< Ezekieli 12 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord was maad to me,
2 “Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.
and he seide, Sone of man, thou dwellist in the myddis of an hous terrynge to wraththe, which han iyen to se, and seen not, and eeris to here, and heren not; for it is an hous terrynge to wraththe.
3 “Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi.
Therfor thou, sone of man, make to thee vessels of passing ouer, and thou schalt passe ouer bi dai bifor hem; forsothe thou schalt passe ouer fro thi place to another place, in the siyt of hem, if perauenture thei biholden, for it is an hous terrynge to wraththe.
4 Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni.
And thou schalt bere withoutforth thi vessels, as the vessels of a man passynge ouer bi dai, in the siyt of hem; sotheli thou schalt go out in the euentid bifore hem, as a man passynge forth goith out.
5 Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.
Bifore the iyen of hem digge the wal to thee, and thou
6 Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.”
schalt go out thorouy it in the siyt of hem. Thou schalt be borun on schuldris, thou schalt be borun out in derknesse; thou schalt hile thi face, and thou schalt not se the erthe, for Y haue youe thee a signe
7 Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama.
of thing to comynge to the hous of Israel. Therfor Y dide as the Lord comaundide to me; Y brouyte forth my vessels, as the vessels of a man passynge ouer bi dai, and in the euentid Y diggide a wal to me with hond; Y yede out in derknesse, and Y was borun on schuldris,
8 Asubuhi neno la Bwana likanijia kusema:
in the siyt of hem. And the word of the Lord was maad eerli to me,
9 “Mwanadamu, je, nyumba ile ya kuasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’
and he seide, Sone of man, whether the hous of Israel, the hous terrynge to wraththe, seiden not to thee, What doist thou?
10 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Neno hili linamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ambao wako huko.’
Seie thou to hem, The Lord God seith these thingis, This birthun is on the duyk, which is in Jerusalem, and on al the hous of Israel, which is in the myddis of hem.
11 Waambie, ‘Mimi ndiye ishara kwenu.’ “Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Watakwenda uhamishoni kama mateka.
Seie thou, Y am youre signe of thing to comynge; as Y dide, so it schal be don to hem; thei schulen go in to passynge ouer, and in to caitifte.
12 “Naye mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani mwake kwenye giza la jioni na kuondoka na tundu litatobolewa ukutani kwa ajili yake ili kupitia hapo. Atafunika uso wake ili kwamba asiweze kuiona nchi.
And the duyk which is in the myddis of hem, schal be borun out on schuldris, and he schal go out in derknesse; thei schulen digge the wal, and lede hym out; his face schal be hilid, that he se not with iye the erthe.
13 Nitatandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa kwenye mtego wangu, nitamleta mpaka Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko.
And Y schal stretche forth my net on hym, and he schal be takun in my net; and Y schal lede hym in to Babiloyne, in to the lond of Caldeis, and he schal not se that lond, and he schal die there.
14 Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote, watumishi wake na majeshi yake yote, nami nitawafuatilia kwa upanga uliofutwa.
And Y schal scatere in to ech wynd alle men that ben aboute hym, his help, and hise cumpenyes; and Y schal draw out the swerd aftir hem.
15 “Wao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
And thei schulen wite, that Y am the Lord, whanne Y schal scatere hem among hethene men, and schal sowe hem abrood in londis.
16 Lakini nitawaacha wachache wao waokoke na upanga, njaa na tauni, ili kwamba katika mataifa watakakokwenda waweze kutambua matendo ya machukizo waliotenda. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
And Y schal leue of hem a fewe men fro swerd, and hungur, and pestilence, that thei telle out alle the grete trespassis of hem among hethene men, to which thei schulen entre; and thei schulen wite, that Y am the Lord.
17 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord was maad to me,
18 “Mwanadamu, tetemeka wakati ulapo chakula chako, tetemeka kwa hofu wakati unywapo maji yako.
and he seide, Thou, sone of man, ete thi breed in disturblyng, but also drynke thi water in haaste and mourening.
19 Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu hao wanaoishi Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyangʼanywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo.
And thou schalt seie to the puple of the lond, The Lord God seith these thingis to hem that dwellen in Jerusalem, in the lond of Israel, Thei schulen ete her breed in angwisch, and thei schulen drynke her watir in desolacioun; that the lond be desolat of his multitude, for the wickidnesse of alle men that dwellen ther ynne.
20 Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.’”
And citees that ben now enhabitid, shulen be desolat, and the lond schal be forsakun; and ye schulen wite, that Y am the Lord.
21 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord was maad to me,
22 “Mwanadamu, ni nini hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia?’
and he seide, Sone of man, what is this prouerbe to you, of men seiynge in the lond of Israel, Daies schulen be differrid in to long tyme, and ech visioun shal perische?
23 Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia wakati kila maono yatakapotimizwa.
Therfor seie thou to hem, The Lord God seith these thingis, Y schal make this prouerbe to ceesse, and it schal no more be seid comynli in Israel; and speke thou to hem, that the daies han neiyid, and ech word of profesie.
24 Kwa maana hapatakuwepo tena na maono ya uongo wala ubashiri wa udanganyifu miongoni mwa watu wa Israeli.
For whi ech visioun schal no more be voide, nether bifor tellyng of thing to comynge schal be douteful in the myddis of the sones of Israel;
25 Lakini Mimi Bwana nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa maana katika siku zako, wewe nyumba ya kuasi, nitatimiza kila nisemalo, asema Bwana Mwenyezi.’”
for Y the Lord schal speke what euer word Y schal speke, and it schal be don; it schal no more be delaied, but in youre daies, ye hous terrynge to wraththe, Y schal speke a word, and Y schal do that word, seith the Lord God.
26 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord was maad to me, and he seide, Thou,
27 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’
sone of man, lo! the hous of Israel, of hem that seien, The visioun which this man seeth, is in to manye daies, and this man profesieth in to longe tymes.
28 “Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema Bwana Mwenyezi.’”
Therfor seie thou to hem, The Lord God seith these thingis, Ech word of me schal no more be deferrid; the word which Y schal speke, schal be fillid, seith the Lord God.

< Ezekieli 12 >