< Ezekieli 13 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
2 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
Adresse tes prédictions aux prophètes d’Israël qui prophétisent, et tu diras à ceux qui prophétisent d’après leur cœur: Ecoutez la parole du Seigneur.
3 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Malheur aux prophètes insensés qui suivent leur esprit, et ne voient rien.
4 Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
Tes prophètes, Israël, étaient comme des renards dans les déserts.;
5 Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
Vous n’êtes pas montés à la rencontre de l’ennemi, vous n’avez pas opposé un mur pour la maison d’Israël, afin de tenir ferme dans le combat au jour du Seigneur.
6 Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
Ils voient des choses vaines, et ils prophétisent le mensonge, disant: Le Seigneur dit, lorsque le Seigneur ne les a pas envoyés; et ils persistent à maintenir leur discours.
7 Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
Est-ce que vous n’avez pas vu une vision vaine, et annoncé une prédiction mensongère? et vous dites: Le Seigneur dit, lorsque moi je n’ai pas parlé.
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Parce que vous avez dit des choses vaines, et que vous avez vu le mensonge; c’est pourquoi, voici que moi je suis contre vous, dit le Seigneur Dieu.
9 Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
Et ma main sera sur les prophètes qui voient des choses vaines, et qui prédisent le mensonge; ils ne seront pas dans le conseil de mon peuple, et ils ne seront point écrits dans le livre de la maison d’Israël, et ils n’entreront pas dans la terre d’Israël, et vous saurez que je suis le Seigneur Dieu;
10 “‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
Parce qu’ils ont trompé mon peuple, disant: Paix, et il n’y a point de paix; et lui bâtissait une muraille; mais eux l’enduisaient de boue, sans paille.
11 kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
Dis à ceux qui enduisent sans mélange, que la muraille tombera; car viendra une pluie inondante, et je lancerai des pierres énormes qui tomberont d’en haut, et un vent de tempête qui la renversera.
12 Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
Si toutefois la muraille tombe, ne vous dira-t-on pas: Où est l’enduit dont vous l’avez enduite?
13 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Je ferai éclater un vent de tempêtes dans mon indignation, et une pluie inondante se répandra dans ma fureur, et dans ma colère des pierres énormes consumeront tout.
14 Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Et je détruirai la muraille que vous avez enduite sans mélange; et je l’égalerai à la terre, et ses fondements seront mis à nu; et elle tombera; et celui qui l’avait enduite sera consumé au milieu d’elle; et vous saurez que moi je suis le Seigneur.
15 Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
Et j’assouvirai mon indignation contre la muraille, et contre ceux qui l’enduisent sans mélange, et je vous dirai: La muraille n’est plus, et ceux qui l’ont enduite ne sont plus.
16 wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
Ils ne sont plus, les prophètes d’Israël qui prophétisent à Jérusalem, et qui voient pour elle une vision de paix; et il n’y a point de paix, dit le Seigneur Dieu.
17 “Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
Et toi, fils d’un homme, tourne ta face contre les filles de ton peuple qui prophétisent d’après leur cœur, et fais des prédictions contre elles,
18 na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
Et dis: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Malheur à celles qui cousent des coussinets pour tous les coudes, et qui font des oreillers sous la tête des personnes de tout âge, afin de s’emparer des âmes; et lorsqu’elles s’emparaient des âmes de mon peuple, elles les vivifiaient.
19 Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
Elles me déshonoraient auprès de mon peuple pour un peu d’orge et un morceau de pain, afin de tuer les âmes qui n’étaient pas mortes, et de vivifier les âmes qui ne vivaient pas, mentant à mon peuple, qui croit aux mensonges.
20 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Voici que moi je suis contre vos coussinets avec lesquels vous prenez des âmes au vol, je les déchirerai de dessus vos bras, et je laisserai aller les âmes que vous avez prises, ces âmes pour qu’elles s’envolent.
21 Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Et je déchirerai vos oreillers; et je délivrerai mon peuple de votre main, et ils ne seront plus en vos mains comme une proie; et vous saurez que je suis le Seigneur,
22 Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
Parce que vous avez affligé en mentant le cœur du juste, que moi je n’ai pas contristé; et parce que vous avez fortifié les mains de l’impie, afin qu’il ne revînt point de sa voie mauvaise, et qu’il ne trouvât point la vie;
23 kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
À cause de cela, vous ne verrez plus de choses vaines, et vous ne ferez plus de prédictions, et j’arracherai mon peuple de votre main, et vous saurez que je suis le Seigneur.

< Ezekieli 13 >