< Ezekieli 13 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
I stalo se slovo Hospodinovo ke mně, řkoucí:
2 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
Synu člověčí, prorokuj proti prorokům Izraelským, kteříž prorokují, a rci prorokujícím z srdce svého: Slyšte slovo Hospodinovo:
3 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
Takto praví Panovník Hospodin: Běda prorokům bláznivým, kteříž následují ducha svého, ješto však nic neviděli.
4 Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
Podobni jsou liškám na pustinách proroci tvoji, Izraeli.
5 Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
Nevstupujete k mezerám, aniž děláte hradby okolo domu Izraelského, aby ostáti mohl v boji v den Hospodinův.
6 Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
Vídají marnost a hádání lživé. Říkají: Praví Hospodin, ješto jich neposlal Hospodin, a troštují lidi, aby jen utvrdili slovo své.
7 Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
Zdaliž vidění marného nevídáte, a hádání lživého nevypravujete? A říkáte: Praví Hospodin, ješto jsem já nemluvil.
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
Pročež takto praví Panovník Hospodin: Proto že mluvíte marnost, a vídáte lež, protož aj, já jsem proti vám, praví Panovník Hospodin.
9 Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
Nebo bude ruka má proti prorokům, kteříž vídají marnost a hádají lež. V losu lidu mého nebudou, a v popisu domu Izraelského nebudou zapsáni, aniž do země Izraelské vejdou. I zvíte, že já jsem Panovník Hospodin,
10 “‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
Proto, proto že v blud uvedli lid můj, říkajíce: Pokoj, ješto nebylo žádného pokoje. Jeden zajisté ustavěl stěnu hliněnou, a jiní obmítali ji vápnem ničemným.
11 kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
Rciž těm, kteříž obmítají vápnem ničemným: I však to padne. Přijde příval rozvodnilý, a vy, kamenové krupobití velikého, spadnete, a vítr bouřlivý roztrhne ji.
12 Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
A aj, když padne ta stěna, zdaliž vám nebude řečeno: Kdež jest to obmítání, jímž jste obmítali?
13 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
Protož takto praví Panovník Hospodin: Roztrhnu ji, pravím, větrem bouřlivým v prchlivosti své, a příval rozvodnilý v hněvě mém přijde, a kamení krupobití velikého v prchlivosti mé k vyhlazení jí.
14 Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Nebo rozbořím stěnu tu, kterouž jste obmetali vápnem ničemným, a porazím ji na zem, tak že odkryt bude grunt její. I padne, a zkaženi budete u prostřed ní, a zvíte, že já jsem Hospodin.
15 Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
A tak vykonaje prchlivost svou na té stěně, a na těch, kteříž ji obmítají vápnem ničemným, dím vám: Není více té stěny, není ani těch, kteříž ji obmítali,
16 wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
Totiž proroků Izraelských, kteříž prorokují Jeruzalému, a ohlašují jemu vidění pokoje, ješto není žádného pokoje, praví Panovník Hospodin.
17 “Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
Ty pak, synu člověčí, obrať tvář svou k dcerám lidu svého, kteréž prorokují z srdce svého, a prorokuj i proti nim.
18 na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
A rci: Takto praví Panovník Hospodin: Běda těm, kteréž šijí polštáříky pod všeliké lokty rukou lidu mého, a dělají kukly na hlavu všeliké postavy, aby lovily duše. Zdaliž loviti máte duše lidu mého, abyste se živiti mohly?
19 Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
Nebo zlehčujete mne u lidu mého pro hrst ječmene a pro kus chleba, umrtvujíce duše, kteréž neumrou, a obživujíce duše, kteréž živy nebudou, lhouce lidu mému, kteříž poslouchají lži.
20 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
Protož takto praví Panovník Hospodin: Aj, já dám se v polštáříky vaše, jimiž vy lovíte tam duše, abyste je oklamaly. Nebo strhnu je s ramenou vašich, a propustím duše, duše, kteréž vy lovíte, abyste je oklamaly.
21 Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
I strhnu kukly vaše, a vytrhnu lid svůj z ruky vaší, tak abyste jich nemohly více loviti, i zvíte, že já jsem Hospodin;
22 Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
Proto že kormoutíte srdce spravedlivého lžmi, ješto jsem já ho nekormoutil, a posilujete rukou bezbožného, aby se neodvrátil od zlé cesty své, obživujíce jej.
23 kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
Protož nebudete vídati marnosti, a s hádáním nebudete se obírati více; nebo vytrhnu lid svůj z ruky vaší, i zvíte, že já jsem Hospodin.

< Ezekieli 13 >