< Kutoka 8 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
And he said Yahweh to Moses go to Pharaoh and you will say to him thus he says Yahweh let go people my so they may serve me.
2 Kama ukikataa kuwaruhusu kuondoka, basi nitaipiga nchi yako yote kwa kuwaletea vyura.
And if [are] refusing you to let [them] go here! I [am] about to strike all territory your with frogs.
3 Mto Naili utafurika vyura. Watakuja kwenye jumba lako la kifalme na katika chumba chako cha kulala na kitandani mwako, katika nyumba za maafisa wako na kwa watu wako, vyura hao wataingia katika meko yenu na kwenye vyombo vya kukandia unga.
And it will swarm the River frogs and they will go up and they will go in house your and in [the] chamber of lying down your and on bed your and in [the] house of servants your and on people your and in ovens your and in kneading troughs your.
4 Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako na maafisa wako wote.’”
And on you and on people your and on all servants your they will go up the frogs.
5 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha mkono wako ukiwa na ile fimbo yako juu ya vijito, mifereji na madimbwi, fanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’”
And he said Yahweh to Moses say to Aaron stretch out hand your with staff your over the rivers over the canals and over the ponds and bring up the frogs on [the] land of Egypt.
6 Ndipo Aroni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, nao vyura wakatokea na kuifunika nchi.
And he stretched out Aaron hand his over [the] waters of Egypt and it went up the frog[s] and it covered [the] land of Egypt.
7 Lakini waganga wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao, nao pia wakafanya vyura kuja juu ya nchi ya Misri.
And they did thus the magicians by enchantments their and they brought up the frogs on [the] land of Egypt.
8 Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kusema, “Mwombeni Bwana awaondoe vyura kutoka kwangu na kwa watu wangu, nami nitawaachia watu wenu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
And he summoned Pharaoh Moses and Aaron and he said pray to Yahweh so may he remove the frogs from me and from people my and I will let go the people so they may sacrifice to Yahweh.
9 Mose akamwambia Farao, “Ninakupa heshima ya kuamua ni wakati gani wa kukuombea wewe, maafisa wako na watu wako ili kwamba vyura watoke kwenu na kwenye nyumba zenu. Isipokuwa wale walio katika Mto Naili.”
And he said Moses to Pharaoh honor yourself over me to when? - will I pray for you and for servants your and for people your to cut off the frogs from you and from houses your only in the River they will remain.
10 Farao akasema, “Kesho.” Mose akamjibu, “Itakuwa kama unavyosema, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote kama Bwana Mungu wetu.
And he said to tomorrow and he said according to word your so that you may know that there not [is] like Yahweh God our.
11 Vyura wataondoka kwako na katika nyumba zako, kwa maafisa wako na kwa watu wako, ila watabakia katika Mto Naili tu.”
And they will depart the frogs from you and from houses your and from servants your and from people your only in the River they will remain.
12 Baada ya Mose na Aroni kuondoka kwa Farao, Mose akamlilia Bwana kuhusu vyura aliokuwa amewaleta kwa Farao.
And he went out Moses and Aaron from with Pharaoh and he cried out Moses to Yahweh on [the] matter of the frogs which he had appointed for Pharaoh.
13 Naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Vyura wakafia ndani ya nyumba, viwanjani na mashambani.
And he did Yahweh according to [the] word of Moses and they died the frogs from the houses from the villages and from the fields.
14 Wakayakusanya malundo, nchi nzima ikanuka.
And people piled up them heaps heaps and it stank the land.
15 Lakini Farao alipoona pametokea nafuu, akaushupaza moyo wake na hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
And he saw Pharaoh that it had come the respite and he made heavy heart his and not he listened to them just as he had said Yahweh.
16 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha fimbo yako uyapige mavumbi ya ardhi,’ nayo nchi yote ya Misri mavumbi yatakuwa viroboto.”
And he said Yahweh to Moses say to Aaron stretch out staff your and strike [the] dust of the earth and it will become gnats in all [the] land of Egypt.
17 Wakafanya hivyo, Aroni aliponyoosha mkono wake wenye fimbo na kuyapiga mavumbi ya nchi, viroboto wakawajia watu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi ya Misri yakawa viroboto.
And they did so and he stretched out Aaron hand his with staff his and he struck [the] dust of the ground and it was the gnat[s] on humankind and on the livestock all [the] dust of the ground it was gnats in all [the] land of Egypt.
18 Lakini waganga walipojaribu kutengeneza viroboto kwa siri ya uganga wao, hawakuweza. Nao viroboto walikuwa juu ya watu na wanyama.
And they did thus the magicians by enchantments their to bring forth the gnats and not they were able and it was the gnat[s] on humankind and on the livestock.
19 Waganga wale wakamwambia Farao, “Hiki ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ukawa mgumu naye hakuwasikiliza, kama vile Bwana alivyosema.
And they said the magicians to Pharaoh [is] [the] finger of God it and it was strong [the] heart of Pharaoh and not he listened to them just as he had said Yahweh.
20 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi na usimame mbele ya Farao wakati anapokwenda mtoni nawe umwambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
And he said Yahweh to Moses rise early in the morning and present yourself before Pharaoh there! [he is] going out the water towards and you will say to him thus he says Yahweh let go people my so they may serve me.
21 Kama hutawaachia watu wangu waondoke nitakupelekea makundi ya mainzi juu yako, kwa maafisa wako, kwa watu wako na kwenye nyumba zenu. Nyumba za Wamisri zitajazwa mainzi, hata na ardhi yote ya Misri.
That except not you [are] letting go people my here I [am] about to send on you and on servants your and on people your and on houses your the swarm and they will be full [the] houses of Egypt the swarm and also the ground which they [are] on it.
22 “‘Lakini siku ile nitafanya kitu tofauti katika nchi ya Gosheni, ambapo watu wangu wanaishi, hapatakuwepo na makundi ya mainzi, ili mpate kujua kwamba Mimi, Bwana, niko katika nchi hii.
And I will separate on the day that [the] land of Goshen which people my [is] standing on it to not to be there a swarm so that you may know that I [am] Yahweh in [the] midst of the land.
23 Nitaweka tofauti kati ya watu wangu na watu wenu. Ishara hii ya ajabu itatokea kesho.’”
And I will make a ransom between people my and between people your to tomorrow it will happen the sign this.
24 Naye Bwana akafanya hivyo. Makundi makubwa ya mainzi yalimiminika katika jumba la kifalme la Farao na katika nyumba za maafisa wake, pia nchi yote ya Misri ikaharibiwa na mainzi.
And he did Yahweh so and it came a swarm massive [the] house of towards Pharaoh and [the] house of servants his and in all [the] land of Egypt it was ruined the land because of the swarm.
25 Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kuwaambia, “Nendeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu katika nchi hii.”
And he summoned Pharaoh Moses and Aaron and he said go sacrifice to God your in the land.
26 Lakini Mose akamwambia, “Hilo halitakuwa sawa. Dhabihu tutakazomtolea Bwana Mungu wetu zitakuwa chukizo kwa Wamisri. Kama tukitoa dhabihu ambazo ni chukizo mbele yao, je, hawatatupiga mawe?
And he said Moses not [is] established to do thus for [the] abomination of Egypt we will sacrifice to Yahweh God our here! we will sacrifice [the] abomination of Egypt to eyes their and not will they stone? us.
27 Ni lazima twende mwendo wa siku tatu mpaka tufike jangwani ili tumtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, kama alivyotuagiza.”
A journey of three days we will go in the wilderness and we will sacrifice to Yahweh God our just as he says to us.
28 Farao akamwambia, “Nitawaruhusu mwende kumtolea Bwana Mungu wenu dhabihu huko jangwani, lakini hamna ruhusa kwenda mbali sana. Sasa mniombee.”
And he said Pharaoh I I will let go you and you will sacrifice to Yahweh God your in the wilderness only certainly not you must be far away to go pray for me.
29 Mose akajibu, “Mara tu nitakapoondoka, nitamwomba Bwana na kesho mainzi yataondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake. Hakikisha tu kwamba Farao hatatenda kwa udanganyifu tena kwa kutokuwaachia watu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
And he said Moses here! I [am] about to go out from with you and I will pray to Yahweh and he will turn aside the swarm from Pharaoh from servants his and from people his tomorrow only may not he repeat Pharaoh to deceive to not to let go the people to sacrifice to Yahweh.
30 Ndipo Mose akamwacha Farao na kumwomba Bwana,
And he went out Moses from with Pharaoh and he prayed to Yahweh.
31 naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Mainzi yakaondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake, wala hakuna hata inzi aliyebakia.
And he did Yahweh according to [the] word of Moses and he turned aside the swarm from Pharaoh from servants his and from people his not it remained one.
32 Lakini wakati huu pia Farao akaushupaza moyo wake, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.
And he made heavy Pharaoh heart his also at the time this and not he let go the people.

< Kutoka 8 >