< Kutoka 8 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
Afterward the Lord sayde vnto Moses, Goe vnto Pharaoh, and tell him, Thus saith the Lord, Let my people goe, that they may serue me:
2 Kama ukikataa kuwaruhusu kuondoka, basi nitaipiga nchi yako yote kwa kuwaletea vyura.
And if thou wilt not let them goe, beholde, I will smite all thy countrey with frogges:
3 Mto Naili utafurika vyura. Watakuja kwenye jumba lako la kifalme na katika chumba chako cha kulala na kitandani mwako, katika nyumba za maafisa wako na kwa watu wako, vyura hao wataingia katika meko yenu na kwenye vyombo vya kukandia unga.
And the riuer shall scral ful of frogges, which shall goe vp and come into thine house, and into thy chamber, where thou sleepest, and vpon thy bed, and into the house of thy seruants, and vpon thy people, and into thine ouens, and into thy kneading troughes.
4 Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako na maafisa wako wote.’”
Yea, the frogges shall climbe vp vpon thee, and on thy people, and vpon all thy seruants.
5 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha mkono wako ukiwa na ile fimbo yako juu ya vijito, mifereji na madimbwi, fanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’”
Also the Lord said vnto Moses, Say thou vnto Aaron, Stretch out thine hande with thy rod vpon the streames, vpon the riuers, and vpon the ponds, and cause frogs to come vp vpon the land of Egypt.
6 Ndipo Aroni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, nao vyura wakatokea na kuifunika nchi.
Then Aaron stretched out his hand vpon the waters of Egypt, and the frogges came vp, and couered the land of Egypt.
7 Lakini waganga wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao, nao pia wakafanya vyura kuja juu ya nchi ya Misri.
And the sorcerers did likewise with their sorceries, and brought frogges vp vpon the land of Egypt.
8 Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kusema, “Mwombeni Bwana awaondoe vyura kutoka kwangu na kwa watu wangu, nami nitawaachia watu wenu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
Then Pharaoh called for Moses and Aaron, and said, Pray ye vnto the Lord, that hee may take away the frogges from mee, and from my people, and I will let the people goe, that they may doe sacrifice vnto the Lord.
9 Mose akamwambia Farao, “Ninakupa heshima ya kuamua ni wakati gani wa kukuombea wewe, maafisa wako na watu wako ili kwamba vyura watoke kwenu na kwenye nyumba zenu. Isipokuwa wale walio katika Mto Naili.”
And Moses said vnto Pharaoh, Concerning me, euen command when I shall pray for thee, and for thy seruants, and for thy people, to destroy the frogges from thee and from thine houses, that they may remaine in the riuer only.
10 Farao akasema, “Kesho.” Mose akamjibu, “Itakuwa kama unavyosema, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote kama Bwana Mungu wetu.
Then he said, To morowe. And he answered, Be it as thou hast said, that thou maiest know, that there is none like vnto the Lord our God.
11 Vyura wataondoka kwako na katika nyumba zako, kwa maafisa wako na kwa watu wako, ila watabakia katika Mto Naili tu.”
So the frogges shall depart from thee, and from thine houses, and from thy seruantes, and from thy people: onely they shall remaine in the riuer.
12 Baada ya Mose na Aroni kuondoka kwa Farao, Mose akamlilia Bwana kuhusu vyura aliokuwa amewaleta kwa Farao.
Then Moses and Aaron went out from Pharaoh: and Moses cryed vnto the Lord concerning the frogges, which hee had sent vnto Pharaoh.
13 Naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Vyura wakafia ndani ya nyumba, viwanjani na mashambani.
And the Lord did according to the saying of Moses: so the frogges died in the houses, in the townes, and in the fieldes.
14 Wakayakusanya malundo, nchi nzima ikanuka.
And they gathered the together by heaps, and the land stanke of them.
15 Lakini Farao alipoona pametokea nafuu, akaushupaza moyo wake na hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
But when Pharaoh sawe that hee had rest giuen him, he hardened his heart, and hearkened not vnto them, as the Lord had said.
16 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha fimbo yako uyapige mavumbi ya ardhi,’ nayo nchi yote ya Misri mavumbi yatakuwa viroboto.”
Againe the Lord sayd vnto Moses, Say vnto Aaron, Stretche out the rod, and smite the dust of the earth, that it may bee turned to lyce throughout all the land of Egypt.
17 Wakafanya hivyo, Aroni aliponyoosha mkono wake wenye fimbo na kuyapiga mavumbi ya nchi, viroboto wakawajia watu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi ya Misri yakawa viroboto.
And they did so: for Aaron stretched out his hand with his rod, and smote the dust of the earth: and lyce came vpon man and vpon beast: all the dust of the earth was lyce throughout all the land of Egypt.
18 Lakini waganga walipojaribu kutengeneza viroboto kwa siri ya uganga wao, hawakuweza. Nao viroboto walikuwa juu ya watu na wanyama.
Nowe the enchanters assaied likewise with their enchantments to bring forth lyce, but they could not. So the lyce were vpon man and vpon beast.
19 Waganga wale wakamwambia Farao, “Hiki ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ukawa mgumu naye hakuwasikiliza, kama vile Bwana alivyosema.
Then saide the enchanters vnto Pharaoh, This is the finger of God. But Pharaohs heart remained obstinate, and hee hearkened not vnto them, as the Lord had said.
20 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi na usimame mbele ya Farao wakati anapokwenda mtoni nawe umwambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
Moreouer the Lord sayd to Moses, Rise vp earely in the morning, and stand before Pharaoh (lo, hee will come forth vnto the water) and say vnto him, Thus saith the Lord, Let my people go, that they may serue me.
21 Kama hutawaachia watu wangu waondoke nitakupelekea makundi ya mainzi juu yako, kwa maafisa wako, kwa watu wako na kwenye nyumba zenu. Nyumba za Wamisri zitajazwa mainzi, hata na ardhi yote ya Misri.
Els, if thou wilt not let my people goe, behold, I will send swarmes of flies both vpon thee, and vpon thy seruants, and vpon thy people, and into thine houses: and the houses of the Egyptians shalbe full of swarmes of flies, and the ground also whereon they are.
22 “‘Lakini siku ile nitafanya kitu tofauti katika nchi ya Gosheni, ambapo watu wangu wanaishi, hapatakuwepo na makundi ya mainzi, ili mpate kujua kwamba Mimi, Bwana, niko katika nchi hii.
But ye land of Goshe, where my people are, wil I cause to be wonderfull in that day, so that no swarmes of flies shalbe there, that thou maiest know that I am the Lord in the middes of the earth.
23 Nitaweka tofauti kati ya watu wangu na watu wenu. Ishara hii ya ajabu itatokea kesho.’”
And I will make a deliuerance of my people from thy people: to morowe shall this miracle be.
24 Naye Bwana akafanya hivyo. Makundi makubwa ya mainzi yalimiminika katika jumba la kifalme la Farao na katika nyumba za maafisa wake, pia nchi yote ya Misri ikaharibiwa na mainzi.
And the Lord did so: for there came great swarmes of flies into the house of Pharaoh, and into his seruants houses, so that through all the lande of Egypt, the earth was corrupt by the swarmes of flies.
25 Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kuwaambia, “Nendeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu katika nchi hii.”
Then Pharaoh called for Moses and Aaron, and saide, Goe, doe sacrifice vnto your God in this lande.
26 Lakini Mose akamwambia, “Hilo halitakuwa sawa. Dhabihu tutakazomtolea Bwana Mungu wetu zitakuwa chukizo kwa Wamisri. Kama tukitoa dhabihu ambazo ni chukizo mbele yao, je, hawatatupiga mawe?
But Moses answered, It is not meete to do so: for then we shoulde offer vnto the Lord our God that, which is an abomination vnto the Egyptians. Loe, can we sacrifice the abomination of the Egyptians before their eyes, and they not stone vs?
27 Ni lazima twende mwendo wa siku tatu mpaka tufike jangwani ili tumtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, kama alivyotuagiza.”
Let vs go three dayes iourney in the desert, and sacrifice vnto the Lord our God, as he hath commanded vs.
28 Farao akamwambia, “Nitawaruhusu mwende kumtolea Bwana Mungu wenu dhabihu huko jangwani, lakini hamna ruhusa kwenda mbali sana. Sasa mniombee.”
And Pharaoh said, I will let you go, that ye may sacrifice vnto the Lord your God in the wildernesse: but goe not farre away, pray for me.
29 Mose akajibu, “Mara tu nitakapoondoka, nitamwomba Bwana na kesho mainzi yataondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake. Hakikisha tu kwamba Farao hatatenda kwa udanganyifu tena kwa kutokuwaachia watu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
And Moses said, Behold, I will go out from thee, and pray vnto the Lord, that the swarmes of flies may depart from Pharaoh, from his seruants, and from his people to morowe: but let Pharaoh from hencefoorth deceiue no more, in not suffering the people to sacrifice vnto the Lord.
30 Ndipo Mose akamwacha Farao na kumwomba Bwana,
So Moses went out from Pharaoh and prayed vnto the Lord.
31 naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Mainzi yakaondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake, wala hakuna hata inzi aliyebakia.
And the Lord did according to the saying of Moses, and the swarmes of flies departed from Pharaoh, from his seruants, and from his people, and there remained not one.
32 Lakini wakati huu pia Farao akaushupaza moyo wake, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.
Yet Pharaoh hardened his heart at this time also, and did not let the people goe.