< Kutoka 1 >

1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake:
Et ce sont ici les noms des fils d’Israël qui entrèrent en Égypte; ils y entrèrent avec Jacob, chacun avec sa famille:
2 Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
Ruben, Siméon, Lévi et Juda;
3 Isakari, Zabuloni na Benyamini;
Issacar, Zabulon et Benjamin;
4 Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
Dan et Nephthali; Gad et Aser.
5 Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
Et toutes les âmes issues des reins de Jacob étaient 70 âmes; or Joseph était en Égypte.
6 Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
Et Joseph mourut, et tous ses frères, et toute cette génération-là.
7 lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
Et les fils d’Israël fructifièrent et foisonnèrent, et multiplièrent, et devinrent extrêmement forts; et le pays en fut rempli.
8 Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri.
Et un nouveau roi se leva sur l’Égypte, qui n’avait point connu Joseph.
9 Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi.
Et il dit à son peuple: Voici, le peuple des fils d’Israël est plus nombreux et plus fort que nous.
10 Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
Allons, soyons prudents à son égard, de peur qu’il ne se multiplie, et que, s’il arrivait une guerre, il ne se joigne, lui aussi, à nos ennemis, et ne fasse la guerre contre nous, et ne monte hors du pays.
11 Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
Et ils établirent sur lui des chefs de corvées pour l’opprimer par leurs fardeaux. Et il bâtit pour le Pharaon des villes à greniers, Pithom et Ramsès.
12 Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
Et selon qu’ils l’opprimaient, il multipliait et croissait; et ils eurent peur des fils d’Israël.
13 kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
Et les Égyptiens firent servir les fils d’Israël avec dureté,
14 Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
et ils leur rendirent la vie amère par un dur service, en argile, et en briques, et par toute sorte de service aux champs: tout le service dans lequel on les faisait servir était avec dureté.
15 Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua,
Et le roi d’Égypte parla aux sages-femmes hébreues, dont l’une avait nom Shiphra et la seconde se nommait Pua,
16 “Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
et il dit: Quand vous accoucherez les femmes hébreues et que vous les verrez sur les sièges, si c’est un fils, vous le ferez mourir, et si c’est une fille, elle vivra.
17 Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
Mais les sages-femmes craignirent Dieu, et ne firent pas comme le roi d’Égypte leur avait dit; et elles laissèrent vivre les enfants mâles.
18 Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
Et le roi d’Égypte appela les sages-femmes, et leur dit: Pourquoi avez-vous fait cela, et avez-vous laissé vivre les enfants mâles?
19 Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
Et les sages-femmes dirent au Pharaon: Parce que les femmes hébreues ne sont pas comme les Égyptiennes; car elles sont vigoureuses: avant que la sage-femme vienne vers elles, elles ont enfanté.
20 Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
Et Dieu fit du bien aux sages-femmes; et le peuple multiplia, et devint très fort.
21 Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
Et il arriva, parce que les sages-femmes craignirent Dieu, qu’il leur fit des maisons.
22 Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”
Et le Pharaon commanda à tout son peuple, disant: Tout fils qui naîtra, jetez-le dans le fleuve; mais toute fille, laissez-la vivre.

< Kutoka 1 >