< Kutoka 6 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”
Then the LORD said to Moses, Now shalt thou see what I will do to Pharaoh; for with a strong hand shall he let them go, and with a strong hand shall he drive them from his land.
2 Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana.
And God spoke to Moses, and said to him, I [am] the LORD:
3 Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.
And I appeared to Abraham, to Isaac, and to Jacob, by [the name of] God Almighty, but by my name JEHOVAH was I not known to them.
4 Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.
And I have also established my covenant with them, to give them the land of Canaan, the land of their pilgrimage, in which they were strangers.
5 Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.
And I have also heard the groaning of the children of Israel, whom the Egyptians keep in bondage: and I have remembered my covenant.
6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.
Wherefore say to the children of Israel, I [am] the LORD, and I will bring you from under the burdens of the Egyptians, and I will deliver you from their bondage, and I will redeem you with out-stretched arm, and with great judgments:
7 Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.
And I will take you to me for a people, and I will be to you a God: and ye shall know that I [am] the LORD your God, who bringeth you out from under the burdens of the Egyptians.
8 Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’”
And I will bring you into the land, concerning which I swore to give it to Abraham, to Isaac, and to Jacob; and I will give it to you for a heritage: I [am] the LORD.
9 Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.
And Moses spoke so to the children of Israel: but they hearkened not to Moses, by reason of anguish of spirit, and cruel bondage.
10 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke to Moses, saying,
11 “Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”
Go in, speak to Pharaoh, king of Egypt, that he let the children of Israel depart from his land.
12 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”
And Moses spoke before the LORD, saying, Behold, the children of Israel have not hearkened to me; how then shall Pharaoh hear me, who [am] of uncircumcised lips?
13 Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.
And the LORD spoke to Moses, and to Aaron, and gave them a charge to the children of Israel, and to Pharaoh, king of Egypt, to bring the children of Israel out of the land of Egypt.
14 Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.
These [are] the heads of their father's houses: The sons of Reuben the first-born of Israel; Hanoch, and Pallu, Hezron, and Carmi: these [are] the families of Reuben.
15 Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.
And the sons of Simeon; Jemuel, and Jamin, and Ohad, and Jachin, and Zohar, and Shaul the son of a Canaanitish woman: these [are] the families of Simeon.
16 Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.
And these [are] the names of the sons of Levi, according to their generations; Gershon, and Kohath, and Merari. And the years of the life of Levi [were] a hundred and thirty-seven years.
17 Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.
The sons of Gershon; Libni, and Shimi, according to their families.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.
And the sons of Kohath; Amram, and Izhar, and Hebron, and Uzziel: and the years of the life of Kohath [were] a hundred and thirty-three years.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.
And the sons of Merari; Mahali and Mushi: these [are] the families of Levi, according to their generations.
20 Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
And Amram took him Jochebed, his father's sister, for a wife; and she bore him Aaron and Moses. And the years of the life of Amram [were] a hundred and thirty-seven years.
21 Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.
And the sons of Izhar; Korah, and Nepheg, and Zichri.
22 Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.
And the sons of Uzziel; Mishael, and Elzaphan, and Zithri.
23 Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
And Aaron took him Elisheba daughter of Amminadab, sister of Naashon, for a wife; and she bore him Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
24 Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.
And the sons of Korah; Assir, and Elkanah, and Abiasaph: these [are] the families of the Korhites.
25 Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.
And Eleazar, Aaron's son, took him [one] of the daughters of Putiel for a wife; and she bore to him Phinehas: these [are] the heads of the fathers of the Levites, according to their families.
26 Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”
These [are] that Aaron and Moses, to whom the LORD said, Bring out the children of Israel from the land of Egypt according to their armies.
27 Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.
These [are] they who spoke to Pharaoh, king of Egypt, to bring out the children of Israel from Egypt: these [are] that Moses and Aaron.
28 Bwana aliponena na Mose huko Misri,
And it came to pass, on the day [when] the LORD spoke to Moses in the land of Egypt,
29 akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”
That the LORD spoke to Moses, saying, I [am] the LORD: speak thou to Pharaoh, king of Egypt, all that I say to thee.
30 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”
And Moses said before the LORD, Behold, I [am] of uncircumcised lips, and how shall Pharaoh hearken to me?

< Kutoka 6 >