< Kutoka 6 >
1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”
And YHWH says to Moses, “Now you see that which I do to Pharaoh, for with a strong hand he sends them away, indeed, with a strong hand he casts them out of his land.”
2 Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana.
And God speaks to Moses and says to him, “I [am] YHWH,
3 Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.
and I appear to Abraham, to Isaac, and to Jacob, as God Almighty; as for My Name YHWH, I have not been known to them;
4 Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.
and I have also established My covenant with them, to give the land of Canaan to them, the land of their sojournings, wherein they have sojourned;
5 Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.
and I have also heard the groaning of the sons of Israel, whom the Egyptians are causing to serve, and I remember My covenant.
6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.
Therefore say to the sons of Israel: I [am] YHWH, and I have brought you out from under the burdens of the Egyptians, and have delivered you from their service, and have redeemed you by an outstretched arm, and by great judgments,
7 Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.
and have taken you to Myself for a people, and I have been to you for God, and you have known that I [am] your God YHWH, who is bringing you out from under the burdens of the Egyptians;
8 Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’”
and I have brought you to the land which I have lifted up My hand to give it to Abraham, to Isaac, and to Jacob, and have given it to you—a possession; I [am] YHWH.”
9 Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.
And Moses speaks so to the sons of Israel, and they did not listen to Moses, for anguish of spirit, and for harsh service.
10 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
And YHWH speaks to Moses, saying,
11 “Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”
“Go in, speak to Pharaoh king of Egypt, and he sends the sons of Israel out of his land”;
12 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”
and Moses speaks before YHWH, saying, “Behold, the sons of Israel have not listened to me, and how does Pharaoh hear me, and I of uncircumcised lips?”
13 Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.
And YHWH speaks to Moses and to Aaron, and charges them for the sons of Israel, and for Pharaoh king of Egypt, to bring out the sons of Israel from the land of Egypt.
14 Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.
These [are] heads of the house of their fathers. Sons of Reuben firstborn of Israel: Enoch, and Phallu, Hezron, and Carmi; these [are] families of Reuben.
15 Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.
And sons of Simeon: Jemuel, and Jamin, and Ohad, and Jachin, and Zohar, and Shaul, son of the Canaanite; these [are] families of Simeon.
16 Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.
And these [are] the names of the sons of Levi, as to their births: Gershon, and Kohath, and Merari; and the years of the life of Levi [are] one hundred and thirty-seven years.
17 Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.
The sons of Gershon: Libni and Shimi, as to their families.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.
And the sons of Kohath: Amram, and Izhar, and Hebron, and Uzziel; and the years of the life of Kohath [are] one hundred and thirty-three years.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.
And the sons of Merari: Mahli and Mushi; these [are] families of Levi, as to their births.
20 Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
And Amram takes his aunt Jochebed to himself for a wife, and she bears Aaron and Moses to him; and the years of the life of Amram [are] one hundred and thirty-seven years.
21 Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.
And sons of Izhar: Korah, and Nepheg, and Zichri.
22 Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.
And sons of Uzziel: Mishael, and Elzaphan, and Sithri.
23 Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
And Aaron takes Elisheba daughter of Amminadab, sister of Naashon, to himself for a wife, and she bears to him Nadab, and Abihu, Eleazar, and Ithamar.
24 Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.
And sons of Korah: Assir, and Elkanah, and Abiasaph; these [are] families of the Korahite.
25 Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.
And Eleazar, Aaron’s son, has taken to himself [one] of the daughters of Putiel for a wife for himself, and she bears Phinehas to him; these [are] heads of the fathers of the Levites, as to their families.
26 Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”
This [is] Aaron—and Moses—to whom YHWH said, “Bring out the sons of Israel from the land of Egypt, by their hosts”;
27 Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.
these are they who are speaking to Pharaoh king of Egypt, to bring out the sons of Israel from Egypt, this [is] Moses—and Aaron.
28 Bwana aliponena na Mose huko Misri,
And it comes to pass in the day of YHWH’s speaking to Moses in the land of Egypt,
29 akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”
that YHWH speaks to Moses, saying, “I [am] YHWH, speak to Pharaoh king of Egypt all that I am speaking to you.”
30 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”
And Moses says before YHWH, “Behold, I [am] of uncircumcised lips, and how does Pharaoh listen to me?”