viver, por suas mentiras ao meu povo que escuta as mentiras”.
20 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
“Portanto, o Senhor Javé diz: 'Eis que eu sou contra suas faixas mágicas, com as quais você caça as almas para fazê-las voar, e eu as arrancarei de seus braços'. Deixarei as almas voar livres, até mesmo as almas que vocês ludibriarem como pássaros”.
21 Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Também rasgarei seus véus e livrarei meu povo de suas mãos; e eles não estarão mais em suas mãos para serem ludibriados. Então você saberá que eu sou Yahweh.
22 Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
Porque com a mentira afligistes o coração do justo, que eu não entristeci; e fortalecestes as mãos do ímpio, para que ele não voltasse de seu mau caminho, e fosse salvo vivo.
23 kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
Portanto, não vereis mais falsas visões nem praticareis adivinhações. Eu livrarei meu povo de suas mãos. Então você saberá que eu sou Yahweh”.

< Ezekieli 13 >