< Kutoka 7 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
Le Seigneur dit, alors à Moïse: Voilà que je t'ai fait comme le Dieu du Pharaon; Aaron, ton frère, sera ton prophète.
2 Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
Tu diras à celui-ci tout ce que je te prescris; et Aaron, ton frère, dira au Pharaon de renvoyer de sa contrée les fils d'Israël.
3 Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
Cependant, j'endurcirai le cœur du Pharaon, puis, je multiplierai mes signes et mes prodiges en la terre d'Égypte.
4 hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
Le Pharaon ne vous écoutera pas, je ferai tomber ma main sur la terre d'Égypte, et, par ma puissance, j'en ferai sortir mon peuple, les fils d'Israël, après les avoir vengés d'une manière terrible.
5 Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
Et tous les Égyptiens connaîtront que je suis le Seigneur qui étends ma main sur la terre d'Égypte, et, du milieu de ce peuple, je ferai sortir les fils d'Israël.
6 Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
Et Moïse avec Aaron exécuta ce que le Seigneur leur avait prescrit; tous les deux obéirent.
7 Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
Moïse avait quatre-vingts ans, et Aaron, son frère, quatre-vingt-trois ans, lorsqu'ils parlèrent au Pharaon.
8 Bwana akamwambia Mose na Aroni,
Or, le Seigneur avait dit à Moïse et à son frère.
9 “Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
Si le Pharaon vous dit: Donnez-nous quelque signe, faites quelque prodige, tu diras à ton frère: Prends ta baguette, et jette-la à terre devant le Pharaon et ses serviteurs, et elle sera changée en serpent.
10 Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
Moïse entra donc avec Aaron devant le Pharaon et ses serviteurs, et ils firent ce que leur avait prescrit le Seigneur; Aaron jeta sa baguette devant le Pharaon et ses serviteurs, et elle fut changée en serpent.
11 Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
Alors, le Pharaon convoqua les sages et les magiciens de l'Égypte, et les magiciens de l'Égypte firent comme Aaron, en s'aidant de leurs sortilèges.
12 Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
Chacun d'eux jeta sa baguette, et les baguettes furent changées en serpents; mais la baguette d'Aaron dévora les leurs.
13 Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
Et le cœur du Pharaon s'endurcit; il n'écouta pas ceux qui lui firent connaître les ordres du Seigneur.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
Et le Seigneur dit à Moïse: Le cœur du Pharaon s'est endurci; il s'obstine à ne point renvoyer le peuple.
15 Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
Aborde le Pharaon dès le matin; il fait à cette heure sa promenade sur l'eau; tu l'attendras sur la rive du fleuve, et tu auras à la main la baguette qui a été changée en serpent.
16 Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
Et tu diras au Pharaon: Le Seigneur Dieu des Hébreux m'a envoyé à toi, disant: Renvoie mon peuple pour qu'il m'offre un sacrifice dans le désert; jusqu'à présent tu ne m’as point écouté.
17 Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
Or, voici ce que dit le Seigneur: À ce signe, tu connaîtras que je suis le Seigneur; voilà que je vais frapper de ma baguette l'eau du fleuve, et elle sera changée en sang.
18 Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
Les poissons du fleuve mourront, le fleuve lui-même deviendra fétide, et les Égyptiens ne pourront plus en boire les eaux.
19 Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
Le Seigneur dit encore à Moïse: Dis à ton frère Aaron: Prends à la main ta baguette, étends la main sur les eaux de l'Égypte, sur les bras du fleuve, sur les canaux, sur les marais, sur tout amas d'eau de la contrée; et les eaux seront changées en sang dans toute la terre d'Égypte, même dans les vases de bois et de pierre.
20 Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
Moïse et Aaron firent ce que Dieu leur avait ordonné; celui-ci, ayant levé sa baguette, frappa l'eau du fleuve devant le Pharaon et ses serviteurs, et toute l'eau du fleuve fut changée en sang,
21 Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
Les poissons du fleuve moururent, le fleuve devint fétide, et les Égyptiens ne purent boire de ses eaux, et il y eut du sang, sur toute la terre d'Égypte.
22 Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
Les magiciens de l'Égypte firent encore comme Aaron, en s’aidant de leurs sortilèges, et le cœur du Pharaon s'endurcit; il n'écouta ni Moïse ni son frère, ainsi que l'avait dit le Seigneur.
23 Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
Après cela, le Pharaon partit, il rentra en ses demeures, et il ne changea pas de pensées, même ayant vu ce prodige.
24 Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
Cependant, tous les Égyptiens creusèrent sur les bords du fleuve pour trouver de l'eau, mais ils ne purent boire de l'eau du fleuve.
25 Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.
Et sept jours se passèrent après que le Seigneur eut frappé le fleuve.

< Kutoka 7 >