< Kutoka 7 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
And the Lord said to Moses, See I have made you a god to Pharaoh, and Aaron your brother will be your prophet.
2 Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
Say whatever I give you orders to say: and Aaron your brother will give word to Pharaoh to let the children of Israel go out of his land.
3 Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
And I will make Pharaoh's heart hard, and my signs and wonders will be increased in the land of Egypt.
4 hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
But Pharaoh will not give ear to you, and I will put my hand on Egypt, and take my armies, my people, the children of Israel, out of Egypt, after great punishments.
5 Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
And the Egyptians will see that I am the Lord, when my hand is stretched out over Egypt, and I take the children of Israel out from among them.
6 Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
And Moses and Aaron did so: as the Lord gave them orders, so they did.
7 Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
And Moses was eighty years old, and Aaron eighty-three years old, when they gave the Lord's word to Pharaoh.
8 Bwana akamwambia Mose na Aroni,
And the Lord said to Moses and Aaron,
9 “Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
If Pharaoh says to you, Let me see a wonder: then say to Aaron, Take your rod and put it down on the earth before Pharaoh so that it may become a snake.
10 Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
Then Moses and Aaron went in to Pharaoh and they did as the Lord had said: and Aaron put his rod down on the earth before Pharaoh and his servants, and it became a snake.
11 Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
Then Pharaoh sent for the wise men and the wonder-workers, and they, the wonder-workers of Egypt, did the same with their secret arts.
12 Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
For every one of them put down his rod on the earth, and they became snakes: but Aaron's rod made a meal of their rods.
13 Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
But Pharaoh's heart was made hard, and he did not give ear to them, as the Lord had said.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
And the Lord said to Moses and Aaron, Pharaoh's heart is unchanged; he will not let the people go.
15 Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
Go to Pharaoh in the morning; when he goes out to the water, you will be waiting for him by the edge of the Nile, with the rod which was turned into a snake in your hand;
16 Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
And say to him, The Lord, the God of the Hebrews, has sent me to you, saying, Let my people go so that they may give me worship in the waste land; but up to now you have not given ear to his words.
17 Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
So the Lord says, By this you may be certain that I am the Lord; see, by the touch of this rod in my hand the waters of the Nile will be turned to blood;
18 Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
And the fish in the Nile will come to destruction, and the river will send up a bad smell, and the Egyptians will not be able, for disgust, to make use of the water of the Nile for drinking.
19 Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
And the Lord said, Say to Aaron, Let the rod in your hand be stretched out over the waters of Egypt, and over the rivers and the streams and the pools, and over every stretch of water, so that they may be turned to blood; and there will be blood through all the land of Egypt, in vessels of wood and in vessels of stone.
20 Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
And Moses and Aaron did as the Lord had said; and when his rod had been lifted up and stretched out over the waters of the Nile before the eyes of Pharaoh and his servants, all the water in the Nile was turned to blood;
21 Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
And the fish in the Nile came to destruction, and a bad smell went up from the river, and the Egyptians were not able to make use of the water of the Nile for drinking; and there was blood through all the land of Egypt.
22 Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
And the wonder-workers of Egypt did the same with their secret arts: but Pharaoh's heart was made hard, and he would not give ear to them, as the Lord had said.
23 Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
Then Pharaoh went into his house, and did not take even this to heart.
24 Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
And all the Egyptians made holes round about the Nile to get drinking-water, for they were not able to make use of the Nile water.
25 Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.
And seven days went past, after the Lord had put his hand on the Nile.

< Kutoka 7 >