< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Entonces Yavé habló a Moisés:
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
El primer día del mes primero ordenarás levantar el Tabernáculo de Reunión.
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
Pondrás allí el Arca del Testimonio y la ocultarás con el velo.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
Introducirás la mesa, arreglarás sus utensilios, pondrás el candelabro y mandarás encender sus lámparas.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
Luego pondrás el altar de oro para el incienso frente al Arca del Testimonio, y pondrás la cortina en la entrada del Tabernáculo.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
Pondrás el altar del holocausto después de la entrada al Tabernáculo de Reunión.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
Pondrás la fuente entre la entrada al Tabernáculo de Reunión y el altar, y echarás agua en ella.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
Arreglarás el patio alrededor, y colgarás la cortina de la entrada al patio.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
Tomarás el aceite de la unción y ungirás el Tabernáculo y todo lo que hay en él. Así lo consagrarás junto con todos sus utensilios, y será sagrado.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
Ungirás también el altar del holocausto y todos sus utensilios, y santificarás el altar. El altar será santísimo.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
También ungirás la fuente y su basa y la consagrarás.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
En seguida ordenarás que Aarón y sus hijos se acerquen a la entrada del Tabernáculo de Reunión, y los lavarás con agua.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
Vestirás a Aarón las ropas sagradas, lo ungirás y lo consagrarás para que sea mi sacerdote.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
Ordenarás que se acerquen sus hijos, les pondrás las túnicas
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
y los ungirás como ungiste a su padre. Serán mis sacerdotes. Su unción les servirá como sacerdocio perpetuo para sus generaciones.
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
Moisés hizo conforme a todo lo que Yavé le ordenó. Así lo hizo.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
Aconteció que el Tabernáculo fue levantado el primer día del primer mes del segundo año.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
Moisés ordenó levantar el Tabernáculo. Asentó sus basas, puso sus tablones, metió sus travesaños y ordenó levantar sus columnas.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
Extendió la tienda sobre el Tabernáculo, y puso el cobertor de la tienda encima de él, como Yavé ordenó a Moisés.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
Después tomó el Testimonio y lo puso dentro del Arca, colocó las varas en el Arca y puso el Propiciatorio encima del Arca.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
Introdujo el Arca en el Tabernáculo, y puso el velo de separación. De este modo ocultó el Arca del Testimonio, como Yavé ordenó a Moisés.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
Luego puso la mesa en el Tabernáculo de Reunión, al lado norte del Tabernáculo, fuera del velo,
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
y puso en orden sobre ella los panes delante de Yavé, como Yavé ordenó a Moisés.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
Luego puso el candelabro en el Tabernáculo de Reunión enfrente de la mesa, al lado sur del Tabernáculo,
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
y ordenó encender las lámparas delante de Yavé, como Yavé ordenó a Moisés.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
Luego puso el altar de oro dentro del Tabernáculo de Reunión delante del velo,
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
y quemó incienso aromático sobre él, como Yavé ordenó a Moisés.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
Puso también la cortina en la entrada al Tabernáculo,
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
puso el altar del holocausto en la entrada del Tabernáculo de Reunión y ofreció holocausto y ofrenda vegetal sobre él, como Yavé ordenó a Moisés.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
Después colocó la fuente entre la entrada al Tabernáculo de Reunión y el altar, y puso allí agua para lavarse.
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
Moisés y Aarón y sus hijos se lavaban sus manos y sus pies en ella.
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Siempre se lavaban cuando entraban en el Tabernáculo de Reunión y al acercarse al altar, como Yavé ordenó a Moisés.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
Finalmente, hizo levantar el patio alrededor del Tabernáculo y del altar y puso la cortina en la entrada del patio. Así acabó Moisés la obra.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Entonces la nube cubrió el Tabernáculo de Reunión y la gloria de Yavé llenó el Tabernáculo.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Moisés no podía entrar en el Tabernáculo de Reunión, porque la nube estaba sobre él y la gloria de Yavé llenó el Tabernáculo.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
Cuando la nube se levantaba de sobre el Tabernáculo, los hijos de Israel salían en todas sus jornadas,
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
pero si la nube no se levantaba, no salían hasta el día cuando se levantaba,
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
porque la nube de Yavé permanecía de día sobre el Tabernáculo, y de noche había fuego en él, a la vista de toda la casa de Israel.

< Kutoka 40 >