< Kutoka 9 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
Forsothe the Lord seide to Moises, Entre thou to Farao, and speke thou to hym, The Lord God of Ebrews seith these thingis, Delyuere thou my puple, that it make sacrifice to me;
2 Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
that if thou forsakist yit, and withholdist hem, lo!
3 mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
myn hond schal be on thi feeldis, on horsis, and assis, and camels, and oxun, and scheep, a pestilence ful greuous;
4 Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
and the Lord schal make a merueilous thing bitwixe the possessiouns of Israel and the possessiouns of Egipcians, that outirli no thing perische of these thingis that perteynen to the sones of Israel.
5 Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
And the Lord ordeinede a tyme, and seide, To morewe the Lord schal do this word in the lond.
6 Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
Therfor the Lord made this word in the tother dai, and alle the lyuynge beestis of Egipcians weren deed; forsothe outirli no thing perischide of the beestis of the sones of Israel.
7 Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
And Farao sente to se, nether ony thing was deed of these thingis whiche Israel weldide; and the herte of Farao was maad greuouse, and he delyuerede not the puple.
8 Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
And the Lord seide to Moises and Aaron, Take ye the hondis ful of askis of the chymeney, and Moises sprynge it in to heuene bifore Farao;
9 Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
and be there dust on al the lond of Egipt; for whi botchis schulen be in men and in werk beestis, and bolnynge bladdris schulen be in al the lond of Egipt.
10 Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
And thei token askis of the chymney, and stoden bifore Farao; and Moises spreynt it into heuene; and woundis of bolnynge bladdris weren maad in men, and in werk beestis;
11 Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
and the witchis myyten not stonde bifor Moises, for woundis that weren in hem, and in al the lond of Egipt.
12 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
And the Lord made hard the herte of Farao, and he herde not hem, as the Lord spak to Moises.
13 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
Also the Lord seide to Moises, Rise thou eerli, and stonde bifore Farao, and thou schalt seie to hym, The Lord God of Ebrews seth these thingis, Delyuere thou my puple, that it make sacrifice to me;
14 au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
for in this tyme Y schal sende alle my veniauncis on thin herte, and on thi seruauntis, and on thi puple, that thou wite, that noon is lijk me in al erthe.
15 Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
For now Y schal holde forth the hond, and Y schal smyte thee and thi puple with pestilence, and thou schalt perische fro erthe;
16 Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
forsothe herfor Y haue set thee, that Y schewe my strengthe in thee, and that my name be teld in ech lond.
17 Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
Yit thou withholdist my puple, and nylt delyuere it?
18 Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
Lo! to morewe in this same our Y schal reyne ful myche hail, which maner hail was not in Egipt, fro the dai in which it was foundid, til in to present tyme.
19 Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
Therfor sende thou `riyt now, and gadere thi werk beestis, and alle thingis whiche thou hast in the feeld; for men and werk beestis and alle thingis that ben in feeldis with outforth, and ben not gaderid fro the feeldis, and haile falle on tho, schulen die.
20 Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
He that dredde `the Lordis word, of the seruauntis of Farao, made his seruauntis and werk beestis fle in to housis;
21 Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
sotheli he that dispiside the `Lordis word, lefte his seruauntis and werk beestis in the feeldis.
22 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
And the Lord seide to Moises, Holde forth thin hond in to heuene, that hail be maad in al the lond of Egipt, on men, and on werk beestis, and on ech eerbe of the feeld in the lond of Egipt.
23 Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
And Moises held forth the yerde in to heuene; and the Lord yaf thundris, and hail, and leitis rennynge aboute on the lond; and the Lord reynede hail on the lond of Egipt;
24 mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
and hail and fier meddlid togidere weren borun forth; and it was of so myche greetnesse, how greet apperide neuere bifore in al the lond of Egipt, sithen thilke puple was maad.
25 Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
And the hail smoot in the lond of Egipt alle thingis that weren in the feeldis, fro man til to werk beeste; and the hail smoot al the eerbe of the feeld, and brak al the flex of the cuntrey;
26 Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
oonli the hail felde not in the lond of Gessen, where the sones of Israel weren.
27 Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
And Farao sente, and clepide Moises and Aaron, and seide to hem, Y haue synned also now; the Lord is iust, Y and my puple ben wickid;
28 Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
preye ye the Lord, that the thundris and hail of God ceesse, and Y schal delyuere you, and dwelle ye no more here.
29 Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
Moyses seide, Whanne Y schal go out of the citee, Y schal holde forth myn hondis to the Lord, and leitis and thundris schulen ceesse, and hail schal not be, that thou wite, that the lond is the Lordis;
30 Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
forsothe Y knowe, that thou and thi seruauntis dreden not yit the Lord.
31 (Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
Therfor the flex and barli was hirt, for the barli was greene, and the flex hadde buriounned thanne knoppis;
32 Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
forsothe wheete and beenys weren not hirt, for tho weren late.
33 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
And Moyses yede out fro Farao, and fro the citee, and helde forth the hondis to the Lord, and thundris and hail ceessiden, and reyn droppide no more on the erthe.
34 Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
Sotheli Farao siy that the reyn hadde ceessid, and the hail, and thundris, and he encreesside synne;
35 Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.
and the herte of hym and of hise seruauntis was maad greuouse, and his herte was maad hard greetli; nethir he lefte the sones of Israel, as the Lord comaundide bi `the hond of Moises.