< Kutoka 6 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”
Yahvé dit à Moïse: « Tu verras maintenant ce que je ferai à Pharaon, car c'est à main forte qu'il les laissera aller, et c'est à main forte qu'il les chassera de son pays. »
2 Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana.
Dieu parla à Moïse, et lui dit: « Je suis Yahvé.
3 Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.
J'ai apparu à Abraham, à Isaac et à Jacob, en tant que Dieu tout-puissant, mais je ne leur ai pas été connu sous mon nom de Yahvé.
4 Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.
J'ai aussi établi mon alliance avec eux, pour leur donner le pays de Canaan, le pays de leurs voyages, dans lequel ils vivaient comme des étrangers.
5 Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.
J'ai entendu les gémissements des enfants d'Israël, que les Égyptiens tiennent en esclavage, et je me suis souvenu de mon alliance.
6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.
C'est pourquoi dis aux enfants d'Israël: « Je suis Yahvé, et je vous ferai sortir de dessous les fardeaux des Égyptiens, je vous délivrerai de leur servitude, je vous rachèterai à bras étendu et par de grands jugements.
7 Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.
Je vous prendrai pour mon peuple. Je serai votre Dieu, et vous saurez que je suis Yahvé, votre Dieu, qui vous fait sortir de dessous les fardeaux des Égyptiens.
8 Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’”
Je vous ferai entrer dans le pays que j'ai juré de donner à Abraham, à Isaac et à Jacob, et je vous le donnerai en héritage: je suis Yahvé.'"
9 Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.
Moïse en parla aux enfants d'Israël, mais ils n'écoutèrent pas Moïse, à cause de l'angoisse de l'esprit et de la cruelle servitude.
10 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
Yahvé parla à Moïse et dit:
11 “Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”
« Va, parle à Pharaon, roi d'Égypte, pour qu'il laisse sortir les enfants d'Israël de son pays. »
12 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”
Moïse parla devant Yahvé, et dit: « Voici, les enfants d'Israël ne m'ont pas écouté. Comment Pharaon m'écoutera-t-il, alors que j'ai des lèvres incirconcises? »
13 Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.
Yahvé parla à Moïse et à Aaron, et leur donna l'ordre de faire sortir du pays d'Égypte les enfants d'Israël et Pharaon, roi d'Égypte.
14 Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.
Voici les chefs des maisons de leurs pères. Fils de Ruben, premier-né d'Israël: Hanoch, Pallu, Hetsron et Carmi. Ce sont là les familles de Ruben.
15 Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.
Fils de Siméon: Jemuel, Jamin, Ohad, Jachin, Zohar et Saül, fils d'une Cananéenne: ce sont là les familles de Siméon.
16 Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.
Voici les noms des fils de Lévi, selon leurs générations: Guerschon, Kehath et Merari. Les années de la vie de Lévi furent de cent trente-sept ans.
17 Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.
Fils de Guerschon: Libni et Schimeï, selon leurs familles.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.
Fils de Kehath: Amram, Jitsehar, Hébron et Uzziel. Les années de la vie de Kehath furent de cent trente-trois ans.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.
Fils de Merari: Mahli et Mushi. Ce sont là les familles des Lévites, selon leurs générations.
20 Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
Amram prit pour femme Jochebed, la sœur de son père, et elle lui enfanta Aaron et Moïse. Les années de la vie d'Amram furent de cent trente-sept ans.
21 Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.
Fils de Jitsehar: Koré, Néphég, et Zicri.
22 Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.
Fils d'Uzziel: Mishaël, Elzaphan et Sithri.
23 Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Aaron prit pour femme Elischéba, fille d'Amminadab, sœur de Nachshon; elle lui enfanta Nadab et Abihu, Eléazar et Ithamar.
24 Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.
Fils de Koré: Assir, Elkana et Abiasaph; ce sont là les familles des Koréens.
25 Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.
Le fils d'Eléazar Aaron prit pour femme une des filles de Putiel, qui lui enfanta Phinées. Ce sont là les chefs des maisons paternelles des Lévites, selon leurs familles.
26 Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”
Ce sont ces Aaron et Moïse à qui Yahvé a dit: « Fais sortir du pays d'Égypte les enfants d'Israël, selon leurs armées. »
27 Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.
Ce sont eux qui ont parlé à Pharaon, roi d'Égypte, pour faire sortir d'Égypte les enfants d'Israël. Ce sont ces Moïse et Aaron.
28 Bwana aliponena na Mose huko Misri,
Le jour où Yahvé parla à Moïse au pays d'Égypte,
29 akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”
Yahvé dit à Moïse: « Je suis Yahvé. Dis à Pharaon, roi d'Égypte, tout ce que je te dirai. »
30 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”
Moïse dit devant Yahvé: « Voici, je suis d'une bouche incirconcise, et comment Pharaon m'écouterait-il? »

< Kutoka 6 >