< Kutoka 9 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
Then Yahweh said to Moses/me, “Go to the king and say to him, ‘This is what Yahweh, the God [we] Hebrews [worship], says: “Allow my people to go, in order that they may worship me.
2 Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
If you still keep refusing to let them go [DOU],
3 mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
I warn you that I will punish you with my power [MTY] by sending a terrible disease on all your animals—on your horses, donkeys, camels, on your cattle, and on your flocks [of sheep and goats].
4 Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
But I, Yahweh, will distinguish between [what I do to] the animals that belong to the Israeli people and [what I do to] your animals. The result will be that no animal that belongs to the Israeli people will die.”’
5 Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
[Tell him that] I have determined/decided that tomorrow is the day that I will do this in this land.”
6 Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
The next day Yahweh did just what he said [that he would do]. A terrible disease afflicted all of the Egyptians’ animals, and many of them [HYP] died. But none of the Israeli people’s animals died.
7 Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
The king sent [men to investigate], and they were surprised [to see] that none of the Israeli people’s animals had died. But [after they reported that to] the king, he continued to be stubborn [IDM], and he did not let the [Israeli] people go.
8 Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
Then Yahweh said to Aaron and Moses/me, “Take a few handfuls of ashes/soot from (a furnace/an oven where they burn lime), and let Moses throw them up into the air, in front of the king.
9 Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
The [ashes/soot] will spread all over the country of Egypt like fine dust. And the ashes/soot will cause boils to afflict both the Egyptian people and their animals, all over the land.”
10 Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
So they/we both got some ashes/soot and [went and] stood in front of the king. Moses/I threw the ashes/soot up into the air. The ashes/soot spread all over, causing boils to afflict the [Egyptian] people and their animals. All the boils became open sores.
11 Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
Even the men who worked magic had boils. The result was that [they were suffering so much that] they were not able to come to Moses/me, because the men who worked magic had boils just like all [the rest of] the Egyptian people.
12 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
But Yahweh caused the king to [continue to] be stubborn [IDM]. He did not pay any attention to what they/we [said], just as Yahweh had told Moses/me [would happen].
13 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
Then Yahweh said to Moses/me, “Get up early [tomorrow] morning. Go and stand in front of the king and tell him that Yahweh God, the one that the Hebrew people [worship], says this: ‘Let my people go, in order that they may worship me [in the desert].
14 au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
[If you do not let them go], this time I will [punish] with plagues [not only] your officials and the rest of your people, but I will punish you yourself [SYN], in order that you will know there is no [god] like me anywhere in the world.
15 Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
By this time I could have used my power [MTY] to strike you and your people with terrible diseases that would have wiped you all from the earth.
16 Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
But I have let you live. The reason I have let you live is to show you my power, with the result that [people] all over the earth [HYP] will know how great I [MTY] am.
17 Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
You are still acting proudly and refusing to let my people go.
18 Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
So listen [to this]: About this time tomorrow I will cause very heavy hail to fall [in Egypt]. From the time Egypt first became [a country], there has never been a hailstorm [as bad as this one will be].
19 Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
So you should send [a message to everyone] to put their cattle, and everything else that they own that is [out] in the fields, under shelters. The hail will fall on every person and every animal that is out in the fields and that is not put under a shelter, and they will all die.’” [So Moses/I did what Yahweh said].
20 Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
Some of the king’s officials who heard what Yahweh had said became very afraid. So they put all their animals and their slaves under shelters.
21 Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
But those who did not pay any attention to what Yahweh had said left their slaves and their animals in the fields.
22 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
Then Yahweh said to Moses/me, “Raise your hand up toward the sky, in order that hail will fall all over the land of Egypt—on the people and on their animals and on all the plants in the fields.”
23 Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
So Moses/I lifted his/my stick up toward the sky. And Yahweh sent down hail, all over the land of Egypt. There was also thunder and lightning.
24 mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
While very heavy hail was falling, there was thunder, and lightning struck the ground. There had never been a hailstorm like that since Egypt first became a country.
25 Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
The hail struck everything that was in the fields all over Egypt—every person and every animal. The hail destroyed the plants in the fields and stripped [the leaves off] the trees.
26 Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
Only in the Goshen region, where the Israeli people were [living], was there no hail.
27 Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
Then the king sent [someone] to summon Aaron and Moses/me. [When they/we came to the king], he said to them/us, “This time [I admit that] I have sinned. What Yahweh [has done] is right, and what I and my people [have done] is wrong.
28 Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
(Pray to/Plead with) Yahweh [to cause it to stop]! [We] cannot [endure any more] of this thunder and hail! I will let your people go; they do not have to stay [here in Egypt] any longer.”
29 Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
Moses/I replied, “As soon as I go out of this city, I will lift up my hands [and pray] to Yahweh. Then the thunder will cease, and no more hail [will fall]. [This will happen] in order that you will know that Yahweh, [not your gods], controls everything [that happens] on the earth.
30 Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
But as for you and your officials, I know that you do not yet fear Yahweh God.”
31 (Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
When the hail fell, the flax was ruined because the buds were forming, and the barley was ruined because its grain was ripe.
32 Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
But none of the wheat crops was ruined, because their shoots were still very small.
33 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
So Moses/I left the king and went outside the city. He/I lifted up his/my hands toward Yahweh [and prayed]. Then the thunder and the hail stopped, and the rain also stopped falling on the land [of Egypt].
34 Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
But when the king saw that the rain and the hail and the thunder had stopped, he sinned again. He and his officials continued to be stubborn [IDM].
35 Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.
So, just as Yahweh had predicted by what he told Moses/me, the king did not allow the Israeli people to leave.

< Kutoka 9 >