< Ezekieli 10 >

1 Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi.
And Y siy, and lo! in the firmament that was on the heed of cherubyns, as a saphir stoon, and as the fourme of licnesse of a kyngis seete apperide theron.
2 Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.
And he seide to the man that was clothid in lynnun clothis, and spak, Entre thou in the myddis of wheelis, that ben vndur cherubyns, and fille thin hond with coolis of fier, that ben bitwixe cherubyns, and schede thou out on the citee.
3 Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani.
And he entride in my siyt; forsothe cherubyns stoden at the riyt side of the hous, whanne the man entride, and a clowde fillide the ynnere halle.
4 Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana.
And the glorie of the Lord was reisid fro aboue cherubyns to the threisfold of the hous; and the hous was fillid with a cloude, and the halle was fillid with schynyng of the glorie of the Lord.
5 Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi wakati anapoongea.
And the sown of wyngis of cherubyns was herd til to the outermere halle, as the vois of almyyti God spekynge.
6 Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu.
And whanne he hadde comaundid to the man that was clothid in lynnun clothis, and hadde seid, Take thou fier fro the myddis of the wheelis, that ben bitwixe cherubyns, he entride, and stood bisidis the wheel.
7 Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje.
And cherub stretchide forth his hond fro the myddis of cherubyns, to the fier that was bitwixe cherubyns; and took, and yaf in to the hondis of hym that was clothid in lynnun clothis; and he took, and yede out.
8 (Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)
And the licnesse of the hond of a man apperide in cherubyns, vndur the wyngis of tho.
9 Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi.
And Y siy, and lo! foure wheelis weren bisidis cherubyns; o wheel bisidis o cherub, and another wheel bisidis another cherub; forsothe the licnesse of wheelis was as the siyt of the stoon crisolitis.
10 Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine.
And the biholdyng of tho was o licnesse of foure, as if a wheel be in the myddis of a wheel.
11 Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda.
And whanne tho yeden, tho yeden in to foure partis; tho turneden not ayen goynge, but to the place to which that that was the firste wheel bowide to go, also othere suyden, and turneden not ayen.
12 Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne.
And al the bodi of tho wheelis, and the neckis, and hondis, and wyngis of the beestis, and the cerclis, weren ful of iyen, in the cumpas of foure wheelis.
13 Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.”
And he clepide tho wheelis volible, ether able to go al aboute, in myn heryng.
14 Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.
Forsothe o beeste hadde foure faces; o face was the face of cherub, and the secounde face the face of a man, and in the thridde was the face of a lioun, and in the fourthe was the face of an egle;
15 Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari.
and the cherubyns weren reisid. Thilke is the beeste, which Y hadde seyn bisidis the flood Chobar.
16 Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao.
And whanne cherubyns yeden, also the wheelis bisidis tho yeden to gidere; whanne cherubyns reisiden her wyngis, that tho schulden be enhaunsid fro the erthe, the wheelis abididen not stille, but also tho weren bisidis cherubyns.
17 Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.
The wheelis stooden with tho cherubyns stondynge, and weren reisid with the cherubyns reisid; for the spirit of lijf was in tho wheelis.
18 Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi.
And the glorie of the Lord yede out fro the threisfold of the temple, and stood on the cherubyns.
19 Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.
And cherubyns reisiden her wyngis, and weren enhaunsid fro the erthe bifore me; and whanne tho yeden out, also the wheelis sueden; and it stood in the entryng of the eest yate of the hous of the Lord, and the glorie of God of Israel was on tho.
20 Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi.
Thilke is the beeste, which Y siy vndur God of Israel, bisidis the flood Chobar. And Y vndurstood that foure cherubyns weren;
21 Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu.
foure faces weren to oon, and foure wyngys weren to oon; and the licnesse of the hond of a man was vndur the wyngis of tho.
22 Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.
And the licnesse of the cheris of tho weren thilke cheeris whiche Y hadde seyn bisidis the flood Chobar; and the biholdyng of tho, and the fersnesse of ech, was to entre bifor his face.

< Ezekieli 10 >