< Kutoka 6 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”
Le Seigneur dit à Moïse: C’est maintenant que tu verras ce que je vais faire à Pharaon; car par l’effet d’une main puissante il les laissera aller, et en vertu d’une main forte, il les pressera de sortir de son pays.
2 Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana.
Le Seigneur parla encore à Moïse, disant: Je suis le Seigneur,
3 Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.
Qui ai apparu à Abraham, à Isaac et à Jacob en Dieu tout-puissant; mais mon nom Adonaï, je ne le leur ai pas manifesté.
4 Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.
Et j’ai fait alliance avec eux, afin de leur donner la terre de Chanaan, terre de leur pèlerinage dans laquelle ils ont été étrangers.
5 Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.
J’ai entendu le gémissement des enfants d’Israël, que les Egyptiens ont opprimés; et je me suis souvenu de mon alliance.
6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.
C’est pourquoi dis aux enfants d’Israël: Je suis le Seigneur qui vous tirerai de la prison des Egyptiens, et vous délivrerai de la servitude: et je vous rachèterai par un bras élevé et de grands jugements.
7 Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.
Et je vous prendrai pour mon peuple, et je serai votre Dieu; ainsi vous saurez que c’est moi, qui suis le Seigneur votre Dieu, qui vous aurai tirés de la prison des Egyptiens,
8 Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’”
Et fait entrer dans la terre, sur laquelle j’ai levé la main, jurant que je la donnerais à Abraham, à Isaac et à Jacob; car je vous la donnerai en possession, moi le Seigneur.
9 Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.
Moïse raconta donc toutes ces choses aux enfants d’Israël, qui ne l’écoutèrent pas à cause de l’angoisse de leur esprit et de leur travail très pénible.
10 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
Et le Seigneur parla à Moïse, disant:
11 “Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”
Entre, et parle à Pharaon, roi d’Egypte, pour qu’il laisse sortir les enfants d’Israël de son pays.
12 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”
Moïse répondit devant le Seigneur: Voilà que les enfants d’Israël ne m’écoutent pas: et comment Pharaon m’écoutera-t-il, surtout moi étant incirconcis des lèvres?
13 Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.
C’est ainsi que le Seigneur parla à Moïse et Aaron et qu’il leur donna ses ordres pour les enfants d’Israël et pour Pharaon, roi d’Egypte, afin qu’ils fissent sortir les enfants d’Israël de la terre d’Egypte.
14 Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.
Voici les chefs des maisons selon leurs familles: Les fils de Ruben, premier-né d’Israël: Hénoch et Phallu, Hesron et Charmi:
15 Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.
C’est là la parenté de Ruben. Les fils de Siméon: Jamuel, Jamin, Ahod, Jachin, Soar et Saül, fils d’une Chananéenne. C’est là la race de Siméon.
16 Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.
Et voici les noms des fils de Lévi, selon leur parenté: Gerson, Caath et Mérari. Or les années de la vie de Lévi furent cent trente-sept.
17 Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.
Les fils de Gerson: Lobni et Séméi, selon leur parenté.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.
Les fils de Caath: Amram-Isaar, Hébron et Oziel: et les années de la vie de Caath furent cent trente-trois.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.
Les fils de Mérari: Moholi et Musi: c’est là la parenté de Lévi selon ses familles.
20 Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
Or Amram prit pour femme Jochabed, fille de son oncle paternel, laquelle lui enfanta Aaron et Moïse. Et les années de la vie d’Amram furent cent trente-sept.
21 Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.
Les fils d’Isaar: Coré, Nepheg et Zéchri.
22 Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.
Les fils d’Oziel: Misaël, Elisaphan et Séthri
23 Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Or Aaron prit pour femme Elisabeth, fille d’Aminadab, sœur de Nahasson, laquelle lui enfanta Nadab, Abiu, Eléazar et Ithamar.
24 Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.
Les fils de Coré: Aser, Elcana, et Abiasaph: c’est là la parenté des Corites.
25 Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.
Mais Eléazar, fils d’Aaron, prit une femme d’entre les filles le Phutiel, laquelle lui enfanta Phinéès. Ce sont là les chefs des familles lévitiques selon leur parenté.
26 Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”
C’est Aaron et Moïse auxquels le Seigneur commanda de retirer les enfants d’Israël de l’Egypte, selon leurs bandes.
27 Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.
Ce sont eux qui parlent à Pharaon, roi d’Egypte, pour qu’ils retirent les enfants d’Israël de l’Egypte: c’est Moïse et Aaron,
28 Bwana aliponena na Mose huko Misri,
Au jour où le Seigneur parla à Moïse dans la terre d’Egypte.
29 akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”
Et le Seigneur parla à Moïse, disant: Je suis le Seigneur; dis à Pharaon, roi d’Egypte, tout ce que moi-même je te dis.
30 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”
Et Moïse répondit devant le Seigneur: Voici que je suis incirconcis des lèvres, comment Pharaon m’écoutera-t-il?

< Kutoka 6 >