< Kutoka 9 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
The Lord told Moses, “Go and speak to Pharaoh. Tell him, ‘This is what the Lord says: Let my people go, so that they can worship me.
2 Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
If you refuse to let them go and keep holding onto them,
3 mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
I will punish you by bringing a very severe plague on your livestock—on your horses, donkeys, camels, herds, and flocks.
4 Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
But the Lord will distinguish between the livestock of the Israelites and the Egyptians, so that none of those belonging to the Israelites will die.’
5 Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
The Lord has set a time, saying, ‘Tomorrow this is what is going to happen here in the country.’”
6 Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
The following day the Lord did what he had said. All the Egyptians' livestock died, but not a single animal belonging to the Israelites died.
7 Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
Pharaoh sent out officials and discovered that not a single one of the Israelites' livestock had died. But Pharaoh was stubborn, and he would not let the people leave.
8 Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
The Lord told Moses and Aaron, “Go and get some handfuls of soot from a furnace. Then have Moses throw it into the air in front of Pharaoh.
9 Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
It will spread like fine dust over the whole country of Egypt, and open sores will break out on people and animals throughout the land.”
10 Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
They got soot from a furnace, and went to see Pharaoh. Moses threw it into the air, and open sores broke out on people and animals.
11 Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
The magicians were unable to come and appear before Moses, because they and all the other Egyptians were covered in sores.
12 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
But the Lord gave Pharaoh a stubborn attitude, and he would not listen to them, just as the Lord had told Moses.
13 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
The Lord told Moses, “Tomorrow morning get up early and go to Pharaoh, and tell him that this is what the Lord, the God of the Hebrews, says: ‘Let my people go, so that they can worship me.
14 au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
This time I will direct all my plagues against you and your officials and your people, so you will realize that there is no one like me in all the earth.
15 Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
By now I could have reached out to strike you and your people with a plague that would have completely destroyed you.
16 Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
However, I have let you live so you can see my power, and that my reputation may be spread throughout the earth.
17 Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
But in your pride you are still tyrannizing my people, and refuse to let them leave.
18 Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
So watch out! About this time tomorrow I will send down the worst hailstorm that has ever fallen on Egypt, from the beginning of its history until now.
19 Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
So order your livestock and everything you have in the field to be brought inside. Every person and every animal that stays outside and is not brought inside will die when the hail falls on them.’”
20 Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
Those of Pharaoh's officials who took seriously what the Lord said rushed to bring their servants and livestock inside.
21 Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
But those who didn't care what the Lord said left their servants and livestock outside.
22 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
The Lord told Moses, “Lift your hand towards the sky so that a hailstorm will fall over the whole of Egypt, on people and on animals, and on everything growing in the fields of Egypt.”
23 Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
Moses held up his staff toward heaven, and the Lord sent thunder and hail, and made lightning hit the ground. This is how the Lord rained hail down on Egypt.
24 mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
As the hail fell it was accompanied by lightning flashing back and forth. The hail that fell was so severe that nothing like it had ever been seen in the whole of Egypt since the beginning of its history.
25 Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
All across Egypt hail hit everything in the fields, both people and animals. It knocked down everything growing in the fields, and stripped every tree bare.
26 Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
Only in the land of Goshen where the Israelites lived was there no hail.
27 Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
Pharaoh called for Moses and Aaron and told them, “I admit that I sinned this time! The Lord is right, and I and my people are wrong!
28 Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
Pray to the Lord for us, because there's been more than enough of God's thunder and hail. I will let you leave. You don't need to stay here any longer.”
29 Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
“Once I've left the city, I will pray to the Lord for you,” Moses told him. “The thunder will stop, and there'll be no more hail, so that you will realize that the earth belongs to the Lord.
30 Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
But I know you and your officials still do not really respect the Lord our God.”
31 (Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
(The flax and barley were destroyed, because the barley was ripe and the flax was flowering.
32 Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
However, the wheat and the spelt were not destroyed because they grow later.)
33 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
Moses left Pharaoh and went out of the city, and prayed to the Lord. The thunder and hail stopped, and the rainstorm finished.
34 Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
When Pharaoh saw that the rain and hail and thunder had stopped, he sinned again, and he chose to become stubborn again, along with his officials.
35 Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.
Because of his stubborn attitude, Pharaoh would not let the Israelites leave, just as the Lord had predicted through Moses.

< Kutoka 9 >