< Kutoka 7 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
Yahvé dit à Moïse: « Voici, je t'ai établi comme Dieu auprès de Pharaon, et Aaron, ton frère, sera ton prophète.
2 Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
Tu diras tout ce que je t'ordonnerai, et Aaron, ton frère, parlera à Pharaon pour qu'il laisse aller les enfants d'Israël hors de son pays.
3 Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
J'endurcirai le cœur de Pharaon, et je multiplierai mes signes et mes prodiges dans le pays d'Égypte.
4 hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
Mais Pharaon ne t'écoutera pas. Je mettrai ma main sur l'Égypte, et je ferai sortir du pays d'Égypte mes armées, mon peuple, les enfants d'Israël, par de grands jugements.
5 Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
Les Égyptiens sauront que je suis Yahvé, quand j'étendrai ma main sur l'Égypte et que je ferai sortir du milieu d'eux les enfants d'Israël. »
6 Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
Moïse et Aaron firent ainsi. Ils firent ce que Yahvé leur avait ordonné.
7 Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
Moïse était âgé de quatre-vingts ans, et Aaron de quatre-vingt-trois ans, lorsqu'ils parlèrent à Pharaon.
8 Bwana akamwambia Mose na Aroni,
Yahvé parla à Moïse et à Aaron, et dit:
9 “Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
« Quand Pharaon vous dira: Fais un miracle, tu diras à Aaron: Prends ta verge, jette-la devant Pharaon, et elle deviendra un serpent ».
10 Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
Moïse et Aaron allèrent trouver Pharaon, et ils firent ce que Yahvé avait ordonné. Aaron jeta sa verge devant Pharaon et devant ses serviteurs, et elle devint un serpent.
11 Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
Alors Pharaon appela aussi les sages et les magiciens. Eux aussi, les magiciens d'Egypte, firent la même chose avec leurs enchantements.
12 Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
Ils jetèrent chacun leurs baguettes et elles devinrent des serpents; mais la baguette d'Aaron engloutit leurs baguettes.
13 Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
Le cœur de Pharaon s'endurcit et il ne les écouta pas, comme Yahvé l'avait dit.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
Yahvé dit à Moïse: « Le cœur de Pharaon est obstiné. Il refuse de laisser partir le peuple.
15 Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
Va voir Pharaon dès le matin. Voici qu'il sort vers l'eau. Tu te tiendras au bord du fleuve pour aller à sa rencontre. Tu prendras dans ta main le bâton qui s'est transformé en serpent.
16 Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
Tu lui diras: « Yahvé, le Dieu des Hébreux, m'a envoyé vers toi pour te dire: « Laisse aller mon peuple, afin qu'il me serve dans le désert. Voici, jusqu'à présent, vous n'avez pas écouté. »
17 Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
Yahvé dit: « A ceci vous saurez que je suis Yahvé. Voici: Je frapperai avec la verge qui est dans ma main sur les eaux qui sont dans le fleuve, et elles seront changées en sang.
18 Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
Les poissons qui sont dans le fleuve mourront et le fleuve deviendra fétide. Les Égyptiens auront horreur de boire de l'eau du fleuve. »'"
19 Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
Yahvé dit à Moïse: « Dis à Aaron: « Prends ta verge et étends ta main sur les eaux de l'Égypte, sur ses rivières, sur ses ruisseaux, sur ses étangs et sur tous ses bassins d'eau, afin qu'elles deviennent du sang. Il y aura du sang dans tout le pays d'Égypte, dans les vases de bois et dans les vases de pierre. »
20 Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
Moïse et Aaron firent ce que l'Éternel leur avait ordonné; ils levèrent la verge et frappèrent les eaux du fleuve, sous les yeux de Pharaon et de ses serviteurs, et toutes les eaux du fleuve se changèrent en sang.
21 Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
Les poissons qui étaient dans le fleuve moururent. Le fleuve devint fétide. Les Égyptiens ne pouvaient pas boire l'eau du fleuve. Le sang était dans tout le pays d'Égypte.
22 Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
Les magiciens d'Égypte firent la même chose avec leurs enchantements. Le cœur de Pharaon s'endurcit et il ne les écouta pas, comme Yahvé l'avait dit.
23 Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
Pharaon se retourna et entra dans sa maison, et il ne prit même pas cela à cœur.
24 Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
Tous les Égyptiens creusèrent autour du fleuve pour trouver de l'eau à boire, car ils ne pouvaient pas boire l'eau du fleuve.
25 Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.
Sept jours s'écoulèrent, après que Yahvé eut frappé le fleuve.

< Kutoka 7 >