< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
locutusque est Dominus ad Mosen dicens
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
mense primo die prima mensis eriges tabernaculum testimonii
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
et pones in eo arcam dimittesque ante illam velum
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
et inlata mensa pones super eam quae rite praecepta sunt candelabrum stabit cum lucernis suis
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
et altare aureum in quo adoletur incensum coram arca testimonii tentorium in introitu tabernaculi pones
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
et ante illud altare holocausti
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
labrum inter altare et tabernaculum quod implebis aqua
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
circumdabisque atrium tentoriis et ingressum eius
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
et adsumpto unctionis oleo ungues tabernaculum cum vasis suis ut sanctificentur
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
altare holocausti et omnia vasa eius
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
labrum cum basi sua omnia unctionis oleo consecrabis ut sint sancta sanctorum
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
adplicabisque Aaron et filios eius ad fores tabernaculi testimonii et lotos aqua
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
indues sanctis vestibus ut ministrent mihi et unctio eorum in sacerdotium proficiat sempiternum
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
fecitque Moses omnia quae praeceperat Dominus
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
igitur mense primo anni secundi in prima die mensis conlocatum est tabernaculum
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
erexitque illud Moses et posuit tabulas ac bases et vectes statuitque columnas
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
et expandit tectum super tabernaculum inposito desuper operimento sicut Dominus imperarat
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
posuit et testimonium in arca subditis infra vectibus et oraculum desuper
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
cumque intulisset arcam in tabernaculum adpendit ante eam velum ut expleret Domini iussionem
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
posuit et mensam in tabernaculo testimonii ad plagam septentrionalem extra velum
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
ordinatis coram propositionis panibus sicut praeceperat Dominus Mosi
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
posuit et candelabrum in tabernaculum testimonii e regione mensae in parte australi
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
locatis per ordinem lucernis iuxta praeceptum Domini
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
posuit et altare aureum sub tecto testimonii contra velum
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
et adolevit super eo incensum aromatum sicut iusserat Dominus
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
posuit et tentorium in introitu tabernaculi
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
et altare holocausti in vestibulo testimonii offerens in eo holocaustum et sacrificia ut Dominus imperarat
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
labrum quoque statuit inter tabernaculum testimonii et altare implens illud aqua
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
laveruntque Moses et Aaron ac filii eius manus suas et pedes
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
cum ingrederentur tectum foederis et accederent ad altare sicut praeceperat Dominus
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
erexit et atrium per gyrum tabernaculi et altaris ducto in introitu eius tentorio postquam cuncta perfecta sunt
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
operuit nubes tabernaculum testimonii et gloria Domini implevit illud
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
nec poterat Moses ingredi tectum foederis nube operiente omnia et maiestate Domini coruscante quia cuncta nubes operuerat
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
si quando nubes tabernaculum deserebat proficiscebantur filii Israhel per turmas suas
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
si pendebat desuper manebant in eodem loco
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
nubes quippe Domini incubabat per diem tabernaculo et ignis in nocte videntibus populis Israhel per cunctas mansiones suas

< Kutoka 40 >