< Ezekieli 13 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de Yahvé me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
Fils d'homme, prophétise contre les prophètes d'Israël qui prophétisent, et dis à ceux qui prophétisent de leur propre cœur: « Écoute la parole de Yahvé! »
3 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
Le Seigneur Yahvé dit: « Malheur aux prophètes insensés, qui suivent leur propre esprit, et qui n'ont rien vu!
4 Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
Israël, tes prophètes ont été comme des renards dans les lieux déserts.
5 Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
Vous n'êtes pas montés dans les brèches, vous n'avez pas bâti la muraille pour la maison d'Israël, pour être debout dans la bataille au jour de l'Éternel.
6 Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
Ils ont vu le mensonge et la divination mensongère, qui disent: « L'Éternel dit »; mais l'Éternel ne les a pas envoyés. Ils ont fait espérer aux hommes que la parole serait confirmée.
7 Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
N'avez-vous pas eu une vision fausse, et n'avez-vous pas parlé d'une divination mensongère, en disant: « Yahvé dit », mais je n'ai pas parlé? ».
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
"'C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: « Parce que vous avez dit des mensonges et vu des mensonges, voici, j'en veux à vous, dit le Seigneur Yahvé.
9 Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
« Ma main sera contre les prophètes qui ont des visions fausses et qui profèrent des divinations mensongères. Ils ne feront pas partie du conseil de mon peuple, ils ne seront pas inscrits dans les livres de la maison d'Israël, et ils n'entreront pas dans le pays d'Israël. Alors vous saurez que je suis le Seigneur Yahvé. »
10 “‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
"'Parce que, même parce qu'ils ont séduit mon peuple, en disant: « La paix », et il n'y a pas de paix. Quand on bâtit une muraille, voici qu'on la couvre de lait de chaux.
11 kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
Dis à ceux qui la recouvrent de lait de chaux qu'elle tombera. Il y aura une pluie débordante; et vous, grands grêlons, vous tomberez. Un vent de tempête la déchirera.
12 Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
Voici, quand la muraille sera tombée, ne vous dira-t-on pas: « Où est l'enduit avec lequel vous l'avez plâtrée? »
13 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
"'C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: « Je la déchirerai même par un vent de tempête dans ma colère. Il y aura une pluie débordante dans ma colère, et de grosses pierres de grêle dans ma fureur pour la consumer.
14 Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
J'abattrai la muraille que tu as enduite de lait de chaux, je la ferai tomber à terre, et ses fondements seront découverts. Elle tombera, et vous serez consumés au milieu d'elle. Alors vous saurez que je suis Yahvé.
15 Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
J'accomplirai ainsi ma colère contre la muraille et contre ceux qui l'ont enduite de chaux. Je vous dirai: « La muraille n'est plus, ni ceux qui l'ont enduite de chaux,
16 wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
c'est-à-dire les prophètes d'Israël qui prophétisent sur Jérusalem, et qui ont des visions de paix pour elle, et il n'y a pas de paix », dit le Seigneur Yahvé ».
17 “Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
Toi, fils de l'homme, tourne ta face vers les filles de ton peuple, qui prophétisent de leur propre cœur; prophétise contre elles,
18 na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
et dis: « Le Seigneur Yahvé dit: « Malheur aux femmes qui cousent des bandes magiques à tous les coudes et font des voiles à la tête des personnes de toute taille pour chasser les âmes! Allez-vous chasser les âmes de mon peuple et garder pour vous des âmes vivantes?
19 Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
Vous m'avez profané parmi mon peuple pour des poignées d'orge et pour des morceaux de pain, pour tuer les âmes qui ne devraient pas mourir et pour sauver les âmes vivantes qui ne devraient pas vivre, par vos mensonges à mon peuple qui écoute les mensonges.''
20 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
« C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: 'Voici que j'en veux à vos bandes magiques, avec lesquelles vous chassez les âmes pour les faire voler, et je les arracherai de vos bras. Je laisserai les âmes voler librement, même celles que vous prenez au piège comme des oiseaux.
21 Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Je déchirerai aussi vos voiles et je délivrerai mon peuple de vos mains; il ne sera plus entre vos mains pour être pris au piège. Alors vous saurez que je suis Yahvé.
22 Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
Car c'est par le mensonge que vous avez attristé le cœur du juste, que je n'ai pas attristé, et que vous avez fortifié les mains du méchant, afin qu'il ne revienne pas de sa mauvaise voie et qu'il soit sauvé vivant.
23 kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
C'est pourquoi vous ne verrez plus de visions trompeuses et ne pratiquerez plus la divination. Je délivrerai mon peuple de ta main. Alors vous saurez que je suis Yahvé.'"