< Kutoka 9 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.”
Tedy řekl Hospodin Mojžíšovi: Vejdi k Faraonovi, a mluv k němu: Takto praví Hospodin, Bůh Hebrejský: Propusť lid můj, ať mi slouží.
2 Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia,
Pakli nebudeš chtíti propustiti, než předce držeti je budeš:
3 mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi.
Aj, ruka Hospodinova bude na dobytku tvém, kterýž jest na poli, na koních, na oslích, na velbloudích, na volích a na ovcech, mor těžký velmi.
4 Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’”
A učiní Hospodin rozdíl mezi dobytky Izraelských a mezi dobytky Egyptských, aby nic neumřelo ze všeho, což jest synů Izraelských.
5 Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.”
A uložil Hospodin čas jistý, řka: Zítra učiní Hospodin věc takovou na zemi.
6 Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa.
I učinil Hospodin tu věc na zejtří, a pomřel všecken dobytek Egyptským; z dobytku pak synů Izraelských ani jedno neumřelo.
7 Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.
I poslal Farao, a aj, neumřelo z dobytků Izraelských ani jedno. Ale obtíženo jest srdce Faraonovo, a nepropustil lidu.
8 Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao.
I řekl Hospodin Mojžíšovi a Aronovi: Vezměte sobě plné hrsti své popela z peci, a ať jej sype Mojžíš k nebi před očima Faraonovýma.
9 Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”
I obrátí se v prach po vší zemi Egyptské, a budou z něho na lidech i na hovadech vředové prýštící se neštovicemi po vší zemi Egyptské.
10 Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama.
Nabravše tedy popela z peci, stáli před Faraonem, a sypal jej Mojžíš k nebi. I byli vředové plní neštovic, prýštící se na lidech i na hovadech.
11 Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote.
Aniž mohli čarodějníci státi před Mojžíšem pro vředy; nebo byli vředové na čarodějnících i na všech Egyptských.
12 Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.
I zsilil Hospodin srdce Faraonovo, a neposlechl jich, tak jakž byl mluvil Hospodin k Mojžíšovi.
13 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu,
Tedy řekl Hospodin Mojžíšovi: Vstana ráno, postav se před Faraonem, a rci k němu: Takto praví Hospodin, Bůh Hebrejský: Propusť lid můj, ať mi slouží.
14 au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
Nebo já teď již pošli všecky rány své na srdce tvé, i na služebníky tvé a na lid tvůj, abys věděl, žeť není podobného mně na vší zemi.
15 Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi.
Nebo nyní, když jsem vztáhl ruku svou, byl bych tebe také ranil i lid tvůj morem tím; a tak bys byl vyhlazen z země.
16 Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.
Ale však proto jsem tě zachoval, abych ukázal na tobě moc svou, a aby vypravovali jméno mé na vší zemi.
17 Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende.
Ještě ty pozdvihuješ se proti lidu mému, nechtěje ho propustiti?
18 Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo.
Aj, já dštíti budu zítra v tentýž čas krupobitím těžkým náramně, jakéhož nebylo v Egyptě od toho dne, jakž založen jest, až do tohoto času.
19 Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’”
Protož nyní pošli, shromažď dobytek svůj a cokoli máš na poli. Na všecky lidi i hovada, kteráž by nalezena byla na poli, a nebyla by shromážděna do domu, spadne krupobití, a pomrou.
20 Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani.
Kdo tedy z služebníků Faraonových ulekl se slova Hospodinova, svolal hbitě služebníky své i dobytek svůj do domu.
21 Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.
Ale kdož nepřiložil srdce svého k slovu Hospodinovu, nechal služebníků svých a dobytka svého na poli.
22 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.”
I řekl Hospodin Mojžíšovi: Vztáhni ruku svou k nebi, ať jest krupobití po vší zemi Egyptské, na lidi i na hovada i na všelikou bylinu polní v zemi Egyptské.
23 Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri,
Tedy vztáhl Mojžíš hůl svou k nebi, a Hospodin vydal hřímání a krupobití. I sstoupil oheň na zem, a dštil Hospodin krupobitím na zemi Egyptskou.
24 mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa.
I bylo krupobití a oheň smíšený s krupobitím těžký velmi, jakéhož nebylo nikdy ve vší zemi Egyptské, jakž v ní bydliti lidé začali.
25 Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti.
I ztloukly kroupy po vší zemi Egyptské, cožkoli bylo na poli od člověka až do hovada; všecku také bylinu polní potloukly kroupy, i všecko stromoví na poli zpřerážely.
26 Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.
Toliko v zemi Gesen, v níž byli synové Izraelští, nebylo krupobití.
27 Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji.
Poslav tedy Farao, povolal Mojžíše a Arona a řekl jim: Zhřešil jsem i nyní. Hospodinť jest spravedlivý, ale já a lid můj bezbožní jsme.
28 Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”
Modlte se Hospodinu, (nebo dosti jest), ať není hřímání Božího a krupobití. Tedy propustím vás, aniž déle zůstávati budete.
29 Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana.
I řekl jemu Mojžíš: Když vyjdu ven z města, rozprostru ruce své k Hospodinu, a hřímání přestane, i krupobití více nebude, abys poznal, že Hospodinova jest země.
30 Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”
Ale vím, že ani ty, ani služebníci tvoji ještě se nebudete báti tváři Hospodina Boha.
31 (Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua.
I potlučen jest len a ječmen; nebo ječmen se byl vymetal, len také byl v hlávkách.
32 Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)
Ale pšenice a špalda nebyla ztlučena, nebo pozdní byla.
33 Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini.
Tedy Mojžíš vyšed od Faraona z města, rozprostřel ruce své k Hospodinu. I přestalo hřímání a krupobití, a ani déšť nelil se na zemi.
34 Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu.
Uzřev pak Farao, že přestal déšť a krupobití a hřímání, opět hřešil; a více obtížil srdce své, on i služebníci jeho.
35 Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.
I zsililo se srdce Faraonovo, a nepropustil synů Izraelských, tak jakž byl mluvil Hospodin skrze Mojžíše.

< Kutoka 9 >