< Ezekieli 11 >

1 Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
و روح مرا برداشته، به دروازه شرقی خانه خداوند که بسوی مشرق متوجه است آورد. و اینک نزد دهنه دروازه بیست و پنج مرد بودند و در میان ایشان یازنیا ابن عزور و فلطیاابن بنایا روسای قوم را دیدم.۱
2 Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
و او مرا گفت: «ای پسر انسان اینها آن کسانی می‌باشند که تدابیرفاسد می‌کنند و در این شهر مشورتهای قبیح می‌دهند.۲
3 Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
و می‌گویند وقت نزدیک نیست که خانه‌ها را بنا نماییم، بلکه این شهر دیگ است و ما گوشت می‌باشیم.۳
4 Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
بنابراین برای ایشان نبوت کن. ای پسر انسان نبوت کن.»۴
5 Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
آنگاه روح خداوند بر من نازل شده، مرافرمود: «بگو که خداوند چنین می‌فرماید: ای خاندان اسرائیل شما به اینطور سخن می‌گویید واما من خیالات دل شما را می‌دانم.۵
6 Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
بسیاری را دراین شهر کشته‌اید و کوچه هایش را از کشتگان پرکرده‌اید.۶
7 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
لهذا خداوند یهوه چنین می‌گوید: کشتگان شما که در میانش گذاشته‌اید، گوشت می‌باشند و شهر دیگ است. لیکن شما را ازمیانش بیرون خواهم برد.۷
8 Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
شما از شمشیرمی ترسید، اما خداوند یهوه می‌گوید شمشیر را برشما خواهم آورد.۸
9 Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
و شما را از میان شهر بیرون برده، شما را به‌دست غریبان تسلیم خواهم نمودو بر شما داوری خواهم کرد.۹
10 Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
به شمشیرخواهید افتاد و در حدود اسرائیل بر شما داوری خواهم نمود و خواهید دانست که من یهوه هستم.۱۰
11 Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
این شهر برای شما دیگ نخواهد بود و شما درآن گوشت نخواهید بود، بلکه در حدود اسرائیل بر شما داوری خواهم نمود.۱۱
12 Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
و خواهید دانست که من آن یهوه هستم که در فرایض من سلوک ننمودید و احکام مرا بجا نیاوردید، بلکه برحسب احکام امت هایی که به اطراف شمامی باشند عمل نمودید.»۱۲
13 Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
و واقع شد که چون نبوت کردم، فلطیا ابن بنایا مرد. پس به روی خوددر‌افتاده، به آواز بلند فریاد نمودم و گفتم: «آه‌ای خداوند یهوه آیا تو بقیه اسرائیل را تمام هلاک خواهی ساخت؟»۱۳
14 Neno la Bwana likanijia kusema:
و کلام خداوند بر من نازل شده، گفت:۱۴
15 “Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
«ای پسر انسان برادران تو یعنی برادرانت که از اهل خاندان تو می‌باشند و تمامی خاندان اسرائیل جمیع کسانی می‌باشند که سکنه اورشلیم به ایشان می‌گویند: شما از خداوند دورشوید و این زمین به ما به ملکیت داده شده است.۱۵
16 “Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
بنابراین بگو: خداوند یهوه چنین می‌گوید: اگرچه ایشان را در میان امت‌ها دور کنم و ایشان را درمیان کشورها پراکنده سازم، اما من برای ایشان درآن کشورهایی که به آنها رفته باشند اندک زمانی مقدس خواهم بود.۱۶
17 “Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
پس بگو خداوند یهوه چنین می‌فرماید: شما را از میان امت‌ها جمع خواهم کرد و شما را از کشورهایی که در آنهاپراکنده شده‌اید فراهم خواهم آورد و زمین اسرائیل را به شما خواهم داد.۱۷
18 “Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
و به آنجا داخل شده، تمامی مکروهات و جمیع رجاسات آن رااز میانش دور خواهند کرد.۱۸
19 Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
و ایشان را یکدل خواهم داد و در اندرون ایشان روح تازه خواهم نهاد و دل سنگی را از جسد ایشان دور کرده، دل گوشتی به ایشان خواهم بخشید.۱۹
20 Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
تا در فرایض من سلوک نمایند و احکام مرا نگاه داشته، آنها رابجا آورند. و ایشان قوم من خواهند بود و من خدای ایشان خواهم بود.۲۰
21 Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
اما آنانی که دل ایشان از عقب مکروهات و رجاسات ایشان می‌رود، پس خداوند یهوه می‌گوید: من رفتارایشان را بر سر ایشان وارد خواهم آورد.»۲۱
22 Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
آنگاه کروبیان بالهای خود را برافراشتند وچرخها به پهلوی ایشان بود و جلال خدای اسرائیل از طرف بالا بر ایشان قرار گرفت.۲۲
23 Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
وجلال خداوند از بالای میان شهر صعود نموده، برکوهی که بطرف شرقی شهر است قرار گرفت.۲۳
24 Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
و روح مرا برداشت و در عالم رویا مرا به روح خدا به زمین کلدانیان نزد اسیران برد و آن رویایی که دیده بودم از نظر من مرتفع شد.۲۴
25 nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.
و تمامی کلام خداوند را که به من نشان داده بود، برای اسیران بیان کردم.۲۵

< Ezekieli 11 >