< Ezekieli 13 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord came to me, saying:
2 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
“Son of man, prophesy to the prophets of Israel who are prophesying, and you shall say to those who prophesy from their own heart: Hear the word of the Lord:
3 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
Thus says the Lord God: Woe to the foolish prophets, who are following their own spirit, and who see nothing.
4 Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
Your prophets, O Israel, were like foxes in the deserts.
5 Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
You have not gone up against the adversary, and you have not established a wall for the house of Israel, so as to stand in battle on the day of the Lord.
6 Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
They see emptiness, and they foretell falsehoods, saying, ‘The Lord says,’ though the Lord has not sent them. And they continued to affirm what they said.
7 Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
Have you not seen a futile vision and spoken a lying divination? And yet you say, ‘The Lord says,’ though I have not spoken.
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
Because of this, thus says the Lord God: Since you have spoken emptiness and have seen falsehoods, therefore: behold, I am against you, says the Lord God.
9 Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
And my hand will be over the prophets who are seeing emptiness and divining lies. They shall not be in the council of my people, and they shall not be written in the writing of the house of Israel. Neither shall they enter into the land of Israel. And you shall know that I am the Lord God.
10 “‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
For they have deceived my people, saying, ‘Peace,’ and there is no peace. And they have built a wall, but they have covered it in clay without straw.
11 kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
Say to those who spread mortar without mixing, that it will fall apart. For there will be an inundating rain, and I will cause full-grown hailstones to rush down from above, and a windstorm to dissipate it.
12 Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
So then, behold: when the wall has fallen, will it not be said to you: ‘Where is the mortar with which you covered it?’
13 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
Because of this, thus says the Lord God: And I will cause a violent wind to burst forth in my indignation, and there will be an inundating rain in my fury, and great hailstones in wrath, to consume.
14 Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
And I will destroy the wall that you have covered without tempering it. And I will level it to the ground, and its foundation will be revealed. And it will fall and be consumed in its midst. And you shall know that I am the Lord.
15 Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
And I will fulfill my indignation against the wall, and against those who cover it without mixing the mortar, and I will say to you: The wall is no more, and those who covered it are no more:
16 wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
the prophets of Israel, who prophesy to Jerusalem, and who see visions of peace for her when there is no peace, says the Lord God.
17 “Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
And as for you, son of man, set your face against the daughters of your people, who prophesy from their own heart. And prophesy about them,
18 na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
and say: Thus says the Lord God: Woe to those who sew together little pillows under every forearm, and who make little cushions for the heads of every stage of life, in order to capture souls. And when they have seized the souls of my people, they became the life of their souls.
19 Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
And they violated me among my people, for the sake of a handful of barley and a fragment of bread, so that they would kill the souls that should not die, and enliven the souls that should not live, lying to my people who believe in falsehoods.
20 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
Because of this, thus says the Lord God: Behold, I am against your little pillows, with which you catch flying souls. And I will tear them away from your arms. And I will release the souls that you are capturing, the souls that should fly.
21 Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
And I will tear away your little cushions. And I will free my people from your hand. And they shall no longer be a prey in your hands. And you shall know that I am the Lord.
22 Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
For by deception you have caused the heart of the just to grieve, whom I would not sadden. And I have strengthened the hands of the impious, so that he would not be turned back from his evil way and live.
23 kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
Therefore, you shall not see emptiness, and you shall not divine divinations, any more. And I will rescue my people from your hand. And you shall know that I am the Lord.”

< Ezekieli 13 >