< Ezekieli 12 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
2 “Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.
Fils d’homme, tu demeures au milieu d’une maison rebelle; ils ont des yeux pour voir, et ne voient pas; ils ont des oreilles pour entendre, et n’entendent pas; car ils sont une maison rebelle.
3 “Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi.
Et toi, fils d’homme, fais-toi un bagage de transporté, et va captif, de jour, sous leurs yeux; va captif, de ton lieu vers un autre lieu, sous leurs yeux; peut-être verront-ils, car ils sont une maison rebelle.
4 Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni.
Et, de jour, tu mettras dehors ton bagage, comme un bagage de transporté, sous leurs yeux; et toi, tu sortiras sur le soir, devant leurs yeux, comme ceux qui s’en vont en captivité.
5 Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.
Perce le mur sous leurs yeux, et mets dehors par là [ton bagage];
6 Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.”
tu le porteras sur l’épaule, sous leurs yeux; tu le mettras dehors dans l’obscurité; tu couvriras ta face, et tu ne verras pas le pays, car je t’ai donné pour signe à la maison d’Israël.
7 Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama.
Et je fis comme il m’avait été commandé: je sortis de jour mon bagage, comme un bagage de transporté, et, sur le soir, je perçai le mur avec la main: je le mis dehors dans l’obscurité, je le portai sur l’épaule, sous leurs yeux.
8 Asubuhi neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à moi, le matin, disant:
9 “Mwanadamu, je, nyumba ile ya kuasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’
Fils d’homme, la maison d’Israël, la maison rebelle, ne t’a-t-elle pas dit: Que fais-tu?
10 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Neno hili linamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ambao wako huko.’
Dis-leur: Ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Cet oracle [concerne] le prince qui est dans Jérusalem, et toute la maison d’Israël qui est au milieu d’eux.
11 Waambie, ‘Mimi ndiye ishara kwenu.’ “Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Watakwenda uhamishoni kama mateka.
Dis: Je suis pour vous un signe; comme j’ai fait, ainsi il leur sera fait: ils iront en exil [et] en captivité.
12 “Naye mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani mwake kwenye giza la jioni na kuondoka na tundu litatobolewa ukutani kwa ajili yake ili kupitia hapo. Atafunika uso wake ili kwamba asiweze kuiona nchi.
Et le prince qui est au milieu d’eux portera [son bagage] sur l’épaule, dans l’obscurité, et sortira; on percera le mur pour le faire sortir par là; il couvrira sa face, afin qu’il ne voie pas de ses yeux le pays.
13 Nitatandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa kwenye mtego wangu, nitamleta mpaka Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko.
Et j’étendrai sur lui mon filet, et il sera pris dans mon piège; et je l’amènerai à Babylone, dans le pays des Chaldéens; mais il ne le verra point, et là il mourra.
14 Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote, watumishi wake na majeshi yake yote, nami nitawafuatilia kwa upanga uliofutwa.
Et tout ce qui l’entoure, son secours, et toutes ses troupes, je les disperserai à tout vent; et je tirerai l’épée après eux.
15 “Wao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
Et ils sauront que je suis l’Éternel, quand je les aurai dispersés parmi les nations et que je les aurai disséminés dans les pays.
16 Lakini nitawaacha wachache wao waokoke na upanga, njaa na tauni, ili kwamba katika mataifa watakakokwenda waweze kutambua matendo ya machukizo waliotenda. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
Et je laisserai de reste d’entre eux quelque peu de gens [sauvés] de l’épée, de la famine et de la peste, afin qu’ils racontent toutes leurs abominations parmi les nations où ils seront venus. Et ils sauront que je suis l’Éternel.
17 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
18 “Mwanadamu, tetemeka wakati ulapo chakula chako, tetemeka kwa hofu wakati unywapo maji yako.
Fils d’homme, mange ton pain dans le trouble, et bois ton eau avec tremblement et dans l’inquiétude;
19 Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu hao wanaoishi Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyangʼanywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo.
et dis au peuple du pays: Ainsi dit le Seigneur, l’Éternel, touchant les habitants de Jérusalem, sur la terre d’Israël: Ils mangeront leur pain avec inquiétude et ils boiront leur eau avec stupeur, parce que leur pays sera désolé, [vide] de tout ce qu’il contient, à cause de la violence de tous ceux qui l’habitent;
20 Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.’”
et les villes habitées seront rendues désertes, et le pays sera une désolation; et vous saurez que je suis l’Éternel.
21 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
22 “Mwanadamu, ni nini hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia?’
Fils d’homme, quel est ce proverbe que vous avez dans la terre d’Israël, disant: Les jours seront prolongés, et toute vision a péri?
23 Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia wakati kila maono yatakapotimizwa.
C’est pourquoi dis-leur: Ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Je ferai cesser ce proverbe, et on ne s’en servira plus comme proverbe en Israël; mais dis-leur: Les jours se sont approchés, et l’accomplissement de chaque vision;
24 Kwa maana hapatakuwepo tena na maono ya uongo wala ubashiri wa udanganyifu miongoni mwa watu wa Israeli.
car il n’y aura plus aucune vision vaine, ni divination flatteuse, au milieu de la maison d’Israël.
25 Lakini Mimi Bwana nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa maana katika siku zako, wewe nyumba ya kuasi, nitatimiza kila nisemalo, asema Bwana Mwenyezi.’”
Car moi, je suis l’Éternel; je parlerai, et la parole que j’aurai dite sera exécutée, elle ne sera plus différée; car en vos jours, maison rebelle, je dirai une parole et je l’exécuterai, dit le Seigneur, l’Éternel.
26 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à moi, disant:
27 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’
Fils d’homme, voici, la maison d’Israël dit: La vision que celui-ci voit est pour des jours lointains, et il prophétise pour des temps éloignés.
28 “Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema Bwana Mwenyezi.’”
C’est pourquoi dis-leur: Ainsi dit le Seigneur, l’Éternel: Aucune de mes paroles ne sera plus différée; la parole que j’aurai dite sera exécutée, dit le Seigneur, l’Éternel.

< Ezekieli 12 >