< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
»Na prvi dan prvega meseca boš postavil šotorsko svetišče skupnosti.
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
Vanj boš postavil skrinjo pričevanja in skrinjo pokril z zagrinjalom.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
Prinesel boš mizo in uredil stvari, ki naj bi bile razvrščene na njej, in vanj boš prinesel svečnik ter prižgal njegove svetilke.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
Postavil boš oltar iz zlata za kadilo pred skrinjo pričevanja in k vratom šotorskega svetišča obesil tanko preprogo.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
Postavil boš oltar žgalne daritve pred vrati šotorskega svetišča shodnega šotora.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
[Okrogel] umivalnik boš postavil med shodni šotor in oltar in vanj boš dal vodo.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
Napravil boš dvor naokoli in pri velikih vratih dvora obesil tanko preprogo.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
Vzel boš mazilno olje in mazilil šotorsko svetišče in vse, kar je v njem in ga posvetil in vse njegove posode in to bo sveto.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
Mazilil boš oltar žgalne daritve in vse njegove posode in oltar posvéti. To bo oltar, najsvetejše.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
Mazilil boš [okrogel] umivalnik in njegovo vznožje in ga posvétil.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
Arona in njegove sinove boš privedel k vratom šotorskega svetišča skupnosti in jih umil z vodo.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
Na Arona boš nadel sveta oblačila in mazili ga in posvéti ga, da mi bo lahko služil v duhovniški službi«.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
Privedel boš njegove sinove in jih oblekel s plašči.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
Mazilil jih boš, kakor si mazilil njihovega očeta, da mi bodo lahko služili v duhovniški službi, kajti njihovo maziljenje bo zagotovo večno duhovništvo skozi njihove rodove.«
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
Tako je Mojzes storil. Glede na vse, kar mu je Gospod zapovedal, tako je storil.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
Pripetilo se je v prvem mesecu, v drugem letu, na prvi dan meseca, da je bilo šotorsko svetišče vzdignjeno.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
Mojzes je vzdignil šotorsko svetišče, privezal njegove podstavke, postavil njegove deske, vstavil njegove zapahe in vzdignil njegove stebre.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
In šotor je razprostrl nad šotorskim svetiščem, in nad njim postavil pokrivalo šotora; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
Vzel je pričevanje, ga položil v skrinjo, drogova namestil na skrinjo in na skrinjo položil sedež milosti.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
Skrinjo je prinesel v šotorsko svetišče in obesil zagrinjalo pokrivala ter pokril skrinjo pričevanja; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
Mizo je položil v shodni šotor, proti severni strani šotorskega svetišča, zunaj zagrinjala.
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
Na njej je urejeno položil kruh pred Gospodom; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
Svečnik je postavil v shodni šotor, nasproti mizi, na strani šotorskega svetišča proti jugu.
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
Pred Gospodom je prižgal svetilke; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
Zlati oltar je postavil v shodnem šotoru pred zagrinjalom
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
in na njem je zažgal dišeče kadilo; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
Pri vratih šotorskega svetišča je obesil tanko preprogo.
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
Pri vratih šotorskega svetišča shodnega šotora je postavil oltar žgalne daritve in na njem daroval žgalno daritev in jedilno daritev; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
Med shodni šotor in oltar je postavil [okrogel] umivalnik in vanj dal vodo, da se z njo umiva.
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
Mojzes, Aron in njegovi sinovi so tam umivali svoje roke in svoja stopala.
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Ko so odhajali v shodni šotor in ko so prihajali bliže k oltarju, so se umili; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
Dvor je uredil naokoli šotorskega svetišča in oltarja in obesil tanko preprogo velikih dvornih vrat. Tako je Mojzes končal delo.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Potem je oblak pokril shodni šotor in Gospodova slava je napolnila šotorsko svetišče.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Mojzes pa ni bil zmožen vstopiti v shodni šotor, ker je na njem vztrajal oblak in Gospodova slava je napolnila šotorsko svetišče.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
Ko je bil oblak dvignjen iznad šotorskega svetišča, so Izraelovi otroci odšli naprej po vseh svojih poteh,
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
toda če oblak ni bil dvignjen, potem niso potovali do dneva, ko je bil dvignjen gor.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
Kajti Gospodov oblak je bil nad šotorskim svetiščem podnevi, ogenj pa je bil na njem ponoči, v očeh vse Izraelove hiše, na vseh njihovih poteh.

< Kutoka 40 >