< Ezekieli 10 >

1 Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi.
Je regardai, et voici, sur le ciel, au-dessus de la tête des chérubins, comme une pierre de saphir, quelque chose de pareil à une forme de trône, au-dessus d'eux.
2 Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.
Et l'Éternel parla à l'homme vêtu de lin, et lui dit: Va entre les roues, sous les chérubins, et remplis tes mains de charbons ardents que tu prendras entre les chérubins; répands-les sur la ville.
3 Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani.
Et il y alla sous mes yeux. Or les chérubins se tenaient à droite de la maison quand l'homme alla, et la nuée remplit le parvis intérieur.
4 Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana.
Alors la gloire de l'Éternel s'éleva de dessus les chérubins, et se dirigea vers le seuil de la maison; et la maison fut remplie de la nuée, pendant que le parvis était rempli de la splendeur de la gloire de l'Éternel.
5 Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi wakati anapoongea.
Et le bruit des ailes des chérubins se fit entendre jusqu'au parvis extérieur, pareil à la voix du Dieu Tout Puissant, quand il parle.
6 Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu.
Quand l'Éternel eut donné cet ordre à l'homme vêtu de lin, en disant: “Prends du feu dans l'intervalle des roues, entre les chérubins”, cet homme alla se placer près des roues.
7 Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje.
Et un des chérubins étendit sa main, du milieu des chérubins, vers le feu qui était entre les chérubins; il en prit et le mit dans les mains de l'homme vêtu de lin, qui se retira après l'avoir reçu;
8 (Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)
Car on voyait aux chérubins une forme de main d'homme sous leurs ailes.
9 Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi.
Je regardai encore, et voici quatre roues près des chérubins, une roue près de chaque chérubin; et l'aspect de ces roues était comme celui d'une chrysolithe.
10 Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine.
A les voir, toutes quatre avaient la même forme; chaque roue semblait traverser par le milieu une autre roue.
11 Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda.
En cheminant, elles allaient de leurs quatre côtés; elles ne se tournaient point dans leur marche; mais de quelque côté que se dirigeât la tête, elles la suivaient, sans se tourner dans leur marche.
12 Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne.
Et le corps entier des chérubins, leur dos, leurs mains, leurs ailes, ainsi que les roues, les roues de chacun des quatre, étaient entièrement couverts d'yeux.
13 Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.”
Les roues, j'entendis qu'on les appelait tourbillon.
14 Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.
Chacun avait quatre faces: le premier, une face de chérubin; le second, une face d'homme; le troisième, une face de lion; et le quatrième, une face d'aigle.
15 Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari.
Et les chérubins s'élevèrent; c'étaient là les animaux que j'avais vus près du fleuve du Kébar.
16 Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao.
Quand les chérubins marchaient, les roues cheminaient à côté d'eux; quand les chérubins déployaient leurs ailes pour s'élever de terre, les roues ne se détournaient pas d'eux.
17 Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.
Quand ils s'arrêtaient, elles s'arrêtaient; quand ils s'élevaient, elles s'élevaient avec eux; car l'esprit des animaux était en elles.
18 Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi.
Puis la gloire de l'Éternel se retira du seuil de la maison, et se tint sur les chérubins.
19 Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.
Et les chérubins déployèrent leurs ailes, et s'élevèrent de terre sous mes yeux, quand ils partirent avec les roues; ils s'arrêtèrent à l'entrée de la porte orientale de la maison de l'Éternel, et la gloire du Dieu d'Israël était sur eux, en haut.
20 Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi.
C'étaient là les animaux que j'avais vus sous le Dieu d'Israël, près du fleuve du Kébar, et je les reconnus pour des chérubins.
21 Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu.
Chacun avait quatre faces, et chacun quatre ailes, et sous leurs ailes il y avait une forme de main d'homme.
22 Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.
Et leurs faces ressemblaient à celles que j'avais vues près du fleuve du Kébar; c'était le même aspect; c'étaient bien eux. Chacun d'eux marchait droit devant soi.

< Ezekieli 10 >