< Kutoka 7 >
1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
And Jehovah said to Moses, See, I have made thee God to Pharaoh; and Aaron thy brother shall be thy prophet.
2 Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
Thou shalt speak all that I command thee; and Aaron thy brother shall speak unto Pharaoh, that he let the children of Israel go out of his land.
3 Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
And I will render Pharaoh's heart obdurate, and multiply my signs and my wonders in the land of Egypt.
4 hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
And Pharaoh will not hearken unto you; and I will lay my hand upon Egypt, and bring forth my hosts, my people, the children of Israel, out of the land of Egypt by great judgments.
5 Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
And the Egyptians shall know that I am Jehovah, when I stretch forth my hand on Egypt, and bring out the children of Israel from among them.
6 Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
And Moses and Aaron did as Jehovah had commanded them: so did they.
7 Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
And Moses was eighty years old, and Aaron was eighty-three years old, when they spoke to Pharaoh.
8 Bwana akamwambia Mose na Aroni,
And Jehovah spoke to Moses and to Aaron, saying,
9 “Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
When Pharaoh shall speak to you, saying, Do a miracle for yourselves, — then thou shalt say unto Aaron, Take thy staff and cast [it] before Pharaoh — it will become a serpent.
10 Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
And Moses and Aaron went in to Pharaoh, and did so, as Jehovah had commanded; and Aaron cast down his staff before Pharaoh, and before his bondmen, and it became a serpent.
11 Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
And Pharaoh also called the sages and the sorcerers; and they too, the scribes of Egypt, did so with their enchantments:
12 Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
they cast down every man his staff, and they became serpents; but Aaron's staff swallowed up their staves.
13 Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
And Pharaoh's heart was stubborn, and he hearkened not to them, as Jehovah had said.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
And Jehovah said to Moses, Pharaoh's heart is hardened: he refuseth to let the people go.
15 Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
Go unto Pharaoh in the morning — behold, he will go out unto the water — and take thy stand by the bank of the river in front of him; and take in thy hand the staff that was turned into a serpent.
16 Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
And say unto him, Jehovah the God of the Hebrews has sent me to thee, saying, Let my people go, that they may serve me in the wilderness; but behold, hitherto thou hast not hearkened.
17 Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
Thus saith Jehovah: In this shalt thou know that I am Jehovah — behold, I will smite with the staff that is in my hand upon the water which is in the river, and it shall be turned into blood.
18 Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
And the fish that is in the river shall die; and the river shall stink; and the Egyptians shall loathe to drink the water out of the river.
19 Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
And Jehovah said to Moses, Say unto Aaron, Take thy staff, and stretch out thy hand upon the waters of the Egyptians — upon their streams, upon their rivers, and upon their ponds, and upon all their reservoirs of water, that they may become blood; and there shall be blood throughout the land of Egypt, both in [vessels of] wood and in [vessels of] stone.
20 Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
And Moses and Aaron did so, as Jehovah had commanded; and he lifted up the staff, and smote the waters that were in the river before the eyes of Pharaoh, and before the eyes of his bondmen; and all the waters that were in the river were turned into blood.
21 Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
And the fish that was in the river died; and the river stank, and the Egyptians could not drink the water of the river; and the blood was throughout the land of Egypt.
22 Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
And the scribes of Egypt did so with their sorceries; and Pharaoh's heart was stubborn, neither did he hearken to them, as Jehovah had said.
23 Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
And Pharaoh turned and went into his house, and took not this to heart either.
24 Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
And all the Egyptians dug round about the river for water to drink; for they could not drink of the water of the river.
25 Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.
And seven days were fulfilled, after Jehovah had smitten the river.