< Ezekieli 1 >
1 Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
And it happened that, in the thirtieth year, in the fourth month, on the fifth of the month, when I was in the midst of the captives beside the river Chebar, the heavens were opened, and I saw the visions of God.
2 Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
On the fifth of the month, the same is the fifth year of the transmigration of king Joachin,
3 neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
the word of the Lord came to Ezekiel, a priest, the son of Buzi, in the land of the Chaldeans, next to the river Chebar. And the hand of the Lord was over him there.
4 Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
And I saw, and behold, a whirlwind arrived from the north. And a great cloud, wrapped in fire and brightness, was all around it. And from its midst, that is, from the midst of the fire, there was something with the appearance of amber.
5 Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
And in its midst, there was the likeness of four living creatures. And this was their appearance: the likeness of a man was in them.
6 lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
Each one had four faces, and each one had four wings.
7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
Their feet were straight feet, and the sole of their foot was like the sole of the foot of a calf, and they sparkled with the appearance of glowing brass.
8 Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
And they had the hands of a man under their wings on the four sides. And they had faces with the wings on the four sides.
9 nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
And their wings were joined to one another. They did not turn as they went. Instead, each one advanced before his face.
10 Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
But as for the likeness of their face, there was the face of a man, and the face of a lion on the right of each of the four, then the face of an ox on the left of each of the four, and the face of an eagle above each of the four.
11 Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
Their faces and their wings were extended above: two wings of each one were joined together, and two covered their bodies.
12 Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
And each one of them advanced before his face. Wherever the impetus of the spirit was to go, there they went. And they did not turn as they advanced.
13 Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
And as for the likeness of the living creatures, their appearance was like that of burning coals of fire, and like the appearance of lamps. This was the vision dashing in the midst of the living creatures, a bright fire, with lightning going forth from the fire.
14 Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
And the living creatures went and returned like flashes of lightning.
15 Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
And as I beheld the living creatures, there appeared above the earth, next to the living creatures, one wheel having four faces.
16 Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
And the appearance of the wheels and their work was like the appearance of the sea. And each of the four were similar to one another. And their appearance and work was like a wheel in the center of a wheel.
17 Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
Going forth, they went by means of their four parts. And they did not turn as they went.
18 Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
Also, the size and height and appearance of the wheels was dreadful. And the entire body was full of eyes all around each of the four.
19 Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
And when the living creatures advanced, the wheels advanced together with them. And when the living creatures were lifted up from the earth, the wheels, too, were lifted up at the same time.
20 Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Wherever the spirit went, as the spirit was going forth to that place, the wheels, too, were lifted up together, so as to follow them. For the spirit of life was in the wheels.
21 Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
When going forth, they went forth, and when standing still, they stood still. And when they were lifted up from the earth, the wheels, too, were lifted up together, so as to follow them. For the spirit of life was in the wheels.
22 Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
And above the heads of the living creatures was the likeness of a firmament: similar to crystal, but dreadful to behold, and extending over their heads from above.
23 Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
And their wings were straight under the firmament, one toward the other. One of them was covered by two wings on his body, and the other was covered similarly.
24 Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
And I heard the sound of their wings, like the sound of many waters, like the sound of the sublime God. When they walked, it was like the sound of a multitude, like the sound of an army. And when they stood still, their wings were let down.
25 Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
For when a voice came from above the firmament, which was over their heads, they stood still, and they put down their wings.
26 Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
And above the firmament, which was suspended over their heads, there was the likeness of a throne, with the appearance of the sapphire stone. And over the likeness of the throne, there was a likeness with the appearance of a man above it.
27 Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
And I saw something with the appearance of amber, with the likeness of fire within it and all around it. And from his waist and upward, and from his waist downward, I saw something with the appearance of fire shining all around.
28 Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.
There was the appearance of the rainbow, as when it is in a cloud on a rainy day. This was the appearance of the splendor on every side.