< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
וידבר יהוה אל משה לאמר׃
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
ביום החדש הראשון באחד לחדש תקים את משכן אהל מועד׃
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
ושמת שם את ארון העדות וסכת על הארן את הפרכת׃
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
והבאת את השלחן וערכת את ערכו והבאת את המנרה והעלית את נרתיה׃
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
ונתתה את מזבח הזהב לקטרת לפני ארון העדת ושמת את מסך הפתח למשכן׃
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
ונתתה את מזבח העלה לפני פתח משכן אהל מועד׃
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
ונתת את הכיר בין אהל מועד ובין המזבח ונתת שם מים׃
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
ושמת את החצר סביב ונתת את מסך שער החצר׃
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
ולקחת את שמן המשחה ומשחת את המשכן ואת כל אשר בו וקדשת אתו ואת כל כליו והיה קדש׃
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
ומשחת את מזבח העלה ואת כל כליו וקדשת את המזבח והיה המזבח קדש קדשים׃
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
ומשחת את הכיר ואת כנו וקדשת אתו׃
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
והקרבת את אהרן ואת בניו אל פתח אהל מועד ורחצת אתם במים׃
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
והלבשת את אהרן את בגדי הקדש ומשחת אתו וקדשת אתו וכהן לי׃
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
ואת בניו תקריב והלבשת אתם כתנת׃
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
ומשחת אתם כאשר משחת את אביהם וכהנו לי והיתה להית להם משחתם לכהנת עולם לדרתם׃
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
ויעש משה ככל אשר צוה יהוה אתו כן עשה׃
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
ויהי בחדש הראשון בשנה השנית באחד לחדש הוקם המשכן׃
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
ויקם משה את המשכן ויתן את אדניו וישם את קרשיו ויתן את בריחיו ויקם את עמודיו׃
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
ויפרש את האהל על המשכן וישם את מכסה האהל עליו מלמעלה כאשר צוה יהוה את משה׃
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
ויקח ויתן את העדת אל הארן וישם את הבדים על הארן ויתן את הכפרת על הארן מלמעלה׃
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
ויבא את הארן אל המשכן וישם את פרכת המסך ויסך על ארון העדות כאשר צוה יהוה את משה׃
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
ויתן את השלחן באהל מועד על ירך המשכן צפנה מחוץ לפרכת׃
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
ויערך עליו ערך לחם לפני יהוה כאשר צוה יהוה את משה׃
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
וישם את המנרה באהל מועד נכח השלחן על ירך המשכן נגבה׃
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
ויעל הנרת לפני יהוה כאשר צוה יהוה את משה׃
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
וישם את מזבח הזהב באהל מועד לפני הפרכת׃
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
ויקטר עליו קטרת סמים כאשר צוה יהוה את משה׃
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
וישם את מסך הפתח למשכן׃
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
ואת מזבח העלה שם פתח משכן אהל מועד ויעל עליו את העלה ואת המנחה כאשר צוה יהוה את משה׃
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
וישם את הכיר בין אהל מועד ובין המזבח ויתן שמה מים לרחצה׃
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
ורחצו ממנו משה ואהרן ובניו את ידיהם ואת רגליהם׃
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
בבאם אל אהל מועד ובקרבתם אל המזבח ירחצו כאשר צוה יהוה את משה׃
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
ויקם את החצר סביב למשכן ולמזבח ויתן את מסך שער החצר ויכל משה את המלאכה׃
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
ויכס הענן את אהל מועד וכבוד יהוה מלא את המשכן׃
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
ולא יכל משה לבוא אל אהל מועד כי שכן עליו הענן וכבוד יהוה מלא את המשכן׃
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
ובהעלות הענן מעל המשכן יסעו בני ישראל בכל מסעיהם׃
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
ואם לא יעלה הענן ולא יסעו עד יום העלתו׃
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
כי ענן יהוה על המשכן יומם ואש תהיה לילה בו לעיני כל בית ישראל בכל מסעיהם׃

< Kutoka 40 >