< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
آنگاه خداوند به موسی فرمود:
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
«در نخستین روز ماه اول، خیمهٔ ملاقات را بر پا کن
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
و صندوق عهد را که ده فرمان در آن قرار دارد، در داخل خیمه بگذار و پردهٔ مخصوص را جلوی آن آویزان کن.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
سپس میز را در خیمه بگذار و لوازمش را روی آن قرار بده. چراغدان را نیز در خیمه بگذار و چراغهایش را روشن کن.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
«مذبح طلا را برای سوزاندن بخور روبروی صندوق عهد بگذار. پردهٔ مدخل خیمه را بیاویز.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
مذبح قربانی سوختنی را مقابل مدخل خیمۀ ملاقات بگذار.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
حوض را بین خیمهٔ ملاقات و مذبح قرار بده و آن را پر از آب کن.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
دیوار پرده‌ای حیاط اطراف خیمه را بر پا نما و پردهٔ مدخل حیاط را آویزان کن.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
«روغن مسح را بردار و خیمه و تمام لوازم و وسایل آن را مسح کرده، تقدیس نما تا مقدّس شوند.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
سپس مذبح قربانی سوختنی و وسایل آن را مسح نموده، تقدیس کن و مذبح، جایگاه بسیار مقدّسی خواهد شد.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
بعد، حوض و پایه‌اش را مسح نموده، تقدیس کن.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
«سپس هارون و پسرانش را کنار مدخل خیمهٔ ملاقات بیاور و آنها را با آب شستشو بده.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
لباس مقدّس را بر هارون بپوشان و او را مسح کرده تقدیس نما تا در مقام کاهنی مرا خدمت کند.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
سپس پسرانش را بیاور و لباسهایشان را به ایشان بپوشان.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
آنها را نیز مانند پدرشان مسح کن تا در مقام کاهنی مرا خدمت کنند. این مسح به منزلهٔ انتخاب ابدی آنها و نسلهای ایشان است به مقام کاهنی.»
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
موسی هر چه را که خداوند به او فرموده بود بجا آورد.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
در نخستین روز ماه اول سال دوم، بعد از بیرون آمدن از مصر، خیمهٔ عبادت بر پا شد.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
موسی خیمهٔ عبادت را به این ترتیب بر پا کرد: اول پایه‌های آن را گذاشت، سپس تخته‌های چوب‌بست را در پایه‌ها نهاده، پشت‌بندهای آنها را نصب کرد و ستونها را بر پا نمود.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
آنگاه، همان‌طور که خداوند فرموده بود، پوشش داخلی سقف را روی چوبها کشید و پوششهای خارجی را روی آن گسترانید.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
بعد، دو لوح سنگی را که ده فرمان خدا روی آنها نوشته بود در صندوق عهد گذاشت و چوبهای حامل را درون حلقه‌ها قرار داد و سرپوش صندوق را که «تخت رحمت» بود، روی آن نهاد.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
آنگاه صندوق عهد را به درون خیمهٔ عبادت برد و پردهٔ مخصوص را جلو آن کشید، درست همان‌گونه که خداوند فرموده بود.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
سپس موسی میز را در سمت شمالی خیمهٔ ملاقات، بیرون پرده گذاشت،
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
و همان‌طور که خداوند به او فرموده بود، نان حضور را روی میز در حضور خداوند قرار داد.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
چراغدان را مقابل میز در سمت جنوبی خیمۀ ملاقات گذاشت
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
و مطابق دستور خداوند چراغهای چراغدان را در حضور خداوند روشن کرد.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
مذبح طلا را در خیمۀ ملاقات، بیرون پرده گذاشت
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
و مطابق دستور خداوند بر آن بخور معطر سوزاند.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
موسی پردهٔ مدخل خیمهٔ عبادت را آویزان کرد.
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
مذبح قربانی سوختنی را مقابل مدخل خیمۀ ملاقات گذاشت و روی آن قربانی سوختنی و هدیه آردی تقدیم کرد، درست همان‌طور که خداوند فرموده بود.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
حوض را بین خیمهٔ ملاقات و مذبح قرار داد و آن را پر از آب کرد.
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
موسی، هارون و پسرانش از آن آب برای شستن دست و پایشان استفاده می‌کردند.
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
آنها هر وقت می‌خواستند به داخل خیمۀ ملاقات بروند و یا به مذبح نزدیک شوند، مطابق دستور خداوند خود را می‌شستند.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
موسی دیوار پرده‌ای دور خیمه و مذبح را بر پا نموده پردهٔ مدخل حیاط را آویزان کرد. به این ترتیب او همهٔ کار را به پایان رسانید.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
آنگاه ابر، خیمهٔ ملاقات را پوشانید و حضور پرجلال خداوند آن را پر ساخت.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
موسی نتوانست وارد خیمۀ ملاقات شود، زیرا ابر بر آن نشسته بود و حضور پرجلال خداوند خیمۀ عبادت را پر ساخته بود.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
از آن پس، هر وقت ابر از روی خیمه برمی‌خاست قوم اسرائیل کوچ می‌کردند و به راهنمایی آن به سفر ادامه می‌دادند.
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
اما تا وقتی که ابر روی خیمه باقی بود، قوم همچنان در جای خود می‌ماندند.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
در روز، ابر روی خیمهٔ عبادت قرار داشت و در شب، آتش در ابر پدیدار می‌شد و قوم می‌توانستند آن را ببینند. به این طریق، ابر خداوند بنی‌اسرائیل را در تمام سفرهایشان هدایت می‌کرد.

< Kutoka 40 >