< Kutoka 1 >
1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake:
Torej to so imena Izraelovih otrok, ki so prišli v Egipt. Z Jakobom je prišel vsak mož in njegova družina.
2 Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
Ruben, Simeon, Lévi in Juda,
3 Isakari, Zabuloni na Benyamini;
Isahár, Zábulon in Benjamin,
4 Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
Dan in Neftáli, Gad in Aser.
5 Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
Vseh duš, ki so prišle iz Jakobovih ledij, je bilo sedemdeset duš, kajti Jožef je bil že v Egiptu.
6 Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
Jožef je umrl in vsi njegovi bratje in ves ta rod.
7 lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
Izraelovi otroci pa so bili rodovitni in obilno narasli in se namnožili in postali silno mogočni in dežela je bila napolnjena z njimi.
8 Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri.
Sedaj je tam vstal nov kralj nad Egiptom, ki ni poznal Jožefa.
9 Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi.
Svojemu ljudstvu je rekel: »Glejte, ljudstva Izraelovih otrok je več in mogočnejši so, kakor smo mi.
10 Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
Pridite, modro ravnajmo z njimi, da se ne bi namnožili in se pripeti, ko izpade kakšna vojna, da se pridružijo tudi našim sovražnikom in se borijo zoper nas in tako jih napodimo iz dežele.«
11 Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
Zato so nadnje postavili preddelavce, da jih stiskajo z njihovimi bremeni. In za faraona so gradili zakladni mesti Pitóm in Ramesés.
12 Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
Toda bolj so jih stiskali, bolj so se množili in rastli. In bili so užaloščeni zaradi Izraelovih otrok.
13 kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
Egipčani so s krutostjo Izraelove otroke prisilili, da so služili.
14 Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
Njihova življenja so zagrenili s trdim suženjstvom, z malto, z opeko in z vsemi vrstami službe na polju. Vse njihove službe, s katerimi so jih pripravili, da jim služijo, so bile s krutostjo.
15 Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua,
Egiptovski kralj je spregovoril hebrejskima babicama, katerih prvi je bilo ime Šifra, ime drugi pa Pua
16 “Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
in rekel: »Ko hebrejskim ženam opravljata službo babice in jih vidita na stolčkih; če je sin, potem ga ubijta, toda če je hči, potem naj živi.«
17 Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
Toda babici sta se bali Boga in nista delali, kakor jima je egiptovski kralj ukazal, temveč sta fantke rešili žive.
18 Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
Egiptovski kralj je dal poklicati babici in jima rekel: »Zakaj sta storili to stvar in fantke rešili žive?«
19 Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
Babici sta faraonu rekli: »Zato ker Hebrejke niso kakor Egipčanke, kajti one so krepke in rodijo prej ko babice pridejo k njim.«
20 Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
Zato je Bog z babicama dobro postopal in ljudstvo se je pomnožilo in postalo zelo mogočno.
21 Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
Pripetilo se je, ker sta se babici bali Boga, da jima je naredil hiši.
22 Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”
Faraon je vsemu svojemu ljudstvu zapovedal, rekoč: »Vsakega sina, ki je rojen, boste vrgli v reko, vsaka hči pa naj bo rešena živa.«