< Ezekieli 10 >

1 Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi.
Et je vis, et voici que sur le firmament qui était au-dessus de la tête des Chérubins, il y avait comme une pierre de saphir; quelque chose paraissant ressembler à un trône apparut au-dessus d'eux.
2 Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.
Et il dit à l'homme vêtu de lin: " Va dans les intervalles des roues, sous les Chérubins; remplis tes mains de charbons ardents pris d'entre les Chérubins, et répands-les sur la ville. " Et il y alla devant mes yeux.
3 Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani.
Or les Chérubins se tenaient à droite de la maison quand l'homme y alla, et la nuée remplit le parvis intérieur.
4 Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana.
Et la gloire de Yahweh s'éleva de dessus les Chérubins et vint sur le seuil de la maison; la maison fut remplie de la nuée, et le parvis était plein de l'éclat de la gloire de Yahweh.
5 Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi wakati anapoongea.
Le bruit des ailes des Chérubins se fit entendre jusqu'au parvis extérieur, comme la voix du Dieu tout-puissant quand il parle.
6 Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu.
Quand il eut donné cet ordre à l'homme vêtu de lin: " Prends du feu dans l'intervalle des roues, entre les Chérubins, " l'homme vint se tenir à côté des roues.
7 Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje.
Et le Chérubin avança la main entre les Chérubins, vers le feu qui était entre les Chérubins; il en prit et le mit dans les mains de l'homme vêtu de lin, qui le prit et sortit.
8 (Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)
Or on voyait aux Chérubins une forme de main d'homme sous leurs ailes.
9 Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi.
Et je vis, et voici quatre roues auprès des Chérubins, une roue à côté de chaque Chérubin, et l'aspect des roues était comme celui de la pierre de Tharsis.
10 Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine.
Et quant à leur aspect, toutes quatre étaient semblables, comme si une roue était au milieu d'une autre roue.
11 Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda.
En avançant, elles allaient sur leurs quatre côtés, et ne se retournaient pas dans leur marche; car vers le lieu où se tournait la tête elles allaient, et elles ne se retournaient pas dans leur marche.
12 Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne.
Et tout le corps des Chérubins, leur dos, leurs mains et leurs ailes, ainsi que les roues, étaient remplies d'yeux tout autour; tous les quatre avaient leurs roues.
13 Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.”
Quant aux roues, on les appelait " agiles. "
14 Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.
Chacun des Chérubins avait quatre faces: la face du premier était la face de chérubin; la face du second était une face d'homme; celle du troisième, une face de taureau, et celle du quatrième, une face d'aigle.
15 Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari.
Et les chérubins s'élevèrent; c'était l'être vivant que j'avais vu au fleuve Chobar.
16 Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao.
Quand les Chérubins allaient, les roues allaient aussi à côté d'eux; et quand les Chérubins dressaient leurs ailes pour s'élever de terre, les roues ne se détournaient pas, elles non plus, d'à côté d'eux.
17 Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.
Quand ils s'arrêtaient, elles s'arrêtaient; quand ils s'élevaient, elles s'élevaient avec eux; car l'Esprit de l'être vivant était en elles.
18 Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi.
La gloire de Yahweh se retira de dessus le seuil de la maison et s'arrêta sur les Chérubins.
19 Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.
Les Chérubins dressèrent leurs ailes et s'élevèrent de terre à mes yeux, quand ils partirent et les roues avec eux. Ils s'arrêtèrent à l'entrée de la porte orientale de la maison de Yahweh; et la gloire du Dieu d'Israël reposait sur eux par-dessus.
20 Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi.
C'était l'être vivant que j'avais vu au-dessous du Dieu d'Israël, au fleuve Chobar; et je sus que c'étaient des Chérubins.
21 Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu.
Chacun avait quatre faces et chacun avait quatre ailes, et une ressemblance de mains d'hommes était sous leurs ailes.
22 Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.
Et quant à la ressemblance de leurs faces, c'étaient les faces que j'avais vues près du fleuve Chobar; c'était le même aspect, c'étaient eux-mêmes. Chacun allait droit devant soi.

< Ezekieli 10 >