< Kutoka 9 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
RAB Musa'ya şöyle dedi: “Firavunun yanına git ve ona de ki, ‘İbraniler'in Tanrısı RAB şöyle diyor: Halkımı salıver, bana tapsınlar.
2 Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
Salıvermeyi reddeder, onları tutmakta diretirsen,
3 mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
RAB'bin eli kırlardaki hayvanlarınızı –atları, eşekleri, develeri, sığırları, davarları– büyük kırıma uğratarak sizi cezalandıracak.
4 Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
RAB İsrailliler'le Mısırlılar'ın hayvanlarına farklı davranacak. İsrailliler'in hayvanlarından hiçbiri ölmeyecek.’”
5 Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
RAB zamanı da belirleyerek, “Yarın ülkede bunu yapacağım” dedi.
6 Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
Ertesi gün RAB dediğini yaptı: Mısırlılar'ın hayvanları büyük çapta öldü. Ama İsrailliler'in hayvanlarından hiçbiri ölmedi.
7 Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
Firavun adam gönderdi, İsrailliler'in bir tek hayvanının bile ölmediğini öğrendi. Öyleyken, inat etti ve halkı salıvermedi.
8 Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
RAB Musa'yla Harun'a, “Yanınıza iki avuç dolusu ocak kurumu alın” dedi, “Musa kurumu firavunun önünde göğe doğru savursun.
9 Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
Kurum bütün Mısır'ın üzerinde ince bir toza dönüşecek; ülkenin her yanındaki insanların, hayvanların bedenlerinde irinli çıbanlar çıkacak.”
10 Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
Böylece Musa'yla Harun ocak kurumu alıp firavunun önünde durdular. Musa kurumu göğe doğru savurdu. İnsanlarda ve hayvanlarda irinli çıbanlar çıktı.
11 Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
Büyücüler çıbandan ötürü Musa'nın karşısında duramaz oldular. Çünkü bütün Mısırlılar'da olduğu gibi onlarda da çıbanlar çıkmıştı.
12 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
RAB firavunu inatçı yaptı, RAB'bin Musa'ya söylediği gibi, firavun Musa'yla Harun'u dinlemedi.
13 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
RAB Musa'ya şöyle dedi: “Sabah erkenden kalkıp firavunun huzuruna çık, de ki, ‘İbraniler'in Tanrısı RAB şöyle diyor: Halkımı salıver, bana tapsınlar.
14 au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
Yoksa bu kez senin, görevlilerinin, halkının üzerine bütün belalarımı yağdıracağım. Öyle ki, bu dünyada benim gibisi olmadığını öğrenesin.
15 Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
Çünkü elimi kaldırıp seni ve halkını salgın hastalıkla vurmuş olsaydım, yeryüzünden silinmiş olurdun.
16 Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
Gücümü sana göstermek, adımı bütün dünyaya tanıtmak için seni ayakta tuttum.
17 Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
Hâlâ halkımı salıvermiyor, onlara üstünlük taslıyorsun.
18 Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
Bu yüzden, yarın bu saatlerde Mısır'a tarihinde görülmemiş ağır bir dolu yağdıracağım.
19 Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
Şimdi buyruk ver, hayvanların ve kırda neyin varsa hepsi sığınaklara konsun. Dolu yağınca, eve getirilmeyen, kırda kalan bütün insanlarla hayvanlar ölecek.’”
20 Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
Firavunun görevlileri arasında RAB'bin uyarısından korkanlar köleleriyle hayvanlarını çabucak evlerine getirdiler.
21 Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
RAB'bin uyarısını önemsemeyenler ise köleleriyle hayvanlarını tarlada bıraktı.
22 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
RAB Musa'ya, “Elini göğe doğru uzat” dedi, “Mısır'ın her yerine, insanların, hayvanların, kırdaki bütün bitkilerin üzerine dolu yağsın.”
23 Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
Musa değneğini göğe doğru uzatınca RAB gök gürlemeleri ve dolu gönderdi. Yıldırım düştü. RAB Mısır'a dolu yağdırdı.
24 mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
Şiddetli dolu yağıyor, sürekli şimşek çakıyordu. Mısır Mısır olalı böylesi bir dolu görmemişti.
25 Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
Dolu Mısır'da insandan hayvana dek kırdaki her şeyi, bütün bitkileri mahvetti, bütün ağaçları kırdı.
26 Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
Yalnız İsrailliler'in yaşadığı Goşen bölgesine dolu düşmedi.
27 Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
Firavun Musa'yla Harun'u çağırtarak, “Bu kez günah işledim” dedi, “RAB haklı, ben ve halkım haksızız.
28 Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
RAB'be dua edin, yeter bu gök gürlemeleri ve dolu. Sizi salıvereceğim, artık burada kalmayacaksınız.”
29 Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
Musa, “Kentten çıkınca, ellerimi RAB'be uzatacağım” dedi, “Gök gürlemeleri duracak, artık dolu yağmayacak. Böylece dünyanın RAB'be ait olduğunu bileceksin.
30 Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
Ama biliyorum, sen ve görevlilerin RAB Tanrı'dan hâlâ korkmuyorsunuz.”
31 (Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
Keten ve arpa mahvolmuştu; çünkü arpa başak vermiş, keten çiçek açmıştı.
32 Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
Ama buğday ve kızıl buğday henüz bitmediği için zarar görmemişti.
33 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
Musa firavunun yanından ayrılıp kentten çıktı. Ellerini RAB'be uzattı. Gök gürlemesi ve dolu durdu, yağmur dindi.
34 Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
Firavun yağmurun, dolunun, gök gürlemesinin kesildiğini görünce, yine günah işledi. Hem kendisi, hem görevlileri inat ettiler.
35 Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.
RAB'bin Musa aracılığıyla söylediği gibi, firavun inat ederek İsrailliler'i salıvermedi.

< Kutoka 9 >