< Kutoka 1 >

1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake:
Voici les noms des fils d'Israël qui vinrent en Égypte (chaque homme et sa famille vinrent avec Jacob):
2 Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
Ruben, Siméon, Lévi et Juda,
3 Isakari, Zabuloni na Benyamini;
Issacar, Zabulon et Benjamin,
4 Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
Dan et Nephtali, Gad et Asher.
5 Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
Toutes les âmes qui sortirent du corps de Jacob étaient au nombre de soixante-dix, et Joseph était déjà en Égypte.
6 Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
Joseph mourut, ainsi que tous ses frères et toute cette génération.
7 lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
Les enfants d'Israël furent féconds, ils augmentèrent en abondance, ils se multiplièrent, ils devinrent extrêmement puissants, et le pays fut rempli d'eux.
8 Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri.
Or, il se leva un nouveau roi sur l'Égypte, qui ne connaissait pas Joseph.
9 Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi.
Il dit à son peuple: « Voici que le peuple des enfants d'Israël est plus nombreux et plus puissant que nous.
10 Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
Venez, traitons-les avec sagesse, de peur qu'ils ne se multiplient et que, lorsqu'une guerre éclatera, ils ne se joignent à nos ennemis, ne nous combattent et ne s'échappent du pays. »
11 Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
Ils établirent donc sur eux des maîtres de corvées pour les accabler de leurs fardeaux. Ils construisirent des villes de stockage pour Pharaon: Pithom et Raamsès.
12 Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
Mais plus ils les accablaient, plus ils se multipliaient et plus ils s'étendaient. Ils se mirent à redouter les enfants d'Israël.
13 kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
Les Égyptiens firent servir les enfants d'Israël sans pitié,
14 Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
et ils leur rendirent la vie amère par un dur service dans le mortier et dans la brique, et par toutes sortes de services dans les champs, tous leurs services, dans lesquels ils les firent servir sans pitié.
15 Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua,
Le roi d'Égypte parla aux sages-femmes hébraïques, dont l'une s'appelait Shiphrah et l'autre Puah,
16 “Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
et il dit: « Lorsque vous exercerez la fonction de sage-femme auprès des femmes hébraïques et que vous les verrez sur l'escabeau, si c'est un fils, vous le tuerez; mais si c'est une fille, elle vivra. »
17 Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
Mais les sages-femmes craignirent Dieu et ne firent pas ce que le roi d'Égypte leur avait ordonné, mais elles sauvèrent les petits garçons vivants.
18 Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
Le roi d'Égypte fit venir les sages-femmes et leur dit: « Pourquoi avez-vous fait cela et sauvé les garçons en vie? ».
19 Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
Les sages-femmes dirent à Pharaon: « Parce que les femmes hébreues ne sont pas comme les Egyptiennes, car elles sont vigoureuses et accouchent avant que la sage-femme ne vienne les voir. »
20 Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
Dieu traita bien les sages-femmes, et le peuple se multiplia et devint très puissant.
21 Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
Comme les sages-femmes craignaient Dieu, il leur donna des familles.
22 Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”
Pharaon donna cet ordre à tout son peuple: « Vous jetterez dans le fleuve tout fils qui naîtra, et vous sauverez vivante toute fille. »

< Kutoka 1 >