< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Et l'Éternel parla à Moïse en ces mots:
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
A l'époque du premier mois, le premier jour du mois, tu élèveras la Résidence de la Tente du Rendez-vous.
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
Et tu y placeras l'Arche du Témoignage et tu voileras l'Arche avec le Rideau.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
Et tu y introduiras la Table et en arrangeras le couvert, puis le Candélabre que tu garniras de ses lampes.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
Et tu mettras l'Autel d'or pour l'encensement devant l'Arche du Témoignage, et tu suspendras le Rideau à la porte de la Résidence.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
Et tu placeras l'Autel des holocaustes devant l'entrée de la Résidence de la Tente du Rendez-vous.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
Et tu placeras le Bassin entre la Tente du Rendez-vous et l'Autel, et tu y mettras de l'eau.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
Et tu dresseras le Parvis à l'entour, et tu suspendras le Rideau à la porte du Parvis.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
Et tu prendras l'Huile d'onction et tu oindras la Résidence et tout ce qu'elle renferme, et tu la consacreras avec tous ses meubles, afin qu'elle soit sacrée.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
Et tu oindras l'Autel des holocaustes et tous ses ustensiles, et tu consacreras l'Autel afin que l'Autel soit souverainement saint.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
Et tu oindras le Bassin et son support et le consacreras.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
Et tu amèneras Aaron et ses fils à l'entrée de la Tente du Rendez-vous et tu feras leur ablution avec de l'eau.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
Et tu revêtiras Aaron des vêtements sacrés,
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
et tu l'oindras et le consacreras pour qu'il me serve dans le sacerdoce.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
Et tu feras approcher ses fils, et tu les revêtiras des tuniques, et tu les oindras comme tu auras oint leur père afin qu'ils me servent dans le sacerdoce, de telle sorte que leur onction leur confère le sacerdoce à perpétuité pour leurs générations futures.
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
Et Moïse se conforma à tous les ordres que l'Éternel lui donnait: ainsi fit-il.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
Et le premier mois de la seconde année, le premier jour du mois, la Résidence fut élevée.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
Et Moïse éleva la Résidence et en posa les soubassements et en plaça les ais et y mit leurs traverses et en dressa les colonnes.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
Et il étendit la tente par-dessus la Résidence, et en haut par-dessus la tente il plaça la couverture, comme l'Éternel l'avait ordonné à Moïse.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
Et prenant le Témoignage, il le mit dans l'Arche, et munit l'Arche de ses barres, et il plaça le Propitiatoire sur le haut de l'Arche,
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
et il introduisit l'Arche dans la Résidence, et suspendit le Rideau, et il voila l'Arche du Témoignage, comme l'Éternel l'avait ordonné à Moïse.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
Et il dressa la Table dans la Tente du Rendez-vous au côté nord de la Résidence en dehors du rideau,
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
et il y arrangea un couvert de pain devant l'Éternel, comme l'Éternel l'avait ordonnée Moïse.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
Et il plaça le Candélabre dans la Tente du Rendez-vous vis-à-vis de la Table au côté sud de la Résidence,
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
et il fixa les lampes devant l'Éternel, comme l'Éternel l'avait ordonné à Moïse.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
Et il plaça l'Autel d'or dans la Tente du Rendez-vous devant le Rideau,
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
et y fit fumer de l'encens odorant, comme l'Éternel l'avait ordonné à Moïse.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
Et il suspendit le Rideau à l'entrée de la Résidence,
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
et il dressa l'Autel des holocaustes à l'entrée de la Résidence de la Tente du Rendez-vous, et y offrit les holocaustes et les offrandes, comme l'Éternel l'avait ordonné à Moïse.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
Et il plaça le Bassin entre la Tente du Rendez-vous et l'Autel, et il y mit de l'eau pour les ablutions,
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
et Moïse et Aaron et ses fils s'y lavèrent les mains et les pieds;
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
au moment de pénétrer dans la Tente du Rendez-vous et de s'approcher de l'Autel ils firent ces ablutions, comme l'Éternel l'avait ordonné à Moïse.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
Et il éleva le Parvis autour de la Résidence et de l'Autel, et fixa le rideau à la porte du Parvis: et ainsi Moïse acheva l'ouvrage.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Alors la nue couvrit la Tente du Rendez-vous, et la gloire de l'Éternel remplit la Résidence.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Et Moïse ne put pénétrer dans la Tente du Rendez-vous, car la nue séjournait sur elle, et la gloire de l'Éternel remplissait la Résidence.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
Et lorsque la nue se levait de dessus la Résidence, les enfants d'Israël levaient le camp dans tous leurs campements.
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
Et quand la nue ne se retirait pas, ils ne levaient pas le camp qu'elle ne se fût retirée.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
Car de jour la nue de l'Éternel couvrait la Résidence et de nuit il y avait un feu, et c'est ce que vit toute la maison d'Israël durant toute sa migration.

< Kutoka 40 >