< Kutoka 8 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
The Lord also said to Moses: “Enter to Pharaoh, and you will say to him: ‘Thus says the Lord: Release my people in order to sacrifice to me.
2 Kama ukikataa kuwaruhusu kuondoka, basi nitaipiga nchi yako yote kwa kuwaletea vyura.
But if you are not willing to release them, behold, I will strike all your coasts with frogs.
3 Mto Naili utafurika vyura. Watakuja kwenye jumba lako la kifalme na katika chumba chako cha kulala na kitandani mwako, katika nyumba za maafisa wako na kwa watu wako, vyura hao wataingia katika meko yenu na kwenye vyombo vya kukandia unga.
And the river will seethe with frogs, which will go up and enter into your house, and your bedroom, and upon your bed, and into the houses of your servants and your people, and into your ovens, and into the remains of your foods.
4 Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako na maafisa wako wote.’”
And to you, and to your people, and to all your servants, the frogs will enter.’”
5 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha mkono wako ukiwa na ile fimbo yako juu ya vijito, mifereji na madimbwi, fanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’”
And the Lord said to Moses: “Say to Aaron: ‘Extend your hand over the rivers, and also over the streams and the marshes, and bring forth frogs over the land of Egypt.’”
6 Ndipo Aroni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, nao vyura wakatokea na kuifunika nchi.
And Aaron extended his hand over the waters of Egypt, and the frogs came up and covered the land of Egypt.
7 Lakini waganga wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao, nao pia wakafanya vyura kuja juu ya nchi ya Misri.
Then the sorcerers also, by their incantations, did similarly, and they brought forth frogs upon the land of Egypt.
8 Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kusema, “Mwombeni Bwana awaondoe vyura kutoka kwangu na kwa watu wangu, nami nitawaachia watu wenu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
But Pharaoh called Moses and Aaron, and he said to them: “Pray to the Lord, so as to take away the frogs from me and from my people. And I will release the people, so as to sacrifice to the Lord.”
9 Mose akamwambia Farao, “Ninakupa heshima ya kuamua ni wakati gani wa kukuombea wewe, maafisa wako na watu wako ili kwamba vyura watoke kwenu na kwenye nyumba zenu. Isipokuwa wale walio katika Mto Naili.”
And Moses said to Pharaoh: “Appoint for me a time, when I should petition on behalf of you, and your servants, and your people, so that the frogs may be driven away from you, and from your house, and from your servants, and from your people, and so that they may remain only in the river.”
10 Farao akasema, “Kesho.” Mose akamjibu, “Itakuwa kama unavyosema, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote kama Bwana Mungu wetu.
And he responded, “Tomorrow.” Then he said, “I will act according to your word, so that you may know that there is no one like the Lord our God.
11 Vyura wataondoka kwako na katika nyumba zako, kwa maafisa wako na kwa watu wako, ila watabakia katika Mto Naili tu.”
And the frogs will withdraw from you, and from your house, and from your servants, and from your people. And they will remain only in the river.”
12 Baada ya Mose na Aroni kuondoka kwa Farao, Mose akamlilia Bwana kuhusu vyura aliokuwa amewaleta kwa Farao.
And Moses and Aaron departed from Pharaoh. And Moses cried out to the Lord on behalf of the promise that he had made to Pharaoh concerning the frogs.
13 Naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Vyura wakafia ndani ya nyumba, viwanjani na mashambani.
And the Lord acted according to the word of Moses. And the frogs died out of the houses, and out of the villages, and out of the fields.
14 Wakayakusanya malundo, nchi nzima ikanuka.
And they gathered them together into immense piles, and the land was polluted.
15 Lakini Farao alipoona pametokea nafuu, akaushupaza moyo wake na hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
Then Pharaoh, seeing that relief had been provided, hardened his own heart, and he did not listen to them, just as the Lord had instructed.
16 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha fimbo yako uyapige mavumbi ya ardhi,’ nayo nchi yote ya Misri mavumbi yatakuwa viroboto.”
And the Lord said to Moses: “Say to Aaron: ‘Extend your staff and strike the dust of the earth. And let there be stinging insects throughout the entire the land of Egypt.’”
17 Wakafanya hivyo, Aroni aliponyoosha mkono wake wenye fimbo na kuyapiga mavumbi ya nchi, viroboto wakawajia watu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi ya Misri yakawa viroboto.
And they did so. And Aaron extended his hand, holding the staff, and he struck the dust of the earth, and there came stinging insects upon men and upon beasts. All the dust of the earth was turned into stinging insects through all the land of Egypt.
18 Lakini waganga walipojaribu kutengeneza viroboto kwa siri ya uganga wao, hawakuweza. Nao viroboto walikuwa juu ya watu na wanyama.
And the sorcerers, with their incantations, did similarly, in order to bring forth stinging insects, but they were not able. And there were stinging insects, as much on men as on beasts.
19 Waganga wale wakamwambia Farao, “Hiki ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ukawa mgumu naye hakuwasikiliza, kama vile Bwana alivyosema.
And the sorcerers said to Pharaoh: “This is the finger of God.” And the heart of Pharaoh was hardened, and he did not listen to them, just as the Lord had instructed.
20 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi na usimame mbele ya Farao wakati anapokwenda mtoni nawe umwambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
The Lord also said to Moses: “Arise at first light, and stand in the sight of Pharaoh, for he will go out to the waters. And you will say to him: ‘Thus says the Lord: Release my people to sacrifice to me.
21 Kama hutawaachia watu wangu waondoke nitakupelekea makundi ya mainzi juu yako, kwa maafisa wako, kwa watu wako na kwenye nyumba zenu. Nyumba za Wamisri zitajazwa mainzi, hata na ardhi yote ya Misri.
But if you will not release them, behold, I will send upon you, and upon your servants, and upon your people, and into your houses, diverse kinds of flies. And the houses of the Egyptians will be filled with diverse kinds of flies, as well as the whole land in which they will be.
22 “‘Lakini siku ile nitafanya kitu tofauti katika nchi ya Gosheni, ambapo watu wangu wanaishi, hapatakuwepo na makundi ya mainzi, ili mpate kujua kwamba Mimi, Bwana, niko katika nchi hii.
And in that day, I will cause a miracle in the land of Goshen, where my people are, so that flies will not be there. And you will know that I am the Lord in the midst of the earth.
23 Nitaweka tofauti kati ya watu wangu na watu wenu. Ishara hii ya ajabu itatokea kesho.’”
And I will set a division between my people and your people. Tomorrow this sign will be.’”
24 Naye Bwana akafanya hivyo. Makundi makubwa ya mainzi yalimiminika katika jumba la kifalme la Farao na katika nyumba za maafisa wake, pia nchi yote ya Misri ikaharibiwa na mainzi.
And the Lord did so. And there came very grievous flies into the houses of Pharaoh and of his servants, and into all the land of Egypt. And the land was polluted, in this way, by the flies.
25 Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kuwaambia, “Nendeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu katika nchi hii.”
And Pharaoh called Moses and Aaron, and he said to them, “Go and sacrifice to your God in this land.”
26 Lakini Mose akamwambia, “Hilo halitakuwa sawa. Dhabihu tutakazomtolea Bwana Mungu wetu zitakuwa chukizo kwa Wamisri. Kama tukitoa dhabihu ambazo ni chukizo mbele yao, je, hawatatupiga mawe?
And Moses said: “It cannot be so. For we will immolate the abominations of the Egyptians to the Lord our God. For if we slaughter those things which the Egyptians worship, in their presence, they will stone us.
27 Ni lazima twende mwendo wa siku tatu mpaka tufike jangwani ili tumtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, kama alivyotuagiza.”
We will sojourn three days’ journey into the wilderness. And we will sacrifice to the Lord our God, just as he has instructed us.”
28 Farao akamwambia, “Nitawaruhusu mwende kumtolea Bwana Mungu wenu dhabihu huko jangwani, lakini hamna ruhusa kwenda mbali sana. Sasa mniombee.”
And Pharaoh said: “I will release you in order to sacrifice to the Lord your God in the desert. Yet you may only go so far. Petition for me.”
29 Mose akajibu, “Mara tu nitakapoondoka, nitamwomba Bwana na kesho mainzi yataondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake. Hakikisha tu kwamba Farao hatatenda kwa udanganyifu tena kwa kutokuwaachia watu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
And Moses said: “After departing from you, I will pray to the Lord. And the flies will withdraw from Pharaoh, and from his servants, and from his people, tomorrow. Yet do not be willing to deceive any longer, so that you would not release the people to sacrifice to the Lord.”
30 Ndipo Mose akamwacha Farao na kumwomba Bwana,
And Moses, departing from Pharaoh, prayed to the Lord.
31 naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Mainzi yakaondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake, wala hakuna hata inzi aliyebakia.
And he acted according to his word. And he took away the flies from Pharaoh, and from his servants, and from his people. There was not even one left behind.
32 Lakini wakati huu pia Farao akaushupaza moyo wake, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.
And the heart of Pharaoh was hardened, so that, even at this turn, he would not release the people.