< Kutoka 9 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
and to say LORD to(wards) Moses to come (in): come to(wards) Pharaoh and to speak: speak to(wards) him thus to say LORD God [the] Hebrew to send: let go [obj] people my and to serve: minister me
2 Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
that if: except if: except refusing you(m. s.) to/for to send: let go and still you to strengthen: hold in/on/with them
3 mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
behold hand: power LORD to be in/on/with livestock your which in/on/with land: country in/on/with horse in/on/with donkey in/on/with camel in/on/with cattle and in/on/with flock pestilence heavy much
4 Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
and be distinguished LORD between livestock Israel and between livestock Egypt and not to die from all to/for son: descendant/people Israel word: thing
5 Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
and to set: make LORD meeting: time appointed to/for to say tomorrow to make: do LORD [the] word: thing [the] this in/on/with land: country/planet
6 Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
and to make: do LORD [obj] [the] word: thing [the] this from morrow and to die all livestock Egyptian and from livestock son: descendant/people Israel not to die one
7 Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
and to send: depart Pharaoh and behold not to die from livestock Israel till one and to honor: heavy heart Pharaoh and not to send: let go [obj] [the] people
8 Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
and to say LORD to(wards) Moses and to(wards) Aaron to take: take to/for you fullness palm your soot kiln and to scatter him Moses [the] heaven [to] to/for eye: seeing Pharaoh
9 Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
and to be to/for dust upon all land: country/planet Egypt and to be upon [the] man and upon [the] animal to/for boil to break out boil in/on/with all land: country/planet Egypt
10 Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
and to take: take [obj] soot [the] kiln and to stand: stand to/for face: before Pharaoh and to scatter [obj] him Moses [the] heaven [to] and to be boil boil to break out in/on/with man and in/on/with animal
11 Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
and not be able [the] magician to/for to stand: stand to/for face: before Moses from face: because [the] boil for to be [the] boil in/on/with magician and in/on/with all Egyptian
12 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
and to strengthen: strengthen LORD [obj] heart Pharaoh and not to hear: hear to(wards) them like/as as which to speak: speak LORD to(wards) Moses
13 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
and to say LORD to(wards) Moses to rise in/on/with morning and to stand to/for face: before Pharaoh and to say to(wards) him thus to say LORD God [the] Hebrew to send: let go [obj] people my and to serve: minister me
14 au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
for in/on/with beat [the] this I to send: depart [obj] all plague my to(wards) heart your and in/on/with servant/slave your and in/on/with people your in/on/with for the sake of to know for nothing like me in/on/with all [the] land: country/planet
15 Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
for now to send: reach [obj] hand: power my and to smite [obj] you and [obj] people your in/on/with pestilence and to hide from [the] land: country/planet
16 Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
and but in/on/with for the sake of this to stand: appoint you in/on/with for the sake of to see: see you [obj] strength my and because to recount name my in/on/with all [the] land: country/planet
17 Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
still you to build in/on/with people my to/for lest to send: let go them
18 Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
look! I to rain like/as time tomorrow hail heavy much which not to be like him in/on/with Egypt to/for from [the] day to found she and till now
19 Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
and now to send: depart to seek refuge [obj] livestock your and [obj] all which to/for you in/on/with land: country all [the] man and [the] animal which to find in/on/with land: country and not to gather [the] house: home [to] and to go down upon them [the] hail and to die
20 Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
[the] afraid [obj] word LORD from servant/slave Pharaoh to flee [obj] servant/slave his and [obj] livestock his to(wards) [the] house: home
21 Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
and which not to set: put heart his to(wards) word LORD and to leave: forsake [obj] servant/slave his and [obj] livestock his in/on/with land: country
22 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
and to say LORD to(wards) Moses to stretch [obj] hand your upon [the] heaven and to be hail in/on/with all land: country/planet Egypt upon [the] man and upon [the] animal and upon all vegetation [the] land: country in/on/with land: country/planet Egypt
23 Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
and to stretch Moses [obj] tribe: rod his upon [the] heaven and LORD to give: cry out voice: thunder and hail and to go: went fire land: country/planet [to] and to rain LORD hail upon land: country/planet Egypt
24 mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
and to be hail and fire to take: fire in/on/with midst [the] hail heavy much which not to be like him in/on/with all land: country/planet Egypt from the past to be to/for nation
25 Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
and to smite [the] hail in/on/with all land: country/planet Egypt [obj] all which in/on/with land: country from man and till animal and [obj] all vegetation [the] land: country to smite [the] hail and [obj] all tree [the] land: country to break
26 Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
except in/on/with land: country/planet Goshen which there son: descendant/people Israel not to be hail
27 Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
and to send: depart Pharaoh and to call: call to to/for Moses and to/for Aaron and to say to(wards) them to sin [the] beat LORD [the] righteous and I and people my [the] wicked
28 Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
to pray to(wards) LORD and many from to be voice: thunder God and hail and to send: let go [obj] you and not to add: again [emph?] to/for to stand: stand
29 Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
and to say to(wards) him Moses like/as to come out: come I [obj] [the] city to spread [obj] palm my to(wards) LORD [the] voice: thunder to cease [emph?] and [the] hail not to be still because to know for to/for LORD [the] land: country/planet
30 Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
and you(m. s.) and servant/slave your to know for before to fear: revere [emph?] from face: because LORD God
31 (Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
and [the] flax and [the] barley to smite for [the] barley Abib and [the] flax bud
32 Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
and [the] wheat and [the] rye not to smite for late they(fem.)
33 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
and to come out: come Moses from from with Pharaoh [obj] [the] city and to spread palm his to(wards) LORD and to cease [the] voice: thunder and [the] hail and rain not to pour land: country/planet [to]
34 Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
and to see: see Pharaoh for to cease [the] rain and [the] hail and [the] voice: thunder and to add: again to/for to sin and to honor: heavy heart his he/she/it and servant/slave his
35 Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.
and to strengthen: strengthen heart Pharaoh and not to send: let go [obj] son: descendant/people Israel like/as as which to speak: speak LORD in/on/with hand: by Moses

< Kutoka 9 >