< Ezekieli 10 >

1 Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi.
Potem sem pogledal in glej, na nebesnem svodu, ki je bil nad glavo kerubov, tam se je nad njimi prikazal kakor kamen safir, kakor videz podobnosti prestola.
2 Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.
In spregovoril je človeku, oblečenemu z lanenim platnom in rekel: »Vstopi med kolesa, celó pod keruba in svojo roko napolni z ognjenim ogljem izmed kerubov in jih raztresi nad mestom.« In vstopil je pred mojim pogledom.
3 Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani.
Torej kerubi so stali na desni strani hiše, ko je mož vstopil; in oblak je napolnil notranji dvor.
4 Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana.
Potem se je Gospodova slava vzdignila od keruba in stala nad hišnim pragom hiše; in hiša je bila napolnjena z oblakom in dvor je bil poln sijaja Gospodove slave.
5 Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi wakati anapoongea.
In zvok kerubovih peruti je bilo slišati celó k zunanjemu dvoru, kakor glas Vsemogočnega Boga, ko spregovori.
6 Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu.
In pripetilo se je, da ko je zapovedal možu, oblečenemu z lanenim platnom, rekoč: »Vzemi ogenj izmed koles, izmed kerubov; « potem je ta vstopil in stal poleg koles.
7 Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje.
In en kerub je svojo roko iztegnil izmed kerubov k ognju, ki je bil med kerubi in vzel od njega in to položil v roke tistega, ki je bil oblečen z lanenim platnom; ki je to vzel in odšel ven.
8 (Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)
In pri kerubih se je prikazala oblika človeške roke pod njihovimi perutmi.
9 Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi.
In ko sem pogledal, glej, štiri kolesa ob kerubih, eno kolo pri enem kerubu in drugo kolo pri drugem kerubu in videz koles je bil kakor barva kamna berila.
10 Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine.
In glede njihovih videzov, so ti štirje imeli eno podobnost, kakor če bi bilo kolo v sredi kolesa.
11 Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda.
Ko so odšla, so odšla na svoje štiri strani; ko so odšla, se niso obračala, toda sledila so h kraju, kamor je pogledala glava; ko so odšla, se niso obračala.
12 Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne.
In njihovo celotno telo in njihovi hrbti in njihove roke in njihove peruti in kolesa so bili naokoli polni oči, celó kolesa, ki so jih ta štiri imela.
13 Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.”
Glede koles, jim je bilo klicano v mojem slišanju: »Oh kolo.«
14 Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.
In vsako je imelo štiri obraze: prvi obraz je bil obraz keruba, drugi obraz je bil obraz človeka, tretji obraz leva in četrti obraz orla.
15 Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari.
In kerubi so bili dvignjeni. To je živo ustvarjeno bitje, ki sem ga videl pri reki Kebár.
16 Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao.
In ko so hodili kerubi, so ob njih šla kolesa, in ko so kerubi dvignili svoje peruti, da se povzpnejo z zemlje, se tudi ista kolesa niso odvrnila od njihove bližine.
17 Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.
Ko so se ustavili, so se ta ustavila; in ko so se dvignili, so se tudi ta sama dvignila, kajti duh živega ustvarjenega bitja je bil v njih.
18 Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi.
Potem je Gospodova slava odšla od hišnega praga in obstala nad kerubi.
19 Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.
In kerubi so dvignili svoje peruti in se v mojem pogledu vzpeli z zemlje; ko so odšli, so bila tudi kolesa poleg njih in vsako je stalo pri vratih vzhodnih velikih vrat Gospodove hiše in slava Izraelovega Boga je bila zgoraj nad njimi.
20 Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi.
To je živo ustvarjeno bitje, ki sem ga videl pod Izraelovim Bogom, poleg reke Kebár; in vedel sem, da so bili to kerubi.
21 Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu.
Vsak je imel po štiri obraze in vsak štiri peruti; in podobnost človeških rok je bila pod njihovimi perutmi.
22 Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.
In podobnost njihovih obrazov so bili isti obrazi, ki sem jih videl poleg reke Kebár, njihovi videzi in oni sami. Vsak je hodil naravnost naprej.

< Ezekieli 10 >