< Ezekieli 1 >
1 Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
В тридесетата година, четвъртия месец, на петия ден от месеца, като бях между пленниците при реката Ховар, отвориха се небесата, и аз видях Божии видения.
2 Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
На петия ден от месеца в тая година, която бе петата от пленяването на цар Иоахина,
3 neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
Господното слово дойде нарочно към свещеника Езекиила, син на Вузия, в Халдейската земя, при реката Ховар; и там Господната ръка биде върху него.
4 Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
Видях, и, ето, вихрушка идеше от север, голям облак и пламнал огън, а около него сияние; и отсред него се виждаше нещо на глед като светъл метал, от средата на огъня.
5 Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
Отсред него се виждаше и подобие на четири живи същества. И това беше изгледът им; те имаха човешко подобие.
6 lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
Всяко от тях имаше четири лица, всяко имаше и четири крила.
7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
Нозете им бяха прави нозе; и стъпалото на нозете им беше подобно на стъпало на телешка нога; и изпущаха искри като повърхността на лъскава мед.
8 Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
И имаха човешки ръце под крилата си на четирите си страни; и на четирите лицата и крилата бяха така:
9 nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
крилата им се съединяваха едно с друго; не се обръщаха като вървяха; всяко вървеше направо пред себе си.
10 Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
А колкото за изгледа на лицата им, той беше като човешко лице; и четирите имаха лъвово лице от дясната страна; и четирите имаха волско лице от лявата; и четирите имаха орлово лице.
11 Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
и лицата им и крилата им бяха обърнати нагоре; две крила на всяко се съединяваха едно с друго, и двете покриваха телата им.
12 Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
И вървяха всяко направо пред себе си; гдето се носеше духа, там вървяха; като вървяха не се обръщаха.
13 Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
А колкото за подобието на живите същества, изгледът им бе като запалени огнени въглища, като изгледа на факли, които се движеха нагоре надолу между живите същества; огънят беше светъл, и светкавица изскачаше из огъня.
14 Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
И живите същества блещукаха наглед като светкавица.
15 Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
А като гледах живите същества, ето по едно колело на земята при живите същества, за всяко от четирите им лица,
16 Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
Изгледът на колелата и направата им бе като цвят на хрисолит; и четирите имаха еднакво подобие; а изгледът им и направата им бяха като че ли на колело в колело.
17 Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
Когато вървяха, вървяха към четирите си страни; не се обръщаха като вървяха.
18 Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
А колелата им бяха високи и страшни; и колелата около тия четири бяха пълни с очи.
19 Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
И когато вървяха живите същества, и колелата вървяха край тях; и когато се издигаха живите същества от земята, и колелата се издигаха.
20 Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Гдето имаше да иде духът, там вървяха и те; там гдето духът имаше да иде, и колелата се издигаха край тях; защото духът на всяко от живите същества беше и в колелата му.
21 Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Когато вървяха ония, вървяха и тия; и когато стояха ония, стояха и тия; а когато ония се издигаха от земята, то и колелата се издигаха край тях; защото духът на всяко от живите същества беше и в колелата му.
22 Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
А над главите на живите същества имаше подобие на един простор, на глед като цвят на страшен кристал, разпрострян над главите им.
23 Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
А под простора крилата им бяха разпрострени, едно срещу друго; всяко същество имаше две, които покриваха телата им отсам; и всяко имаше две, които ги покриваха оттам.
24 Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
И когато вървяха, чувах фученето на крилата им като бучене на големи води, като глас на Всесилния, шум на метеж като шум на войска. Когато се спираха, спущаха крилата си.
25 Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
И глас се издаде от горе из простора, който бе над главите им; и като се спряха спуснаха крилата си.
26 Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
И над простора, който бе върху главите им, се виждаше подобие на престол, наглед като камък сапфир; и върху подобието на престола имаше подобие на глед като човек, седящ на него на високо.
27 Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
И видях нещо наглед като светъл метал, като изглед на огън в него от всяка страна; от това, което се виждаше, че е кръстът му, и нагоре, и от това, което се виждаше, че е кръстът му, и надолу видях като изглед на огън, обиколен със сияние.
28 Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.
Какъвто е изгледът на дъгата в облака в дъждовен ден, такъв бе изгледът на обикалящото сияние. Това бе изгледът на подобието на Господната слава. И когато го видях, паднах на лицето си, и чух глас на едного, който говореше.