< Ezekieli 10 >

1 Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi.
Потом видех, и гле, на небу које беше над главама херувимима показа се над њима као камен сафир на очи као престо.
2 Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.
И проговори човеку обученом у платно, и рече: Уђи међу точкове под херувимима, и узми пуне прегршти жеравице између херувима и разаспи на град. И уђе на моје очи.
3 Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani.
А херувими стајаху с десне стране дома кад уђе човек, и облак напуни унутрашњи трем.
4 Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana.
И слава Господња подиже се с херувима на праг од дома, и напуни се дом облака, а трем се напуни светлости славе Господње.
5 Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi wakati anapoongea.
И лупа крила у херувима чујаше се до спољашњег трема као глас Бога Свемогућег кад говори.
6 Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu.
И кад заповеди човеку обученом у платно говорећи: Узми огња између точкова између херувима; он уђе и стаде код точкова.
7 Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje.
И један херувим пружи руку своју између херувима к огњу који беше међу херувимима, и узе и метну у прегршти обученом у платно и он прими и изиђе.
8 (Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)
А виђаше се у херувима као рука човечија под крилима.
9 Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi.
И видех, и гле, четири точка код херувима, по један точак код једног херувима, и точкови беху на очи као камен хрисолит.
10 Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine.
И на очи беху сва четири точка једнака, и као да је точак у точку.
11 Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda.
Кад иђаху, иђаху сва четири, сваки на своју страну, и идући не скретаху, него куда гледаше глава онамо иђаху и идући не скретаху.
12 Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne.
А све им тело и леђа и руке и крила и точкови, сва четири точка њихова, беху пуна очију свуда унаоколо.
13 Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.”
А точкови се зваху како чух: кола.
14 Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.
А четири лица имаше свака животиња: једно лице херувимско, друго лице човечије и треће лице лавово и четврто лице орлово.
15 Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari.
И подигоше се херувими у вис; то беху исте животиње које видех на реци Хевару.
16 Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao.
А кад иђаху херувими, иђаху и точкови уз њих, и кад херувими махаху крилима својим да се подигну од земље, точкови се не одмицаху од њих.
17 Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.
Кад се они устављаху, устављаху се и точкови; а кад се они подизаху, подизаху се и точкови; јер беше дух животињски у њима.
18 Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi.
И слава Господња отиде изнад прага од дома, и стаде над херувиме.
19 Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.
И херувими махнувши крилима подигоше се од земље преда мном полазећи, и точкови према њима; и стадоше на источним вратима дома Господњег, и слава Бога Израиљевог беше озго над њима.
20 Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi.
То беху исте животиње које видех под Богом Израиљевим на реци Хевару, и познах да су херувими.
21 Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu.
Свака имаше четири лица и четири крила, и као рука човечија беше им под крилима.
22 Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.
И лица им беху иста која видех на реци Хевару; обличја беху иста, исти беху; сваки иђаше право на према се.

< Ezekieli 10 >