< Ezekieli 12 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
and to be word LORD to(wards) me to/for to say
2 “Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.
son: child man in/on/with midst house: household [the] rebellion you(m. s.) to dwell which eye to/for them to/for to see: see and not to see: see ear to/for them to/for to hear: hear and not to hear: hear for house: household rebellion they(masc.)
3 “Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi.
and you(m. s.) son: child man to make to/for you article/utensil captivity and to reveal: remove by day to/for eye: seeing their and to reveal: remove from place your to(wards) place another to/for eye: seeing their perhaps to see: examine for house: household rebellion they(masc.)
4 Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni.
and to come out: send article/utensil your like/as article/utensil captivity by day to/for eye: seeing their and you(m. s.) to come out: come in/on/with evening to/for eye: seeing their like/as exit captivity
5 Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.
to/for eye: seeing their to dig to/for you in/on/with wall and to come out: send in/on/with him
6 Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.”
to/for eye: seeing their upon shoulder to lift: raise in/on/with darkness to come out: send face your to cover and not to see: see [obj] [the] land: country/planet for wonder to give: make you to/for house: household Israel
7 Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama.
and to make: do so like/as as which to command article/utensil my to come out: send like/as article/utensil captivity by day and in/on/with evening to dig to/for me in/on/with wall in/on/with hand in/on/with darkness to come out: send upon shoulder to lift: bear to/for eye: seeing their
8 Asubuhi neno la Bwana likanijia kusema:
and to be word LORD to(wards) me in/on/with morning to/for to say
9 “Mwanadamu, je, nyumba ile ya kuasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’
son: child man not to say to(wards) you house: household Israel house: household [the] rebellion what? you(m. s.) to make: do
10 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Neno hili linamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ambao wako huko.’
to say to(wards) them thus to say Lord YHWH/God [the] leader [the] oracle [the] this in/on/with Jerusalem and all house: household Israel which they(masc.) in/on/with midst their
11 Waambie, ‘Mimi ndiye ishara kwenu.’ “Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Watakwenda uhamishoni kama mateka.
to say I wonder your like/as as which to make: do so to make: do to/for them in/on/with captivity in/on/with captivity to go: went
12 “Naye mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani mwake kwenye giza la jioni na kuondoka na tundu litatobolewa ukutani kwa ajili yake ili kupitia hapo. Atafunika uso wake ili kwamba asiweze kuiona nchi.
and [the] leader which in/on/with midst their to(wards) shoulder to lift: raise in/on/with darkness and to come out: come in/on/with wall to dig to/for to come out: send in/on/with him face his to cover because which not to see: see to/for eye he/she/it [obj] [the] land: country/planet
13 Nitatandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa kwenye mtego wangu, nitamleta mpaka Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko.
and to spread [obj] net my upon him and to capture in/on/with net my and to come (in): bring [obj] him Babylon [to] land: country/planet Chaldea and [obj] her not to see: see and there to die
14 Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote, watumishi wake na majeshi yake yote, nami nitawafuatilia kwa upanga uliofutwa.
and all which around him (helper his *Q(K)*) and all band his to scatter to/for all spirit: breath and sword to empty after them
15 “Wao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
and to know for I LORD in/on/with to scatter I [obj] them in/on/with nation and to scatter [obj] them in/on/with land: country/planet
16 Lakini nitawaacha wachache wao waokoke na upanga, njaa na tauni, ili kwamba katika mataifa watakakokwenda waweze kutambua matendo ya machukizo waliotenda. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
and to remain from them human number from sword from famine and from pestilence because to recount [obj] all abomination their in/on/with nation which to come (in): come there and to know for I LORD
17 Neno la Bwana likanijia kusema:
and to be word LORD to(wards) me to/for to say
18 “Mwanadamu, tetemeka wakati ulapo chakula chako, tetemeka kwa hofu wakati unywapo maji yako.
son: child man food: bread your in/on/with quaking to eat and water your in/on/with quivering and in/on/with anxiety to drink
19 Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu hao wanaoishi Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyangʼanywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo.
and to say to(wards) people [the] land: country/planet thus to say Lord YHWH/God to/for to dwell Jerusalem to(wards) land: soil Israel food: bread their in/on/with anxiety to eat and water their in/on/with horror to drink because be desolate land: country/planet her from fullness her from violence all [the] to dwell in/on/with her
20 Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.’”
and [the] city [the] to dwell to destroy and [the] land: country/planet devastation to be and to know for I LORD
21 Neno la Bwana likanijia kusema:
and to be word LORD to(wards) me to/for to say
22 “Mwanadamu, ni nini hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia?’
son: child man what? [the] proverb [the] this to/for you upon land: soil Israel to/for to say to prolong [the] day and to perish all vision
23 Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia wakati kila maono yatakapotimizwa.
to/for so to say to(wards) them thus to say Lord YHWH/God to cease [obj] [the] proverb [the] this and not to use a proverb [obj] him still in/on/with Israel that if: except if: except to speak: speak to(wards) them to present: come [the] day and word: promised all vision
24 Kwa maana hapatakuwepo tena na maono ya uongo wala ubashiri wa udanganyifu miongoni mwa watu wa Israeli.
for not to be still all vision vanity: false and divination smooth in/on/with midst house: household Israel
25 Lakini Mimi Bwana nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa maana katika siku zako, wewe nyumba ya kuasi, nitatimiza kila nisemalo, asema Bwana Mwenyezi.’”
for I LORD to speak: speak [obj] which to speak: speak word and to make: do not to draw still for in/on/with day your house: household [the] rebellion to speak: speak word and to make: do him utterance Lord YHWH/God
26 Neno la Bwana likanijia kusema:
and to be word LORD to(wards) me to/for to say
27 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’
son: child man behold house: household Israel to say [the] vision which he/she/it to see to/for day many and to/for time distant he/she/it to prophesy
28 “Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema Bwana Mwenyezi.’”
to/for so to say to(wards) them thus to say Lord YHWH/God not to draw still all word my which to speak: speak word and to make: do utterance Lord YHWH/God

< Ezekieli 12 >