< Kutoka 9 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
Рече же Господь к Моисею: вниди к фараону и речеши ему: сия глаголет Господь Бог Еврейский: отпусти люди Моя, да послужат Мне:
2 Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
аще убо не восхощеши отпустити людий Моих, но и еще их удержиши:
3 mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
се, рука Господня будет на скоты твоя в полях и на кони, и на ослы и на велблюды, и на говяда и на овцы, смерть велика зело:
4 Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
и дивна сотворю Аз во время оно между скоты Египетскими и между скоты сынов Израилевых: и не умрет от всех скотов сынов Израилевых ни едино.
5 Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
И даде Бог предел глаголя: во утрие сотворит Господь глаголгол сей на земли.
6 Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
И сотвори Господь глаголгол сей на утрии, и измре весь скот Египетский: от скота же сынов Израилевых не умре ни едино.
7 Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
Видев же фараон, яко не умре от всех скотов сынов Израилевых ни едино, отягчися сердце фараону, и не отпусти людий.
8 Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
Рече же Господь к Моисею и Аарону, глаголя: возмите вы полны руце пепела пещнаго, и да разсыплет Моисей к небеси пред фараоном и пред рабы его:
9 Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
и да будет прах по всей земли Египетстей, и будут на человецех и на скотех гнойнии струпи, горящии на человецех и на скотех по всей земли Египетстей.
10 Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
И взя пепел пещный пред фараоном, и разсыпа его Моисей к небеси: и быша гнойнии струпи, горящии на человецех и на скотех,
11 Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
и не можаху волсви стояти пред Моисеом струпов ради: быша бо струпи на волсвех и на всей земли Египетстей.
12 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
Ожесточи же Господь сердце фараоново, и не послуша их, якоже повеле Господь Моисею.
13 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
И рече Господь к Моисею: востани заутра и стани пред фараоном, и рцы к нему: сице глаголет Господь Бог Еврейский: отпусти люди Моя, да послужат Мне:
14 au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
в сей бо час Аз испущу вся казни Моя в сердце твое и рабов твоих и людий твоих: да увеси, яко несть ин, якоже Аз, во всей земли:
15 Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
ныне бо пустив руку Мою, поражу тя и люди твоя умерщвлю, и потребишися от земли:
16 Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
и сего ради пощаден еси доселе, да покажу на тебе крепость Мою, и яко да проповестся имя Мое по всей земли:
17 Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
еще ли убо ты востаеши на людий Моих, еже не отпустити их?
18 Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
Се, Аз одождю в сей же час заутра град мног зело, яков не бяше во Египте, от негоже дне создася, даже до дне сего:
19 Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
ныне убо потщися собрати скот твой, и елика ти суть на поли: вси бо человецы и скоти, елицы аще обрящутся на полях и не внидут в дом, падет же на ня град, измрут.
20 Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
Иже убояся слова Господня от рабов фараоновых, собра скоты своя в домы:
21 Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
а иже не вня мыслию слову Господню, остави скоты на полях.
22 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
Рече же Господь к Моисею: простри руку твою на небо, и будет град по всей земли Египетстей, на человеки и на скоты и на всю траву земную.
23 Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
Простре же Моисей руку на небо, и Господь даде громы и град, и течаше огнь по земли, и одожди Господь град по всей земли Египетстей:
24 mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
бяше же град и огнь горящь со градом, град же мног зело зело, яков не бысть во Египте, отнележе быша люди в нем.
25 Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
Порази же град во всей земли Египетстей от человека до скота, и всяку траву яже на поли порази град, и вся древа яже на полях сотре град:
26 Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
токмо в земли Гесемстей, идеже бяху сынове Израилевы, не бысть град.
27 Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
Послав же фараон, призва Моисеа и Аарона и рече им: согреших ныне: Господь праведен аз же и людие мои нечестиви:
28 Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
помолитеся убо о мне ко Господу, и да престанут быти громи Божии и град и огнь на земли, и отпущу вы, и ктому не приложите медлити.
29 Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
Рече же ему Моисей: егда изыду из града, простру руце мои на небо ко Господу, и громи престанут, и град и дождь не будет ктому, да увеси, яко Господня есть земля:
30 Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
ты же и раби твои, вем, яко еще не убоястеся Господа.
31 (Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
Лен же и ячмень побит есть, ячмень бо испущаше класы, а лен семя:
32 Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
пшеница же и жито не побиты, поздны бо бяху.
33 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
Изыде же Моисей от фараона из града и простре руце свои ко Господу, и громове престаша, и град и дождь не укану на землю ктому.
34 Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
Видев же фараон, яко преста дождь и град и громи, приложи согрешати еще, и отягчи сердце свое и рабов своих:
35 Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.
и ожесточися сердце фараоново и рабов его, и не отпусти сынов Израилевых, якоже глагола Господь к Моисею.

< Kutoka 9 >