< Kutoka 1 >
1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake:
These ben the names of the sones of Israel, that entriden into Egipt with Jacob; alle entriden with her housis;
2 Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
Ruben, Symeon,
3 Isakari, Zabuloni na Benyamini;
Leuy, Judas, Isachar, Zabulon, and Benjamin,
4 Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
Dan, and Neptalim, Gad, and Aser.
5 Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
Therfor alle the soules of hem that yeden out of `the hipe of Jacob weren seuenti and fyue.
6 Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
Forsothe Joseph was in Egipt; and whanne he was deed, and alle hise brithren, and al his kynrede,
7 lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
the sones of Israel encreessiden, and weren multiplied as buriounnyng, and thei weren maad strong greetli, and filliden the lond.
8 Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri.
A newe kyng, that knewe not Joseph, roos in the meene tyme on Egipt, and seide to his puple, Lo!
9 Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi.
the puple of the sones of Israel is myche, and strongere than we;
10 Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
come ye, wiseli oppresse we it, lest perauenture it be multiplied; and lest, if batel risith ayens vs, it be addid to oure enemyes, and go out of the lond, whanne we ben ouercomun.
11 Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
And so he made maistris of werkis souereyns to hem, that thei schulden turmente hem with chargis. And thei maden citees of tabernaclis to Farao, Fiton, and Ramesses.
12 Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
And bi hou myche thei oppressiden hem, bi so myche thei weren multiplied, and encreessiden more.
13 kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
And Egipcians hatiden the sones of Israel, and turmentiden, and scorneden hem;
14 Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
and brouyten her lijf to bitternesse bi hard werkis of cley and to tijl stoon, and bi al seruage, bi which thei weren oppressid in the werkis of erthe.
15 Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua,
Forsothe the kyng of Egipt seide to the mydwyues of Ebrews, of whiche oon was clepid Sefora, the tother Fua;
16 “Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
and he commaundide to hem, Whanne ye schulen do the office of medewyues to Ebrew wymmen, and the tyme of childberyng schal come, if it is a knaue child, sle ye him; if it is a womman, kepe ye.
17 Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
Forsothe the medewyues dredden God, and diden not bi the comaundement of the kyng of Egipt, but kepten knaue children.
18 Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
To whiche clepid to hym the kyng seide, What is this thing which ye wolden do, that ye wolden kepe the children?
19 Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
Whiche answeriden, Ebrew wymmen ben not as the wymmen of Egipt, for thei han kunnyng of the craft of medewijf, and childen bifore that we comen to hem.
20 Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
Therfor God dide wel to medewyues; and the puple encreesside, and was coumfortid greetli.
21 Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
And for the mydewyues dredden God, he bildide `housis to hem.
22 Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”
Therfor Farao comaundide al his puple, and seide, What euer thing of male kynde is borun to Ebrewis, `caste ye into the flood; what euer thing of wymmen kynde, kepe ye.