< Kutoka 6 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”
Wtedy PAN powiedział do Mojżesza: Teraz zobaczysz, co uczynię faraonowi. Mocną ręką bowiem wypuści ich i mocną ręką wypędzi ich ze swojej ziemi.
2 Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana.
Nadto Bóg mówił do Mojżesza: Ja jestem PANEM.
3 Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.
Objawiłem się Abrahamowi, Izaakowi i Jakubowi [pod tym imieniem]: Bóg Wszechmogący, ale z mojego imienia JEHOWA nie byłem przez nich poznany.
4 Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.
Ustanowiłem też z nimi moje przymierze, aby dać im ziemię Kanaan, ziemię ich pielgrzymowania, w której przebywali jako obcy.
5 Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.
Usłyszałem także jęk synów Izraela, których Egipcjanie trzymają w niewoli, i wspomniałem na moje przymierze.
6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.
Dlatego powiedz synom Izraela: Ja jestem PAN, wyprowadzę was spod ciężarów Egipcjan, wyrwę was z ich niewoli i wybawię was wyciągniętym ramieniem i przez wielkie sądy.
7 Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.
Wezmę was sobie za lud i będę wam Bogiem. Poznacie, że ja jestem PAN, wasz Bóg, który was wyprowadza spod ciężarów Egipcjan.
8 Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’”
I wprowadzę was do ziemi, którą przysiągłem dać Abrahamowi, Izaakowi i Jakubowi; i dam ją wam w dziedzictwo. Ja [jestem] PAN.
9 Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.
I Mojżesz mówił tak do synów Izraela, ale nie usłuchali go z powodu udręki ducha i ciężkiej niewoli.
10 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
Wtedy PAN powiedział do Mojżesza:
11 “Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”
Idź, powiedz faraonowi, królowi Egiptu, żeby wypuścił synów Izraela ze swej ziemi.
12 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”
Mojżesz zaś odpowiedział przed PANEM: Oto synowie Izraela nie posłuchali mnie, jakże więc posłucha mnie faraon? Jestem przecież nieobrzezanych warg.
13 Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.
Wtedy PAN przemówił do Mojżesza i Aarona i dał im rozkaz dla synów Izraela i dla faraona, króla Egiptu, aby wyprowadzili synów Izraela z ziemi Egiptu.
14 Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.
Oto naczelnicy domów ich ojców: synowie Rubena, pierworodnego Izraela: Henoch, Pallu, Chesron i Karmi. To są rodziny Rubena.
15 Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.
Synowie Symeona: Jemuel, Jamin, Ohad, Jakin, Sochar i Szaul, syn Kananejki. To są rodziny Symeona.
16 Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.
Oto imiona synów Lewiego według ich pokoleń: Gerszon, Kehat i Merari. A lat życia Lewiego [było] sto trzydzieści siedem.
17 Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.
Synowie Gerszona: Libni i Szimei, według ich rodzin.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.
Synowie Kehata: Amram, Ishar, Chebron i Uzziel. A lat życia Kehata [było] sto trzydzieści trzy.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.
Synowie Merariego: Machli i Muszi. To są rodziny Lewiego według ich pokoleń.
20 Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
I Amram pojął za żonę Jokebed, swoją ciotkę, która urodziła mu Aarona i Mojżesza. A lat życia Amrama [było] sto trzydzieści siedem.
21 Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.
Synowie Ishara: Korach, Nefeg i Zikri.
22 Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.
Synowie Uzziela: Miszael, Elsafan i Sitri.
23 Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
I Aaron pojął za żonę Eliszebę, córkę Aminadaba, siostrę Nachszona. Ona mu urodziła Nadaba, Abihu, Eleazara i Itamara.
24 Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.
A synowie Koracha: Assir, Elkana i Abiasaf. To są rodziny Korachitów.
25 Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.
I Eleazar, syn Aarona, pojął za żonę jedną z córek Putiela. Ona mu urodziła Pinchasa. Oto [są] naczelnicy ojców Lewitów według ich rodzin.
26 Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”
To [są] ci właśnie Aaron i Mojżesz, do których mówił PAN: Wyprowadźcie synów Izraela z ziemi Egiptu według ich zastępów.
27 Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.
To oni mówili do faraona, króla Egiptu, aby wyprowadzić synów Izraela z Egiptu. [To jest] właśnie Mojżesz i Aaron.
28 Bwana aliponena na Mose huko Misri,
A w tym dniu, kiedy PAN mówił do Mojżesza w ziemi Egiptu;
29 akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”
PAN powiedział do niego: Ja jestem PAN. Mów do faraona, króla Egiptu, wszystko, co do ciebie mówię.
30 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”
Mojżesz zaś odpowiedział przed PANEM: Oto jestem nieobrzezanych warg, jakże posłucha mnie faraon?

< Kutoka 6 >