< Ezekieli 11 >

1 Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
L'Esprit me souleva et me conduisit à la porte orientale de la maison de Yahvé, qui donne sur l'orient. Et voici, vingt-cinq hommes étaient à l'entrée de la porte. Je vis parmi eux Jaazania, fils d'Azzur, et Pelatia, fils de Benaja, chefs du peuple.
2 Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
Il me dit: « Fils de l'homme, ce sont là des hommes qui méditent l'iniquité et qui donnent de mauvais conseils dans cette ville,
3 Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
qui disent: Le temps n'est pas encore venu de bâtir des maisons. C'est ici le chaudron, et nous sommes la viande ».
4 Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
C`est pourquoi prophétise contre eux. Prophétise, fils de l'homme. »
5 Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
L'Esprit de Yahvé tomba sur moi, et il me dit: « Parle. Yahvé dit: « C'est ainsi que vous avez parlé, maison d'Israël, car je sais ce qui vous passe par la tête.
6 Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
Vous avez multiplié vos morts dans cette ville, et vous avez rempli ses rues de cadavres. »
7 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
"'C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: « Tes victimes que tu as déposées au milieu, ce sont les viandes, et ceci est le chaudron; mais toi, on te fera sortir du milieu.
8 Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
Tu as craint l'épée, et je ferai venir sur toi l'épée, dit le Seigneur Yahvé.
9 Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
« Je vous ferai sortir du milieu, je vous livrerai entre les mains des étrangers, et j'exercerai mes jugements au milieu de vous.
10 Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Vous tomberez par l'épée. Je vous jugerai sur la frontière d'Israël. Alors vous saurez que je suis Yahvé.
11 Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
Ce ne sera pas votre chaudron, et vous ne serez pas la viande au milieu de celui-ci. Je vous jugerai à la frontière d'Israël.
12 Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
Vous saurez que je suis Yahvé, car vous n'avez pas suivi mes lois. Vous n'avez pas exécuté mes ordonnances, mais vous avez agi selon les ordonnances des nations qui vous entourent. »'"
13 Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
Comme je prophétisais, Pelatia, fils de Benaja, mourut. Alors je tombai sur ma face, et je criai d'une voix forte, en disant: « Ah! Seigneur Yahvé! Vas-tu faire disparaître le reste d'Israël? »
14 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de l'Éternel me fut adressée, en ces termes:
15 “Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
« Fils d'homme, tes frères, les hommes de ta famille, et toute la maison d'Israël, tous, sont ceux à qui les habitants de Jérusalem ont dit: « Éloigne-toi de l'Éternel. Ce pays nous a été donné en propriété.
16 “Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
« C'est pourquoi tu diras: « Le Seigneur Yahvé dit: « Si je les ai éloignés parmi les nations, si je les ai dispersés parmi les pays, je leur servirai de sanctuaire pour un peu de temps dans les pays où ils sont venus »".
17 “Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
C'est pourquoi tu diras: « Le Seigneur Yahvé dit: « Je vous rassemblerai du milieu des peuples, je vous réunirai des pays où vous avez été dispersés, et je vous donnerai le pays d'Israël. »
18 “Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
"'Ils viendront là, et ils enlèveront de là toutes ses choses détestables et toutes ses abominations.
19 Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
Je leur donnerai un seul cœur, et je mettrai en eux un esprit nouveau. J'ôterai de leur chair le cœur de pierre et je leur donnerai un cœur de chair,
20 Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
afin qu'ils marchent selon mes lois, qu'ils observent mes ordonnances et qu'ils les mettent en pratique. Ils seront mon peuple, et je serai leur Dieu.
21 Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
Mais quant à ceux dont le cœur marche selon le cœur de leurs choses détestables et de leurs abominations, je ferai retomber leur voie sur leur propre tête, dit le Seigneur Yahvé. »
22 Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Alors les chérubins élevèrent leurs ailes, et les roues étaient à côté d'eux. La gloire du Dieu d'Israël était au-dessus d'eux, en haut.
23 Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
La gloire de Yahvé s'éleva du milieu de la ville et se tint sur la montagne qui est à l'est de la ville.
24 Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
L'Esprit m'éleva et me conduisit en vision, par l'Esprit de Dieu, en Chaldée, vers les captifs. Et la vision que j'avais eue s'éloigna de moi.
25 nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.
Et je dis aux captifs tout ce que Yahvé m'avait montré.

< Ezekieli 11 >