< Kutoka 6 >
1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”
But the Lord told Moses, “Now you'll see what I'm going to do to Pharaoh. Using my great strength I will force him to let them go; because of my power he will send them out from his country.”
2 Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana.
God spoke to Moses and told him, “I am Yahweh!
3 Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.
I revealed myself as God Almighty to Abraham, to Isaac, and to Jacob, but they didn't know my name, ‘Yahweh.’
4 Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.
I also confirmed my solemn agreement with them to give them the land of Canaan, the country where they were living as foreigners.
5 Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.
In addition I've heard the groans of the Israelites that the Egyptians are treating as slaves, and I haven't forgotten the agreement I promised them.
6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.
So tell the Israelites, ‘I am the Lord and I will save you from the forced labor the Egyptians are making you do; I will set you free from being their slaves. I will rescue you using my power and imposing heavy punishments.
7 Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.
I will make you my own people. Then you will know that I am the Lord your God, who rescued you from slavery in Egypt.
8 Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’”
I will take you to the land that I solemnly promised to give to Abraham, Isaac, and Jacob. I will give it to you to own. I am the Lord!’”
9 Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.
Moses explained this to the Israelites but they did not listen to him, because they were so discouraged and because of the hard labor they were forced to do.
10 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
Then the Lord said to Moses,
11 “Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”
“Go and speak to Pharaoh, king of Egypt. Tell him to let the Israelites leave his country.”
12 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”
But Moses replied, “Even my own people don't listen to me. Why would Pharaoh listen to me, especially since I'm such a poor speaker?”
13 Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.
But the Lord spoke to Moses and Aaron, and told them what to do regarding the people of Israel and Pharaoh, king of Egypt, in order to bring the Israelites out of Egypt.
14 Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.
These were the Israelite family heads. The sons of Reuben, the firstborn son of Israel, were Hanok and Pallu, Hezron and Karmi. These were the families of Reuben.
15 Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.
The sons of Simeon were Jemuel, Jamin, Ohad, Jachin, Zohar, and Shaul, (the son of a Canaanite woman). These were the families of Simeon.
16 Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.
These were the names of the sons of Levi according to their genealogical records: Gershon, Kohath, and Merari. Levi lived for 137 years.
17 Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.
The sons of Gershon, by families, were Libni and Shimei.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.
The sons of Kohath were Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel. Kohath lived for 133 years.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.
The sons of Merari were Mahli and Mushi. These were the families of the Levites according to their genealogical records.
20 Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
Amram married his father's sister Jochebed, and she had their sons Aaron and Moses. Amram lived for 137 years.
21 Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.
The sons of Izhar were Korah, Nepheg, and Zichri.
22 Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.
The sons of Uzziel were Mishael, Elzaphan, and Sithri.
23 Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Aaron married Elisheba, daughter of Amminadab and sister of Nahshon. She had their sons Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
24 Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.
The sons of Korah were Assir, Elkanah, and Abiasaph. These were the Korahite families.
25 Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.
Eleazar, son of Aaron, married one of the daughters of Putiel, and she had their son Phinehas. These are the ancestors of the Levite families, listed according to their clans. Eleazar son of Aaron married one of the daughters of Putiel, and she gave birth to his son, Phinehas. These are the heads of the Levite families, listed by family.
26 Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”
Aaron and Moses mentioned here are the ones the Lord told, “Lead the Israelites out of Egypt, divided up in their respective tribes.”
27 Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.
Moses and Aaron were also the ones who went to speak with Pharaoh, king of Egypt, about the Israelites leaving Egypt.
28 Bwana aliponena na Mose huko Misri,
When the Lord spoke to Moses in Egypt,
29 akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”
he said to him, “I am the Lord. Tell Pharaoh, king of Egypt, all that I tell you.”
30 Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”
But Moses replied, “I'm not a good speaker—why would Pharaoh listen to me?”