< Kutoka 8 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
Amalalu, Hina Gode da Mousesema amane sia: i, “Felouma masa! Ema amane sia: ma, “Hina Gode da amane sia: sa, ‘Na dunu fi di gagui amo Nama nodone sia: ne gadomusa: fisidigima.
2 Kama ukikataa kuwaruhusu kuondoka, basi nitaipiga nchi yako yote kwa kuwaletea vyura.
Di da higasea, Na da dia sogega se iasimu. Soge huluane da guama amoga dedeboi dagoi ba: mu.
3 Mto Naili utafurika vyura. Watakuja kwenye jumba lako la kifalme na katika chumba chako cha kulala na kitandani mwako, katika nyumba za maafisa wako na kwa watu wako, vyura hao wataingia katika meko yenu na kwenye vyombo vya kukandia unga.
Naile Hano da guama amoga nabaidafa ba: mu. Amasea, guama da hano yolesili, dia diasu amola dia debea amoga heda: mu. Ilia da dia eagene ouligisu dunu amola ilia diasuga masunu. Amola ilia dilia ha: i manu ofodo amola gobele nasu amo ganodini ba: mu.
4 Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako na maafisa wako wote.’”
Ilia da di, dia fi dunu amola dia ouligisu dunu ilima soagala: le, fila heda: mu.
5 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha mkono wako ukiwa na ile fimbo yako juu ya vijito, mifereji na madimbwi, fanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’”
Hina Gode da Mousesema amane sia: i, “Di Elanema ea dagulu lale, hano amola hano logo amola hano wayabo huluane amo da: iya ea dagulu ligia gadoma: ne sia: ma. Guama da heda: le, Idibidi soge huluane dedeboma: ne sia: ma.”
6 Ndipo Aroni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, nao vyura wakatokea na kuifunika nchi.
Amalalu, Elane da ea dagulu hano da: iya ligia gadoi. Amola guama da heda: le, Idibidi soge huluane dedeboi.
7 Lakini waganga wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao, nao pia wakafanya vyura kuja juu ya nchi ya Misri.
Be Felou ea fefedoasu dawa: dunu da ilia hou hamobeba: le, guama da heda: i.
8 Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kusema, “Mwombeni Bwana awaondoe vyura kutoka kwangu na kwa watu wangu, nami nitawaachia watu wenu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
Felou da Mousese amola Elane misa: ne sia: i. E da elama amane sia: i, “Alia Hina Godema E da amo guama sefasima: ne sia: ne gadoma. Amasea, na da dia fi ilia da Godema gobele salasu hou hamoma: ne, logo doasimu.”
9 Mose akamwambia Farao, “Ninakupa heshima ya kuamua ni wakati gani wa kukuombea wewe, maafisa wako na watu wako ili kwamba vyura watoke kwenu na kwenye nyumba zenu. Isipokuwa wale walio katika Mto Naili.”
Mousese da bu adole i, “Na da di, dia ouligisu dunu amola dia fi dunu amo fidima: ne hahawane Godema sia: ne gadomu. Na sia: ne gadoma: ne, di eso ilegema. Amasea, guama huluane da fadegale, Naile Hano amo ganodini fawane guama ba: mu.”
10 Farao akasema, “Kesho.” Mose akamjibu, “Itakuwa kama unavyosema, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote kama Bwana Mungu wetu.
Felou da bu adole i, “Dia na fidima: ne, aya sia: ne gadoma!” Mousese da amane sia: i, “Dia adole ba: i defele na da hamomu. Amasea, ‘gode’ eno ninia Hina Gode defele da hamedafa gala, amo di da dawa: mu.
11 Vyura wataondoka kwako na katika nyumba zako, kwa maafisa wako na kwa watu wako, ila watabakia katika Mto Naili tu.”
Di, dia eagene ouligisu dunu amola dia fi huluane da guama afia: i dagoi ba: mu. Naile Hano ganodini fawane da guama ba: mu.
12 Baada ya Mose na Aroni kuondoka kwa Farao, Mose akamlilia Bwana kuhusu vyura aliokuwa amewaleta kwa Farao.
Amalalu, Mousese amola Elane da Felou yolesili, asili Hina Gode da guama sefasima: ne, Ema sia: ne gadoi.
13 Naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Vyura wakafia ndani ya nyumba, viwanjani na mashambani.
Hina Gode da Mousese ea sia: ne gadoi defele hamoi. Guama huluane diasu amola gagoi amola ifabi amo ganodini esafulu da bogogia: i dagoi.
14 Wakayakusanya malundo, nchi nzima ikanuka.
Idibidi dunu da guama bogoi amo gilisili ligisi biba heda: i dialu. Soge huluane da gaha bagade nabi.
15 Lakini Farao alipoona pametokea nafuu, akaushupaza moyo wake na hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
Be Felou da guama bogoi dagoi ba: beba: le, ea dogo da bu igi agoane hamoi. Hina Gode Ea sia: i defele, e da Mousese amola Elane ela sia: hame nabi.
16 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha fimbo yako uyapige mavumbi ya ardhi,’ nayo nchi yote ya Misri mavumbi yatakuwa viroboto.”
Hina Gode da Mousesema amane sia: i, “Di Elanema amane sia: ma. E da ea daguluga osoba fama. Amasea osobo su Idibidi soge huluane amo ganodini da afadenene mimini ba: mu.”
17 Wakafanya hivyo, Aroni aliponyoosha mkono wake wenye fimbo na kuyapiga mavumbi ya nchi, viroboto wakawajia watu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi ya Misri yakawa viroboto.
Amaiba: le, Elane da ea daguluga osobo fai. Osobo su Idibidi soge ganodini huluane da afadenene mimini hamoi. Ilia da dunu amola ohe fi amo da: iya fila heda: le dedeboi dagoi.
18 Lakini waganga walipojaribu kutengeneza viroboto kwa siri ya uganga wao, hawakuweza. Nao viroboto walikuwa juu ya watu na wanyama.
Idibidi fefedoasu dunu da gasa fili mimini hamomusa: hamonanu. Be hamedei. Mimini da bagohame soge huluane ganodini ba: i.
19 Waganga wale wakamwambia Farao, “Hiki ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ukawa mgumu naye hakuwasikiliza, kama vile Bwana alivyosema.
Idibidi fefedoasu dunu da Felouma amane sia: i, “Gode Hi da amo hou hamoi.” Be Felou ea dogo da ga: nasi hamoi. E da Hina Gode Ea sia: i defele, Mousese amola Elane ela sia: hame nabi.
20 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi na usimame mbele ya Farao wakati anapokwenda mtoni nawe umwambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
Hina Gode da Mousesema amane sia: i, “Hahabedafa, Felou da Naile Hano amoga ahoanumu. Di ema ba: la masa. Ema amane sia: ma, ‘Hina Gode da agoane sia: sa, Na fi dunu da Nama nodone sia: ne gadomusa: , di ili ga masa: ne fisidigima.
21 Kama hutawaachia watu wangu waondoke nitakupelekea makundi ya mainzi juu yako, kwa maafisa wako, kwa watu wako na kwenye nyumba zenu. Nyumba za Wamisri zitajazwa mainzi, hata na ardhi yote ya Misri.
Na da dima sisasa. Di da fisidigimu higasea, Na da dima se nabasu imunu. Na da fane dima amola dia eagene ouligisu dunuma amola dia fi dunu huluane ilima asunasimu. Idibidi dunu ilia diasu huluane da fane amoga nabai ba: mu. Amola Idibidi soge osobo huluane da fane amoga dedeboi dagoi ba: mu.
22 “‘Lakini siku ile nitafanya kitu tofauti katika nchi ya Gosheni, ambapo watu wangu wanaishi, hapatakuwepo na makundi ya mainzi, ili mpate kujua kwamba Mimi, Bwana, niko katika nchi hii.
Be Gousiene amo Na fi ilia esalebe soge amoga Na da fane hame asunasimu. Di da Na, Hina Gode, da amo hou hamonanebe dawa: ma: ne, Na da Na fi amola dia fi hisu ba: sa. Amo musa: hame ba: su hou da aya ba: mu.”
23 Nitaweka tofauti kati ya watu wangu na watu wenu. Ishara hii ya ajabu itatokea kesho.’”
24 Naye Bwana akafanya hivyo. Makundi makubwa ya mainzi yalimiminika katika jumba la kifalme la Farao na katika nyumba za maafisa wake, pia nchi yote ya Misri ikaharibiwa na mainzi.
Hina Gode da fane gilisisu bagohame amo Felou ea diasuga amola eagene ouligisu dunu ilia diasuga asunasi. Fane idimu hamedeidafa misiba: le, Idibidi soge huluane da gugunufinisi dagoi ba: i.
25 Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kuwaambia, “Nendeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu katika nchi hii.”
Amalalu, Felou da Mousese amola Elane ema misa: ne sia: i. E da elama amane sia: i, “Defea! Dilia Hina Godema gobele salasu hou hamoma: ne, Idibidi soge ganodini hamomusa: masa.”
26 Lakini Mose akamwambia, “Hilo halitakuwa sawa. Dhabihu tutakazomtolea Bwana Mungu wetu zitakuwa chukizo kwa Wamisri. Kama tukitoa dhabihu ambazo ni chukizo mbele yao, je, hawatatupiga mawe?
Be Mousese da bu adole i, “Agoane hamosea da moloi hame ba: mu. Ninia ohe fi amo gobele salasu hamoma: ne medole legesea, Idibidi dunu da higa: i ba: mu. Amo hou ninia Idibidi dunu ilia siga ba: ma: ne hamosea, ilia da amo hou higa: iba: le, nini igiga gala: le legemu.”
27 Ni lazima twende mwendo wa siku tatu mpaka tufike jangwani ili tumtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, kama alivyotuagiza.”
Logo afae fawane gala. Ninia da eso udiana amo wadela: i hafoga: i soge ganodini ga ahoasea, ninia Hina Gode Ea sia: defele, Ema gobele salasu hamomu.”
28 Farao akamwambia, “Nitawaruhusu mwende kumtolea Bwana Mungu wenu dhabihu huko jangwani, lakini hamna ruhusa kwenda mbali sana. Sasa mniombee.”
Felou da amane sia: i, “Defea! Dilia Hina Godema gobele salasu hamoma: ne, wadela: i hafoga: i sogega masunu da defea. Be sedagaga mae masa. Amola na fidima: ne Godema sia: ne gadoma.”
29 Mose akajibu, “Mara tu nitakapoondoka, nitamwomba Bwana na kesho mainzi yataondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake. Hakikisha tu kwamba Farao hatatenda kwa udanganyifu tena kwa kutokuwaachia watu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
Mousese da bu adole i, “Na da ga ahoasea, na da Hina Godema E da fane amo dima, dia eagene ouligisu dunuma amola dia fi huluane ilima fisili sefasima: ne sia: mu. Be di da ninia fi ilia Hina Godema gobele salasu hamoma: ne masunu logo damumusa: , ninima bu mae ogogoma.”
30 Ndipo Mose akamwacha Farao na kumwomba Bwana,
Mousese da Felou yolesili asili, Godema sia: ne gadoi.
31 naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Mainzi yakaondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake, wala hakuna hata inzi aliyebakia.
Amola Hina Gode da Mousese ea adole ba: su defele hamoi dagoi. Fane huluane da Felou, ea eagene ouligisu dunu amola ea fi dunu huluane yolesi dagoi. Fane afae esalebe da hamedafa ba: i.
32 Lakini wakati huu pia Farao akaushupaza moyo wake, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.
Be Felou da bu eno ea dogo ga: nasi hamoi. E da Isala: ili dunu ga fisili masa: ne hame fisidigi.

< Kutoka 8 >